"Iringa hakuna ngoma !!"

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
MKOA WAREJESHA sh.milioni 300 bila kutumia

Katika hali ya kushangaza na isiyo ya kawaida hata kidogo, Halmashauri za Wilaya Saba za Mkoa wa Iringa zimeshindwa kutumia zaidi ya shilingi milioni Milioni miatatu (300) zilizotolewa na mradi wa Tunajali, kwa ajili ya huduma ya matunzo na matibabu kwa watu wenye virusi vya UKIMWI.

Fedha hizo zimeshindwa kutumika huku takwimu za Kitaifa zikionesha kwamba mkoa wa Iringa ndio unaoongoza kwa kasi kubwa ya maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 15.7 na wakati huo huo, mkoa ukiwa katika utekelezaji wa mkakati wake mpya wa kukabiliana na janga hilo unaolenga kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia hamsini katika kipindi cha miaka minne ijayo.

Aibu ya kutozitumia fedha hizo ilibainika juzi mjini Iringa kwenye kikao cha Ushauri cha Mkoa wa Iringa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo baada ya Meneja Mipango wa Tunajali mkoani Iringa, Dk. John Kahemele kutoa taarifa hiyo ya kusikitisha.

Source: Lukwangule Ent.
 
Back
Top Bottom