The Zanzibar Echo
JF-Expert Member
- Apr 21, 2025
- 490
- 836
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ametetea uamuzi wa nchi yake kusitisha ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Nguvu za Atomiki,IAEA, akimtuhumu mkuu wake kwa mwenendo wa kile alichokiita uharibifu.
SiasaMashariki ya Kati
Iran yatetea uamuzi wake wa kusimamisha ushirikiano na IAEA
Thelma Mwadzaya
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ametetea uamuzi wa nchi yake kusitisha ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Nguvu za Atomiki,IAEA, akimtuhumu mkuu wake kwa mwenendo wa kile alichokiita uharibifu.
Wakati huohuo, Ujerumani na Ufaransa kwa pamoja zimeilaani Iran kwa kumtishia mkuu wa shirika la IAEA baada ya kunyimwa ridhaa ya kuyatembelea maeneo ya shughuli za nyuklia yaliyshambuliwa.Yote hayo yakiendelea Iran inasisitiza kuwa ina haki ya kuwa na nyuklia kwa matumizi ya amani.
Wabunge wa Iran walipitisha muswada wa kusitisha ushirikiano na IAEA muda mfupi baada ya mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na Israel tarehe 13 Juni, na mashambulizi ya baadaye yaliyofanywa na Marekani kwenye vituo vya shughuli za nyuklia vya Iran.
Maafisa wa Iran wanasema IAEA imeshindwa kuwajibika kitaalamu
Ingawa usitishaji wa mapigano kati ya Iran na Israel ulianza tarehe 24 Juni, maafisa wa Iran wameendelea kulalamikia kile wanachokiita kushindwa kwa IAEA kuchukua msimamo wa kitaalamu na usioegemea upande wowote. Pia walikosoa azimio la IAEA la tarehe 12 Juni lililodai kuwa Iran haijazingatia wajibu wake kuhusu mkataba wa nyuklia.
Rais Macron, katika chapisho la hadhara, alitoa wito wa kuheshimu usitishaji wa mapigano na kurejea kwa mazungumzo kuhusu masuala ya nyuklia na makombora ya masafa marefu. Alisisitiza pia umuhimu wa Tehran kuwaruhusu wakaguzi wa IAEA kurejea nchini humo ili kuhakikisha uwazi kamili.
Hata hivyo, Iran imesisitiza kuwa hali ya sasa bado ni tete mno kuhakikisha usalama wa wakaguzi wa kimataifa, hasa ikizingatiwa kuwa maeneo yao ya nyuklia yalishambuliwa moja kwa moja siku chache zilizopita. Ufaransa, Ujerumani na Uingereza zilitoa taarifa ya pamoja kulaani vitisho dhidi ya Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Rafael Grossi, baada ya Iran kukataa ombi lake la kutembelea maeneo ya nyuklia yaliyoshambuliwa.
Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Rafael Grossi ni jasusi wa Israel?
Ingawa vitisho hivyo havikufafanuliwa wazi, gazeti la kihafidhina la Iran Kayhan lilikuwa tayari limechapisha makala inayodai kuwa Grossi ni jasusi wa Israel na kusema anapaswa kuhukumiwa kifo akiingia nchini humo, hali iliyozua hasira katika miji mikuu ya nchi za Magharibi.
SiasaMashariki ya Kati
Iran yatetea uamuzi wake wa kusimamisha ushirikiano na IAEA
Thelma Mwadzaya
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ametetea uamuzi wa nchi yake kusitisha ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Nguvu za Atomiki,IAEA, akimtuhumu mkuu wake kwa mwenendo wa kile alichokiita uharibifu.
Wakati huohuo, Ujerumani na Ufaransa kwa pamoja zimeilaani Iran kwa kumtishia mkuu wa shirika la IAEA baada ya kunyimwa ridhaa ya kuyatembelea maeneo ya shughuli za nyuklia yaliyshambuliwa.Yote hayo yakiendelea Iran inasisitiza kuwa ina haki ya kuwa na nyuklia kwa matumizi ya amani.
Wabunge wa Iran walipitisha muswada wa kusitisha ushirikiano na IAEA muda mfupi baada ya mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na Israel tarehe 13 Juni, na mashambulizi ya baadaye yaliyofanywa na Marekani kwenye vituo vya shughuli za nyuklia vya Iran.
Maafisa wa Iran wanasema IAEA imeshindwa kuwajibika kitaalamu
Ingawa usitishaji wa mapigano kati ya Iran na Israel ulianza tarehe 24 Juni, maafisa wa Iran wameendelea kulalamikia kile wanachokiita kushindwa kwa IAEA kuchukua msimamo wa kitaalamu na usioegemea upande wowote. Pia walikosoa azimio la IAEA la tarehe 12 Juni lililodai kuwa Iran haijazingatia wajibu wake kuhusu mkataba wa nyuklia.
Rais Macron, katika chapisho la hadhara, alitoa wito wa kuheshimu usitishaji wa mapigano na kurejea kwa mazungumzo kuhusu masuala ya nyuklia na makombora ya masafa marefu. Alisisitiza pia umuhimu wa Tehran kuwaruhusu wakaguzi wa IAEA kurejea nchini humo ili kuhakikisha uwazi kamili.
Hata hivyo, Iran imesisitiza kuwa hali ya sasa bado ni tete mno kuhakikisha usalama wa wakaguzi wa kimataifa, hasa ikizingatiwa kuwa maeneo yao ya nyuklia yalishambuliwa moja kwa moja siku chache zilizopita. Ufaransa, Ujerumani na Uingereza zilitoa taarifa ya pamoja kulaani vitisho dhidi ya Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Rafael Grossi, baada ya Iran kukataa ombi lake la kutembelea maeneo ya nyuklia yaliyoshambuliwa.
Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Rafael Grossi ni jasusi wa Israel?
Ingawa vitisho hivyo havikufafanuliwa wazi, gazeti la kihafidhina la Iran Kayhan lilikuwa tayari limechapisha makala inayodai kuwa Grossi ni jasusi wa Israel na kusema anapaswa kuhukumiwa kifo akiingia nchini humo, hali iliyozua hasira katika miji mikuu ya nchi za Magharibi.