Iran yapitisha mswada wa kusimamisha ushirikiano na IAEA

Iran yapitisha mswada wa kusimamisha ushirikiano na IAEA

Ritz

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2011
Posts
54,015
Reaction score
43,157
Wanaukumbi.

Bunge la Iran limepitisha muswada wa kusimamisha ushirikiano na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki, IAEA. hatua iliyochukuliwa kufuatia vita kati ya Israel na Jamhuri hiyo ya kiislamu.
Spika wa Bunge Mohammad Bagher Ghalibaf hapo awali alitangaza kwamba mpango wa nyuklia wa Iran utafuatiliwa "kwa kasi zaidi."

Kura hiyo inaiondoa Iran katika mfumo wa uangalizi wa kimataifa huku ikiacha kujiondoa rasmi kwenye NPT.

Israel ilianza kuishambulia Iran Juni 13 ikisema dhamira yake ni kuizuwia Tehran, kuendelea na mpango wake wa nyuklia. Israel imesema mpango huo ni hatari kwa usalama wake.

Spika wa bunge amenukuliwa akisema kuwa IAEA ilikataa hata kulaani shambulizi lililofanywa kwenye vinu vya Iran vya nyuklia

SOURCE 👇🏽

Iran’s parliament voted on Wednesday to suspend all cooperation with the International Atomic Energy Agency (IAEA), effectively ending i ... https://share.google/xVeENSGyBKMwFgLXU
 
Wanaukumbi.

Bunge la Iran limepitisha muswada wa kusimamisha ushirikiano na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki, IAEA. hatua iliyochukuliwa kufuatia vita kati ya Israel na Jamhuri hiyo ya kiislamu.

Hatua hiyo ambayo bado inahitaji kuidhinishwa na Baraza la Juu la usalama wa Taifa nchini humo, inajiri kufuatia vita vya Jamhuri hiyo ya kiislamu na Israel.

Israel ilianza kuishambulia Iran Juni 13 ikisema dhamira yake ni kuizuwia Tehran, kuendelea na mpango wake wa nyuklia. Israel imesema mpango huo ni hatari kwa usalama wake.

Spika wa bunge amenukuliwa akisema kuwa IAEA ilikataa hata kulaani shambulizi lililofanywa kwenye vinu vya Iran vya nyuklia

Bunge la Iran limepitisha muswada wa kusimamisha ushirikiano na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki, IAEA. hatua iliyochukuliwa kufuatia vita kat… Source: dw.com Iran yapitisha mswada wa kusimamisha ushirikiano na IAEA – DW – 25.06.2025
Je ...Kuhusu USA kushambulia vinu vya nyuklia...hakuna tamko lolote?
 
Je ...Kuhusu USA kushambulia vinu vya nyuklia...hakuna tamko lolote?
Walishasema wazi hamna madhara yeyote mzigo uliamishwa siku nyingi Israel na Marekani ndiyo wanapeana lawama.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
White House press secretary Karoline Leavitt issued a sharp rebuke Tuesday of a leaked Pentagon report that said the United States’ strikes on Iranian nuclear facilities over the weekend only set the country’s program back by a few months.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Ali Khezrian, mwakilishi wa Tehran, aliishutumu IAEA kwa "ujasusi" na kusema shirika hilo lilihamisha habari za Irani kwa Israeli.

Sheria pia inataka kuendelea kurutubishwa uranium bila ufuatiliaji wa kimataifa.
 
Sheria hiyo inakataza uwekaji wa kamera za ufuatiliaji wa IAEA kwenye vituo vya nyuklia na kupiga marufuku kuingia kwa wakaguzi wa kimataifa nchini.

Sheria pia inaharamisha kutoa ripoti zozote kwa IAEA, huku bunge likianzisha adhabu kwa maafisa wanaoshindwa kutekeleza.
 
Wanaukumbi.

Bunge la Iran limepitisha muswada wa kusimamisha ushirikiano na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki, IAEA. hatua iliyochukuliwa kufuatia vita kati ya Israel na Jamhuri hiyo ya kiislamu.
Spika wa Bunge Mohammad Bagher Ghalibaf hapo awali alitangaza kwamba mpango wa nyuklia wa Iran utafuatiliwa "kwa kasi zaidi."

Kura hiyo inaiondoa Iran katika mfumo wa uangalizi wa kimataifa huku ikiacha kujiondoa rasmi kwenye NPT.

Israel ilianza kuishambulia Iran Juni 13 ikisema dhamira yake ni kuizuwia Tehran, kuendelea na mpango wake wa nyuklia. Israel imesema mpango huo ni hatari kwa usalama wake.

Spika wa bunge amenukuliwa akisema kuwa IAEA ilikataa hata kulaani shambulizi lililofanywa kwenye vinu vya Iran vya nyuklia

SOURCE 👇🏽

Iran’s parliament voted on Wednesday to suspend all cooperation with the International Atomic Energy Agency (IAEA), effectively ending i ... https://share.google/xVeENSGyBKMwFgLXU
Screenshot_20250625_160116_Instagram.jpg
 
hapa kuku mweusi kajimwagia rangi nyeupe
 
© Trump: "Israel was hit very hard.


Especially in the last few days, Israel was really hit hard. boy, those ballistic missiles took out a lot of buildings."
=========================
© Trump: "Israel ilipigwa vibaya sana.
Hasa katika siku chache zilizopita, Israeli ilipigwa sana. kijana, makombora hayo ya balestiki yalichukua majengo mengi."
 
Chini ya kifungu kilichoambatanishwa, ukiukaji wowote wa sheria utazingatiwa kuwa uhalifu unaoadhibiwa na adhabu ya hiari ya daraja la sita.
 
Haya majitu hayapaswi kumiliki Nuclear hata kidogo
 
Netanyahu na Trump, walijazana ujinga sana walikuwa na fikra za Libya na Iraq, serikali zao zilivyoangusha.


Malengo yao ya vita yalikuwa ni kwenda kuharibu vinu vya nukilia, kuangusha utawala wa Ayatollah na kuilazimisha Iran kusaini makubaliano ya amani na Israel kama walivyo fanya Misri na Jordan lakini yote yamegonga ukuta wamejikutana wanazoa kifusi Tell Aviv, Haifa na miji migine.

Marekani isingeingilia hii vita. ballistic za Iran zingeendelea kurushwa ndani ya miezi michache tu waisrael wote wangeikimbia nchi yao. Bahati mbaya Israel ina eneo dogo kambi za jeshi na makazi ya watu yapo karibu.

Jana Netanyahu anaaema ameshinda vita😁
 
Kila nchi ina haki ya kumiliki silaha za nyukulia usiwe punguani hao wanaomiliki kazi yao kuuwa watoto na wanawqke wewe unaona ndiyo wana haki.
Wanaua watoto kama collateral damage, target ni wazazi wao wangekuwa Magaidi, Roughly jamii za Kiislamu za Mashariki ya kati ni hatari kwa utulivu na stability ya dunia. Wanapaswa wadhibitiwe.
 
Yanayopaswa kumiliki ni yale mauaji yanawaua watoto na bunduki, pindi wanapojaribu kwenda kuchukua vyakula vya misaada pale Gaza?
Wanaua watoto kama collateral damage, target ni wazazi wao wangekuwa Magaidi, Roughly jamii za Kiislamu za Mashariki ya kati ni hatari kwa utulivu na stability ya dunia. Wanapaswa wadhibitiwe.
 
Back
Top Bottom