Iran yamnyonga mpiga filimbi 'aliyeteswa ili kuungama'

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Sep 11, 2020
69
104
Iran imemnyonga bingwa wa kupiga filimbi ambaye alidai kuwa aliteswa kwa kuchukuliwa video akilazimishwa kufanya maungamo ya uongo kwenye kesi ambayo iliibua kilio cha kimataifa.

Navid Afkari 27, alinyongwa katika gereza la Adelabad lililopo Shiraz nchini humo baada ya kuhukumiwa kwa kosa la kumchoma na kifaa chenye ncha mpaka kufa mlinzi wa kampuni ya maji wakati wa maandamano ya kupinga Serikali mwaka 2018, kilisema chombo cha habari cha serikali siku ya Jumamosi ya tarehe 12 Septemba 2020.

Afkari ambaye ameangukia kwenye hukumu ya kifo, alisema kuwa alishinikizwa kufanya maungamo ya uongo, kwa mujibu wa familia yake, wanaharakati na mwanasheria wake wanasema hakuna ushahidi wa makosa yake. Watu walio upande wake wanamtaja kama ‘ Mfungwa wa kisiasa ‘.

Mwanasheria wake, Hassan Younesi alishutumu mamlaka kwa kumkatalia mteja wake kutembelewa na familia yake kabla ya kunyongwa kama sheria inavyotaka.

Mahakama ya Iran imekanusha madai ya kumtesa, na mahakama kuu nchini humo ilikataa tahakiki ya kesi hiyo mwishoni mwa mwezi wa nane.

Kaka zake Ifkari, Vahid na Habib walihukumiwa kifungo cha miaka 54 na 27 jela kwa kesi hiyo hiyo, hii ni kwa mujibu wa wanaharakati wa haki za binadamu nchini humo.

Mama yao amesema kuwa watoto wake walilazimishwa kutoleana ushuhuda kwa kuteswa.

Shirika la Amnesty International lilisema siku ya Ijumaa ya tarehe 11 Septemba 2020 kuwa Afkari alikua karibu kunyongwa kwa siri , kwenye kuongezea hilo Afkari alipigia simu familia yake tarehe 6 Septemba akisema anapelekwa katika gereza la Adelabab ambalo lina ulinzi wa juu na masharti magumu.

Champion wrestler executed by hanging after being 'tortured into confession'
 
Iran imemnyonga bingwa wa kupiga filimbi ambaye alidai kuwa aliteswa kwa kuchukuliwa video akilazimishwa kufanya maungamo ya uongo kwenye kesi ambayo iliibua kilio cha kimataifa.

Navid Afkari 27, alinyongwa katika gereza la Adelabad lililopo Shiraz nchini humo baada ya kuhukumiwa kwa kosa la kumchoma na kifaa chenye ncha mpaka kufa mlinzi wa kampuni ya maji wakati wa maandamano ya kupinga Serikali mwaka 2018, kilisema chombo cha habari cha serikali siku ya Jumamosi ya tarehe 12 Septemba 2020.

Afkari ambaye ameangukia kwenye hukumu ya kifo, alisema kuwa alishinikizwa kufanya maungamo ya uongo, kwa mujibu wa familia yake, wanaharakati na mwanasheria wake wanasema hakuna ushahidi wa makosa yake. Watu walio upande wake wanamtaja kama ‘ Mfungwa wa kisiasa ‘.

Mwanasheria wake, Hassan Younesi alishutumu mamlaka kwa kumkatalia mteja wake kutembelewa na familia yake kabla ya kunyongwa kama sheria inavyotaka.

Mahakama ya Iran imekanusha madai ya kumtesa, na mahakama kuu nchini humo ilikataa tahakiki ya kesi hiyo mwishoni mwa mwezi wa nane.

Kaka zake Ifkari, Vahid na Habib walihukumiwa kifungo cha miaka 54 na 27 jela kwa kesi hiyo hiyo, hii ni kwa mujibu wa wanaharakati wa haki za binadamu nchini humo.

Mama yao amesema kuwa watoto wake walilazimishwa kutoleana ushuhuda kwa kuteswa.

Shirika la Amnesty International lilisema siku ya Ijumaa ya tarehe 11 Septemba 2020 kuwa Afkari alikua karibu kunyongwa kwa siri , kwenye kuongezea hilo Afkari alipigia simu familia yake tarehe 6 Septemba akisema anapelekwa katika gereza la Adelabab ambalo lina ulinzi wa juu na masharti magumu.

Champion wrestler executed by hanging after being 'tortured into confession'

KUMWAGA DAMU HAWA WATU NI IBADA
 
Kama aliua aachwe tu? Mfanye maandamano ili mtuvunjie maduka yetu then muachwe tu? Mbona wezi wakiwaibia elfu mbili mnawachoma moto.
Na mara hii muandamane hukohuko makwenu mkijichanganya mtajuta.

Sent from my SM-M205F using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ya wezi haifanywi kisheria, wanaofanya hivyo ni wahalifu pia. Kuna haja ya kuangalia upya adhabu ya kifo, kifungo cha maisha ni adhabu tosha
Kama aliua aachwe tu? Mfanye maandamano ili mtuvunjie maduka yetu then muachwe tu? Mbona wezi wakiwaibia elfu mbili mnawachoma moto.
Na mara hii muandamane hukohuko makwenu mkijichanganya mtajuta.

Sent from my SM-M205F using JamiiForums mobile app
 
Hivi hii haki ya binadamu kumtoa mwwnzie uhai tumeitoa wapii?
Hapa mkuu;

Aliyemuumba Simba kula nyama pekee ili aendelee kuishi ndiye huyo huyo aliyemuumba Swala!

Iwapo unamuonea huruma Swala kuliwa na Simba utaona huruma pia kumuona Simba akifa njaa.

Tafakari
 
Ma Ayatollah huwa hayapatagi usingizi bila kumwaga damu.
Acha ushithole ww, ivi umewahi kulalamika yule mweusi kama ww alipopigwa risasi juzi marekani bila ya hatia, na Yule George je, huyo alienyogwa kauwa huko Iran so ni haki yake, ACHENI UPUUZI
fm_facts-20200916-0001.jpg
 
  • Thanks
Reactions: RTI
Wewe ndio unapaswa uulizwe kama ni mzima, unaunga mkono uuwaji kwa sababu vitendo kama hivyo viliwahi kutokea katika nchi nyingine.
Unakua uko kimya wanapouliwa kinyama wamarekani weusi ila jamaa kahukumiwa mahkama hukumu ya kifo kwa kosa la mauwaji unapiga kelele? Ivi ww ni mzima mkuu?
 
Kila nchi na hukumu yake, kama kauwa nchi ya Iran hukumu inasema na yy auliwe, sasa ww kinachokuuma ni nn?? Au ulitaka muuwaji azurure? Hizo nchi mnazoziita za kidemocrasisia mbona wanauliwa black man kweupe mbona huongei humu hulaaani, acheni upimbi
Wewe ndio unapaswa uulizwe kama ni mzima, unaunga mkono uuwaji kwa sababu vitendo kama hivyo viliwahi kutokea katika nchi nyingine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom