Lazima usaili huu ufanyike uwanjani, manake kwa mfumo wa ajira wa taasisi hii pamoja na kuangalia professionalism, ukakamavu ni nyenzo na kigezo muhimu sana kupata ajira kwenye taasisi hii.
Waombaji wote wajiandae vizuri kwa mazoezi ya physique (physical fitness) , kukimbizana lazima hata uwe na masters.
Manake wote watakaofaulu usaili watatakiwa kupelekwa kwenye mafunzo (recruit corse) isiyopungua miezi 8 kabla ya kuajiriwa rasmi as the institution is paramilitary.
Kwenye recruit course kuamka asubuhi ni saa 10 asubuhi na kulala ni saa 4 usiku kila siku, ratiba imekamilika watu wajiandae kwa hectics.
Aidha taasisi imeshafunga kupokea maombi tokea tarehe 22/10 .Usiangaike kutuma kama ulikuwa haujatuma hadi tar 21/10.
Waombaji wote wawe wavumilivu, mchakato ajira hizi unaweza chukua muda mrefu hususani kwenye zoezi la kuscrin vyeti vya wale ambao wataitwa kwenye usaili.
Kama umetumia nakala ya vyeti vya kufoji, jiandae kujitetea mahakamani.
Aidha mnaaswa kuepuka na matapeli wanaowadanganya kwamba wanaweza kukusaidia kupata ajira kwenye taasisi kwa njia ya mkato na hivyo wapewe fedha au bakshishi ya aina yeyote. Yeyeto atakayekutana na mtu wa namna hiyo amripoti kwa Mkurugenzi mkuu TAKUKURU +255 22 2150043-6,+255 22 2150047 au ofisi yeyote ya takukuru iliyo karibu.
Taratibu za ajira kwenye hii Taasisi hazina upendeleo.