Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
India imeripoti kushuka kwa maambukizi ya virusi vya corona katika miji yake mikubwa miwili ya Delhi na Mumbai, inayokaliwa na zaidi ya theluthi mbili ya wakazi bilioni 1.4 wa taifa hilo.
Maambukizi mapya 326,098 yameripotiwa ndani ya saa 24 zilizopita, pamoja na vifo 3,890, ingawa wataalamu wa afya wanasema idadi inayoripotiwa huenda ikawa ndogo kuliko uhalisia.
Kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja uliopita, chini ya visa 10,000 vya maambukizi vimeripotiwa ndani ya siku moja. Mji wa Delhi umeshuhudia visa 8,506 vya maambukizi ndani ya saa 24 zilizopita. Katika mji wa kibiashara wa Mumbai, maambukizi yameshuka kufikia visa pungufu ya 2,000 kutoka 11,000 kwa siku.
Waziri Mkuu, Narendra Modi amewaonya wananchi kuchukua tahadhari zaidi hasa wakati huu ambapo maambukizi ya virusi vya corona yamehamia katika maeneo ya vijijini yenye uhaba mkubwa wa miundombinu ya afya.
Chanzo: ABC News
Maambukizi mapya 326,098 yameripotiwa ndani ya saa 24 zilizopita, pamoja na vifo 3,890, ingawa wataalamu wa afya wanasema idadi inayoripotiwa huenda ikawa ndogo kuliko uhalisia.
Kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja uliopita, chini ya visa 10,000 vya maambukizi vimeripotiwa ndani ya siku moja. Mji wa Delhi umeshuhudia visa 8,506 vya maambukizi ndani ya saa 24 zilizopita. Katika mji wa kibiashara wa Mumbai, maambukizi yameshuka kufikia visa pungufu ya 2,000 kutoka 11,000 kwa siku.
Waziri Mkuu, Narendra Modi amewaonya wananchi kuchukua tahadhari zaidi hasa wakati huu ambapo maambukizi ya virusi vya corona yamehamia katika maeneo ya vijijini yenye uhaba mkubwa wa miundombinu ya afya.
Chanzo: ABC News