Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mwenyekiti wa BAVICHA jimbo la Geita Vijijini, Mbeshi Paulo, ameripotiwa kutoweka katika mazingira ya utata baada ya kuchukuliwa na watu waliodaiwa kujitambulisha kuwa askari wa Polisi.
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) Taifa, Wakili Deogratius Mahinyila, kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa X amedai kuwa tukio hilo lilitokea mnamo 18 Julai 2025 baada ya gari kufika nyumbani kwa Mbeshi na kumchukua kwa maelezo kuwa walikuwa ni askari wa Jeshi la Polisi.
Habari zaidi zinasema familia yake haijui alipo, licha ya kufanya juhudi za kumtafuta katika vituo mbalimbali vya Polisi bila mafanikio.
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) Taifa, Wakili Deogratius Mahinyila, kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa X amedai kuwa tukio hilo lilitokea mnamo 18 Julai 2025 baada ya gari kufika nyumbani kwa Mbeshi na kumchukua kwa maelezo kuwa walikuwa ni askari wa Jeshi la Polisi.
Habari zaidi zinasema familia yake haijui alipo, licha ya kufanya juhudi za kumtafuta katika vituo mbalimbali vya Polisi bila mafanikio.