inabidi nibadilike

Lighton

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2019
Posts
1,904
Reaction score
3,099
Nimewaza sana Jana na Leo, kuhusu mwenendo wa maisha yangu. Jinsi ninavyo lala na wanawake tofauti tofauti.

Mimi Miongoni mwa watu ambao wamepitia changamoto nyingi tokea utotoni. Pamoja na kupitia changamoto zote hizo namshukuru MUNGU Kwa jinsi nilivyo, ameniumba kijana mzuri,mpole,mnyenyekevu,mwenye heshima na adabu kwa wakubwa na wadogo, Nina huruma sana. Anyway nisijipakulie sana minyama.

Kasoro yangu ni moja, tokea nikiwa mdogo, nimejikuta nikiandamwa sana na tamaa za ngono, ukiniona na ukiambiwa stori zangu huwezi kuamini, hata rafiki zangu Kuna muda walistaajabu, walipogundua chaini ya wanawake nilio nao.

Hii imekuwa shida, sijawahi kutosheka ngono, na Wala sijawahi kuikinai. Ila naona wakati umefika wa kusema inatosha. Haijalishi napata matamanio kiasi gani Ila inabibidi nijifunze Kuacha. Nimekuwa nikipinga sana kubebewa ujauzito na kutaa ndoa na mahusiano ya kudumu, niliachana na girlfriend wangu kwasababu ya kuwa na wanawake wengi.

Najitahidi sana niondokane na hili jinamizi na Kwa msaada wa MUNGU naamini nitashinda.

Mods naomba mnipigie wimbo wa Mathias walichupa@nitashinda.
 
Nenda kanisani kwako ufanyiwe maombi inaonekana umevamiwa na Pepo la Ngono.

Anza kwa kuepukana na vitu ambavyo vinakusababishia mawazo ya Ngono kila mara.
Kama unapenda kuangalia video za Ngono Acha kbsa na uzifute kwenye simu.
Block pornographic websites zote.
Epukana na watu ambao wanaenda kuongelea habari za Ngono muda wote.

Afu cha muhimu kbsa tafuta ishu ya kufanya uwe busy uache kuwaza waza Ngono.
Inaonekana hujishughulishi na chochote upo upo Tu na unajua an idol mind is a devil's workshop.

Kila la heri.
 
Kwahiyo sisi tunaobadili mienendo yetu bila kuja kuutangazia umma mnatuonaje?

Swine
 
Hadi hapa umeshindwa kuacha mkuu, maana unataka kujaribu kuacha kwa maandishi kama ulivyoandika hapa.
Ungekuwa unataka kuacha kweli basi ungeacha tu kimya kimya!
Kwa kiasi kikubwa hutaweza kuacha kwa namna hii bali labda utapumzika tu kidogo!

Nilikuwa kama wewe mkuu, na nilijaribu kuacha lakini niliishia tu kupumzika kama miezi kadhaa lakini Moto niliokuja nao awamu ya pili ilikuwa zaidi ya mwanzoni.
Mkuu Fanya usijizuie, ukimpata mwanamke kula, usipopata jichukulie Sheria mkononi.... Yaani pale tu ukijisikia basi usihangaike kutafuta mwanamke kama yupo mbali... Jichukulie Sheria mkononi ili mradi hamu ziishe ulale kwa amani.

Mkuu, haya mambo ni kama tu vile maji yanayopita kwenye mkondo... Unaweza ukayazuia tu kwa muda, yakatulia kidogo huku yakijazana! Lakini punde tu yakipata upenyo au sehemu dhaifu, basi yanavunja kizuizi yanamwagika kwa Fujo na mwishowe kuleta mafuriko!

Acha maji yapite kwenye mkondo wake (mtoni) maana msimu wa mvua ukiisha basi nayo hupungua, kwenda pole pole na hata kuisha kabisa.

Kila la heri mkuu!
 
Mimi mwenyewe nashindwa kuwa na misimamo, niliwahi kukaa miezi mitatu sijachakata mbususu yoyote na nilikuwa fresh tu. Siku nilipokutana na pisi yangu flani hivi, nikavunja nadhiri zangu😭
 
Kazi zangu Mimi kuanzia jumatatu mpaka ijumaa nakuwa busy sana Ila jumamosi na jumapili ni hatari sana.
Siangalii picha za ngono Ila nikikutana na manzi Ina nyaash🙆 ugonjwa wangu Mimi ni nyash.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…