Ili kuwaje mpaka ukajikuta umepata maumivu ya mapenzi?

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Mar 25, 2014
10,399
14,313
MAPENZI NI MATAMU, NAOFIA KUUMIZA MOYO
NASHINDWA KUJARIBU, ROHO INANIUMA SANA...
ROHO INANIUMA ENH, ROHO INANIUMAAAA,
ROHO INANIUMA, ROHO INANIUMA,
ROHO INANIUMA ENH..
NAHOFIA KUUMIZA MOYOOOOO, BILA HATA KUPEWA POLE.
DUDU LIUMALO KWANINI NILIPE KIDOLE, OH MOYO

ROHO INANIUMA MIYE.{ KIITIKIO CHA KWENYE WIMBO WA FID-Q_FOHO}

Nimekaa nyumbani nikawa nawaza mahusiano yangu machungu, ya mapenzi niliyowahi kupitia huko nyuma,
najua hakuna ambaye hajawahi kupita kwenye kipindi kIgumu cha maumivu au kidonda kibaya cha mapenzi. kipindi cha maumivu ya mapenzi hufanya mtu awe kama kichaa na mbaya zaidi kichaa wa mapenzi huwa anajijua kabisa kuwa yupo kwenye uwendaazimu, utashindwa kula, kutwa unalia...ukijaribu kulala usingizi hauji...akili inakuwa kama haifanyi kazi...

wengine maumivu ya mapenzi huwapelekea hadi kugombana na ndugu, kuacha kazi zao za maana kisa tu haya mapenzi.

si dhani kama kwa karne za hivi sasa kuna mtu ambaye hajawahi kuumizwa kwenye mahusiano....
nakumbuka
"kulikuwa na kijana anaitwa STUNTER alikuwa na uwezo wa kifedha kutokana na biashara zake za mbao alizokuwa anazifanya, ikatokea siku moja STUNTER alikutana na miss chagga alikuwa ni mrembo, miss chagga alimvutia sana STUNTER ,tatizo moja tu alilokuwa nalo miss chagga alikuwa teja wa madawa ya kulevya na alishawahi kuwahadithia baadhi ya marafiki zake kuwa chanzo cha yeye kukithiri kutumia madawa ya kulevya ni maumivu ya mapenzi. kwakuwa STUNTER alikuwa na uwezo mkubwa tu ki fedha aliamua kumsaidia miss chagga ili baadaye akipona kutoka kwenye uteja wa madawa waoane. kweli jitihada za STUNTER kwa miss chagga zilizaa matunda. miss chagga alipona kabisa urembo wake wa asili alionao ulijidhihirisha kiukweli alivutia sana. STUNTER aliamua kumsomesha miss chagga kwakuwa miss chagga alikuwa na ufaulu mzuli kidato cha sita hawakupata shida ya kutafuta chuo miss chagga alianza chuo kwa msaada mkubwa sana wa STUNTER ....

miss chagga alifanya vizuri kwenye mtihani wake wa mwisho pale chuoni akapata GPA {alama/marks} za juu sana. kipindi hicho kwa ufaulu mkubwa kama alioupata mashirika yalikuwa yanakutafuta yenyewe hivyo miss chagga alipata kazi yenye mshahara mnono alipewa gari na nyumba. kiukweli upendo kwa STUNTER ulizidi walipendana na walihaidiana kuoana hivyo walikuwa wapo kwenye maandalizi ya kuoana.
bahati ilikuwa upande wa miss chagga kwani alichaguliwa kwenda nje ya nchi kuongeza elimu STUNTER hakuwa na jinsi aliamua kumruhusu mpenzi wake aende, miss chagga alipoenda nje alisahau fadhira zote alizofanyiwa na STUNTER. mawasiriano baina ya STUNTER na miss chagga yalikatika kabisa. STUNTER alichanganyikiwa sana msichana aliyempenda, aliyemthamini, aliyemuonyesha kila aina ya starehe, aliyemsaidia leo ameondoka amemuacha peke yake, tena mbaya zaidi amemuacha jangwani bila kumpa ata maji ya kunywa.


STUNTER alilia akakosa wa kumfuta machozi, hakuona ladha ya chakula kwani alishazoe kula pamoja na kipenzi cha moyo wake miss chagga
siku moja STUNTER alipata taarifa kuwa miss chagga anarejea kutoka ughaibuni na nia ya kurejea kwake ni kuja kuolewa...ni kama hiyo taarifa ilikitibua kidonda cha mapenzi kilichokuwa kimeanza kupona cha STUNTER

zile taarifa zilikuwa za kweli miss chagga alirudi bongo akiwa na mshana jr kama mumewe mtarajiwa, STUNTER alifanya jitihada za kumtafuta miss chagga jitihada zake zilifanikiwa.
kumbe kuna kitu kikubwa STUNTER alikipanga, siku aliyokutana na miss chagga , STUNTER aliMfuata miss chagga akamkumbatia kwa nguvu lakini baada ya STUNTER kumuachia miss chagga alianguka kama gunia.. STUNTER alimuua miss chagga ....kipindi hayo yote yanafanyika mshana jr , LEGE , miku pamoja na little hulk walikuwepo eneo la tukio, walimvaa STUNTER wakampiga sana lakini Nifah , Mondray , The Boss na mitale na midimu ambao walikuwa ni maaskari waliwahi eneo la tukio wakamkamata STUNTER

wivu wa mapenzi ulimfanya STUNTER asote gerezani miaka 7 hakuomba kutoka, hakujutia kufanya hicho alicho kifanya lakini alijutia wema wake aliomfanyia miss chagga.
siku ya hukumu ilipofika mbele ya hakimu Daby , STUNTER alikuwa anashitakiwa na jamhuri kwa kosa la mauaji.. nameless girl na Shunie ambao walikuwa ni mawakili walijitolea kumtetea STUNTER
hakimu Daby alilizishwa na hoja za wakili Shunie kuwa mtuhumiwa kipindi anafanya mauaji hakuwa na akili timamu na kutokana na polisi kutokujua majukumu yao hawakumpeleka STUNTER kupimwa akili....wakili nameless girl nae akaesema kuwa jamhuri itoe visibitisho ambavyo ni kisu na zile nguo zenye damu zitakazoonyesha kuwa ni kweli mtuhumiwa alifanya kosa....hoja hizo zenye msingi zilimfanya STUNTER aachiwe huru...

alikuwa huru lakini hakuwa na kitu, hakuwa na mali wala pesa, ndugu jamaa na marafiki zake wote walimgeuka na kumuona muuaji. STUNTER alichanganyikiwa..... na mbaya zaidi alikuwa CHIZI TENA CHIZI WA MAPENZI"


najua nawewe msomaji uliwahi kuumizwa kwa namna moja ama nyingine....najua unayo mengi ya kutuhadithia...naomba utuambie kuwa ilikuwaje hadi ukajikuta una kidonda kikubwa cha mapenzi, ni kitu gani hutokisahau tokea ulivyoumizwa kwenye mapenzi...je unajutia au umeona ni bora ulivyoumizwa kwani umejifunza kutokana na kuumizwa?
lengo ni kutoa funzo kwa wengine wanaojiingiza kwenye mahusiano

{ N.B STORY HII HAIHUSIANI NA MAISHA HALISI YA MARAFIKI AMBAO MAJINA YAO NIMEYATUMIA KWENYE HADITHI HII }
 
Bado najiuliza uliwaza nini kutumia hao wahusika?

Good idea though..
akili za usiku tu hizo mkubwa...back to the point naomba utuambie kuwa ilikuwaje hadi ukajikuta una kidonda kikubwa cha mapenzi, ni kitu gani hutokisahau tokea ulivyoumizwa kwenye mapenzi...je unajutia au umeona ni bora ulivyoumizwa kwani umejifunza kutokana na kuumizwa?
 
Kwanza hongera kwa Ubunifu brother. Mimi sio mpenzi wa stor ila yako imenigusa sio kwasababu umetumia nomino yangu no! Ninja STUNTER acha kupenda hivyo utakuja kujifia.

Ushuhuda. Kuna jamaa jirani yangu nilipata nafasi ya kumjua tena saana saana. Yeye alinizidi umri kidogo. Huyu jamaa alikuwa mwalimu wa shule fulani sasa katika ile shule alibahatika kupata mrembo wa kidato cha nne.

Walifanya mambo yao kwa siri saana na jamaa alimhudumia kila kitu mwanamke na mwanamke hivyo hivyo. Form four KE alifanikiwa kufaulu akachaguliwa shule ya serikali. Na kwa kuwa KE kwao mambo yalikuwa mabaya ikabidi ticha ambaye ni jirani yangu akajitambulishe kwa wazazi wake KE ili awe mchumba wake na amsomeshe. Jamaa alifanya hivyo wazazi wakaridhia na jamaa akawa anahudumia karo na kila kitu pamoja na kwa wazazi alikuwa akivuna shamba lake gunia kadhaa alikuwa anapeleka kwa Wakwe watarajiwa.

Walipendana saana kwa kipindi chote baadae KE akafanikiwa kujiunga chuo SUA. Ticha akamwambia kwasababu umeshafika chuo ni bora tukafunga ndoa. KE alikataa akamwambia subiri nimalize. Ticha akaona isiwe kesi asubiri ila siku baada ya siku binti akaanza kubadilika. Siku moja akamwambia ticha afanye mpango wa kubadilisha fani ya ualimu asomee kitu kingine. Ticha hakukubaliana na huo ushauri akamwambia kama mimi nimeweza kukusomesha na kukufanyia kila kitu kwa carrier hii kwanin leo nije niibadilishe? Jamaa hakumwelewa binti ila akasoma hapa mambo yameshachafuka.

Binti alifanikiwa kumaliza chuo na alianza kujirudi kwa jamaa na taratibu zikafanyika ndoa ikafungwa. Jamaa alipigana kila kona binti/mkewe akapata kazi.

Stor ni ndefu saana . Kukatisha binti alifanikiwa kupata kazi kwa mgongo wa jamaa ila alikuja kukataa kuishi naye kwa kigezo hawezi kukubali kuolewa na mwalimu. Hii ni stori ya kweli sijatunga.
Kuumizwa katika mapenzi kupo na tumeshaumizwa kama sio Kuumizwa. Umenikumbusha mbali saana eddy love.
 
Nimechukua siti apa mbele ntarudi nisikute mtu kakaa
back to the point naomba utuambie kuwa ilikuwaje hadi ukajikuta una kidonda kikubwa cha mapenzi, ni kitu gani hutokisahau tokea ulivyoumizwa kwenye mapenzi...je unajutia au umeona ni bora ulivyoumizwa kwani umejifunza kutokana na kuumizwa?
 
Haya wahusika kujeni huku mtoe maelezo.. Inaonesha mshana jr ana hela kumzidi STUNTER maana miss chagga bila hela ndefu huambulii hata busu.
back to the point naomba utuambie kuwa ilikuwaje hadi ukajikuta una kidonda kikubwa cha mapenzi, ni kitu gani hutokisahau tokea ulivyoumizwa kwenye mapenzi...je unajutia au umeona ni bora ulivyoumizwa kwani umejifunza kutokana na kuumizwa?
 
Kwanza hongera kwa Ubunifu brother. Mimi sio mpenzi wa stor ila yako imenigusa sio kwasababu umetumia nomino yangu no! Ninja STUNTER acha kupenda hivyo utakuja kujifia.

Ushuhuda. Kuna jamaa jirani yangu nilipata nafasi ya kumjua tena saana saana. Yeye alinizidi umri kidogo. Huyu jamaa alikuwa mwalimu wa shule fulani sasa katika ile shule alibahatika kupata mrembo wa kidato cha nne.

Walifanya mambo yao kwa siri saana na jamaa alimhudumia kila kitu mwanamke na mwanamke hivyo hivyo. Form four KE alifanikiwa kufaulu akachaguliwa shule ya serikali. Na kwa kuwa KE kwao mambo yalikuwa mabaya ikabidi ticha ambaye ni jirani yangu akajitambulishe kwa wazazi wake KE ili awe mchumba wake na amsomeshe. Jamaa alifanya hivyo wazazi wakaridhia na jamaa akawa anahudumia karo na kila kitu pamoja na kwa wazazi alikuwa akivuna shamba lake gunia kadhaa alikuwa anapeleka kwa Wakwe watarajiwa.

Walipendana saana kwa kipindi chote baadae KE akafanikiwa kujiunga chuo SUA. Ticha akamwambia kwasababu umeshafika chuo ni bora tukafunga ndoa. KE alikataa akamwambia subiri nimalize. Ticha akaona isiwe kesi asubiri ila siku baada ya siku binti akaanza kubadilika. Siku moja akamwambia ticha afanye mpango wa kubadilisha fani ya ualimu asomee kitu kingine. Ticha hakukubaliana na huo ushauri akamwambia kama mimi nimeweza kukusomesha na kukufanyia kila kitu kwa carrier hii kwanin leo nije niibadilishe? Jamaa hakumwelewa binti ila akasoma hapa mambo yameshachafuka.

Binti alifanikiwa kumaliza chuo na alianza kujirudi kwa jamaa na taratibu zikafanyika ndoa ikafungwa. Jamaa alipigana kila kona binti/mkewe akapata kazi.

Stor ni ndefu saana . Kukatisha binti alifanikiwa kupata kazi kwa mgongo wa jamaa ila alikuja kukataa kuishi naye kwa kigezo hawezi kukubali kuolewa na mwalimu. Hii ni stori ya kweli sijatunga.
Kuumizwa katika mapenzi kupo na tumeshaumizwa kama sio Kuumizwa. Umenikumbusha mbali saana eddy love.
pole sana...asante...si unajua akili za usiku...
 
Kweli mkuu...
Kumbuka
Outrages, sabotages, disappointments and betrayals can not be covered by tears. Dawa ni kujenga moyo wa chuma tu na kuwa mbinafsi.
ila kwa wengine huwa ngumu sana kujenga mioyo ya chuma sijui kwanini hadi wanajikuta wanapoteza uelekeo wa maisha.
 
back to the point naomba utuambie kuwa ilikuwaje hadi ukajikuta una kidonda kikubwa cha mapenzi, ni kitu gani hutokisahau tokea ulivyoumizwa kwenye mapenzi...je unajutia au umeona ni bora ulivyoumizwa kwani umejifunza kutokana na kuumizwa?

Kwa kweli sijawahi kuumizwa kwenye ishu ya mapenzi maana sijayapa uzito.
 
Kwanza hongera kwa Ubunifu brother. Mimi sio mpenzi wa stor ila yako imenigusa sio kwasababu umetumia nomino yangu no! Ninja STUNTER acha kupenda hivyo utakuja kujifia.

Ushuhuda. Kuna jamaa jirani yangu nilipata nafasi ya kumjua tena saana saana. Yeye alinizidi umri kidogo. Huyu jamaa alikuwa mwalimu wa shule fulani sasa katika ile shule alibahatika kupata mrembo wa kidato cha nne.

Walifanya mambo yao kwa siri saana na jamaa alimhudumia kila kitu mwanamke na mwanamke hivyo hivyo. Form four KE alifanikiwa kufaulu akachaguliwa shule ya serikali. Na kwa kuwa KE kwao mambo yalikuwa mabaya ikabidi ticha ambaye ni jirani yangu akajitambulishe kwa wazazi wake KE ili awe mchumba wake na amsomeshe. Jamaa alifanya hivyo wazazi wakaridhia na jamaa akawa anahudumia karo na kila kitu pamoja na kwa wazazi alikuwa akivuna shamba lake gunia kadhaa alikuwa anapeleka kwa Wakwe watarajiwa.

Walipendana saana kwa kipindi chote baadae KE akafanikiwa kujiunga chuo SUA. Ticha akamwambia kwasababu umeshafika chuo ni bora tukafunga ndoa. KE alikataa akamwambia subiri nimalize. Ticha akaona isiwe kesi asubiri ila siku baada ya siku binti akaanza kubadilika. Siku moja akamwambia ticha afanye mpango wa kubadilisha fani ya ualimu asomee kitu kingine. Ticha hakukubaliana na huo ushauri akamwambia kama mimi nimeweza kukusomesha na kukufanyia kila kitu kwa carrier hii kwanin leo nije niibadilishe? Jamaa hakumwelewa binti ila akasoma hapa mambo yameshachafuka.

Binti alifanikiwa kumaliza chuo na alianza kujirudi kwa jamaa na taratibu zikafanyika ndoa ikafungwa. Jamaa alipigana kila kona binti/mkewe akapata kazi.

Stor ni ndefu saana . Kukatisha binti alifanikiwa kupata kazi kwa mgongo wa jamaa ila alikuja kukataa kuishi naye kwa kigezo hawezi kukubali kuolewa na mwalimu. Hii ni stori ya kweli sijatunga.
Kuumizwa katika mapenzi kupo na tumeshaumizwa kama sio Kuumizwa. Umenikumbusha mbali saana eddy love.
huruma sana kwa mwalimu
 
Kidonda nilicho nacho mpaka leo ni mpenzi wangu wa kidato cha tatu (yeye alikua cha kwanza) kuninyima gemu akidai anataka kutunza bikra mpaka ndoa, kisha miaka 2 mbele nikasikia anagawa kama pipi kwa wanafunzi wa chuo.

Hadi leo namtafuta.
 
Eddy we ni bonge la mtunzi hongera sana acha kukalia hiko kipaji nimetulia hapa najua namsoma Lege au The Bold kitu kimeishia kati ila stunter asingemuua miss chagga Mungu analipa hapa hapa ata kama anachelewa
 
Kidonda nilicho nacho mpaka leo ni mpenzi wangu wa kidato cha tatu (yeye alikua cha kwanza) kuninyima gemu akidai anataka kutunza bikra mpaka ndoa, kisha miaka 2 mbele nikasikia anagawa kama pipi kwa wanafunzi wa chuo.

Hadi leo namtafuta.
pole sana mkuu inamaana bado hujampata mwingine...tuu
 
ila kwa wengine huwa ngumu sana kujenga mioyo ya chuma sijui kwanini hadi wanajikuta wanapoteza uelekeo wa maisha.
(Nadhani Niutofauti wa mioyo baina ya watu, eksipiriensi na maamuzi ya akili ya mtu.) Penzi linawakoleza
 
Eddy we ni bonge la mtunzi hongera sana acha kukalia hiko kipaji nimetulia hapa najua namsoma Lege au The Bold kitu kimeishia kati ila stunter asingemuua miss chagga Mungu analipa hapa hapa ata kama anachelewa
asante...bado najifunza...ila muda ukifika...mtanisoma...ila usisahau kushare nasi story yako..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom