Ili kuepusha majanga kwenye ndoa turudi kwenye mila zetu

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,221
22,292
ILI KUEPUSHA MAJANGA KWENYE NDOA TURUDI KWENYE MILA ZETU

Siku hizi watu hawazingatii kabisa mambo ya kimila. Tumewadharau sana wazee wetu ndo maana majanga kila siku kwenye ndoa.

Enzi zetu ukitaka kuoa kuna njia mbili; aidha uchague mchumba wewe mwenyewe au wazee wakuchagulie.

Na kabla ya ndoa lazima tambiko lifanyike ili mizimu itoe kibali. Tambiko huwa ni la siku tatu ambapo wakati wote wa tambiko chakula kikuu ni supu ya mkia wa kondoo ambayo haijawekwa chumvi.

Pia kwa siku hizo tatu hakuna kuoga wala kuvaa viatu. Na ikitokea wazee wamekuchagulia mchumba basi hutamwona huyo binti hadi siku ya ndoa tena jioni maana muda wote kafunikwa usoni.

Na kama una bahati unaweza kukuta tayari ana mimba kwahiyo mtoto anahesabiwa ni wa kwako.

Nadhani ili kuepusha majanga turudi kwenye mila zetu.
 
Ili turudi kwenye mila zetu inabidi turudishe dunia nyuma.

Wadau kwa sasa hicho kitu hakiwezekani kabisa. Hii ni kwa sababu dunia imekuwa na harakati nyingi sana za kimaisha kiasi kwamba hata wazee wanakosa nafasi ya kukaa na watoto ili wawafunze maadili.

Ukichunguza hata mtaani kwako utakuta mtoto ana mtoto yaani yeye mwenyewe bado anahitaji malezi ya wazazi lakini tayari vijana walishamtundika mimba au kishazalishwa.

Pia asilimia kubwa ya watoto wa sasa hivi anqlelewa na mzazi mmoja ndio hizo mimba zisizo na mpangilio so unategemea kutakuwa na maadili.

Shughuli zetu za kujipatia kipato lazima uwahi usafiri asubuhi unakutana na mwanafunzi naye anawahi shule unarudi labdq saa moja jioni mwanafunzi nae anahangaika kupata usafiri wa kurudi, je anakaa saa ngapi na wazazi wake ili kujifunza chochote.

Sasa hivi kwa kweli ni kumuomba tu Mungu atupe.maarifa tuepukane na majanga.
 
Mambo yaliyofanya ndoa za zamani zidumu.

1.Ubabe. Hii ndilo la kwanza. Mwanamke alikuwa kama mtoto ndani ya nyumba. Akiadhibiwa hana pa kusema. Muda wote amekaa kwa nidhamu.

2. Jamii haikusupport habari ya kuachana. Ukishalipiwa mali ni kama umenunuliwa. Hata upigwe ung'olewe meno huna pa kusema. Unavumilia na kutulia.

3. Mali yote ilikuwa mali ya mwanaume. Mwanamke alikuwa hana kitu chochote. Japo ndiye analima na kuzalisha chakula sana, lakini si mali yake.

Mkitaka ndoa zidumu na zisiwe na majanga kama zamani basi turudie hizo mila.
 
Tulipo acha mila zetu wazee walikuja yatakuja tokes tu ila tukajikuta wajanja kumbe wajinga na uzao wa majanga

Leo kamke kanavaa visuruali kujipost Kama kimepotea kweny mitandao kila siku kuvutia wanaume za watu tunaona kawaida na bado mpaka mje sikia mtu kakatwa kichwa maana sikio tayar
 
Back
Top Bottom