Hellow!
Utapingana na Mimi kama hujawahi simama Katika umma wa wananchi kama kiongozi, ila utakubaliana nami kuwa Katika halaiki yoyote, kelele za umati wa watu kushangilia au kuzomea zina nguvu kubwa sana Katika kuongeza ujasiri au kuingiza hofu kwa kiongozi asimamaye jukwaani.
Niliwahi kushuhudia umma wa wananchi ukimpigia kelele hayati Nyerere alipokuwa jukwaani akimnadi Hayati Mkapa jukwaani, Kila alipojaribu kuongea kelele ziliongezeka, Kila alipoinua kifimbo chake kutuliza sauti zile ,sauti hazikukoma, ilifika time wapiga kelele wale walienda kumchukua mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Kiboko Nyerere Ili aje kuongeza kelele Katika mkutano ule, baada ya kelele kuzidi alipofika ndugu yule, Mwalimu alisikika akisema nilidhani Niko Kenya, na baada ya kusema hayo, aliteremka jukwaani na mkutano uliishia pale. HAYO yalitokea mwaka 1995 kwenye kuanza mfumo mpya wa vyama vingi, Mrema akiwa mgombea wa upinzani uwanja wa Mukendo Primary School.
Mji wa Yeriko uliangushwa kwa kelele za sifa kwa Mungu mkuu, kelele ziliingiza hofu kwa maadui wakakosa Cha kufanya. Hilo linarufunza nguvu ya kupaza sauti kuzomea au kushangilia.
(Zaburi 137:4)
Tutaimbaje wimbo wa BWANA Katika nchi ya ugeni( utumwani),
Nchi inahujumiwa na kufilisiwa, tutaimbaje wimbo wa furaha Katika nchi yetu?
Kuelekea Katika majukwaa mbalimbali ya kisiasa 2025, wananchi wanatakiwa kupiga tu kelele, kelele ni kelele,
Kuimba ni kelele,
Kulia ni kelele pia,
Kuzomea ni kelele pia,
Kushangilia ni kelele pia.
-Martin Luther alipiga kelele Amerika ikasikia,
-Desmond Tutu alipiga kelele, ubaguzi wa rangi ukayeyuka,
-Mwl Nyerere alipiga kelele ya haki, nchi ikazukiwa na Nuru, tukapata uhuru.
-Tundu Antipas Lissu anapiga kelele kutafuta kuondoa haramu ndani ya sanduku la kura. "NO REFORMS, NO ELECTION". Amesikika🔥💪
- Joseph at Gwajima anapiga kelele kudai maono ya nchi yaandikwe ubaoni Ili Kila Rais ajaye asome na kutekeleza maono hayo, SI kila mmoja kuja na lake.
-Rabbon anapambana kuuleta ufalme wa Mungu Katika siasa za nchi yetu, viongozi walevi wa namna mbalimbali wasipate fursa kuongoza watu, haki itawale ,hofu ya Mungu itawale, UOVU utokomee, elimu ishamiri nchi istawi.
Kila asimamaye jukwaani apate kelele anayostahili kulingana na matendo yake.
1. Anayestahili kelele za shangwe, apewe shangwe,
2. Anayestahili kelele za kuzomewa, apewe haki yake.
Karibuni tupige kelele 🙏,
Na hakika adui atakuwa mdogo sana, nguvu zitamwisha, vifundo vya miguu vitakosa nguvu, hatoendelea kutoa hadaa na uongo kwa wananchi Tena.
NOTE: Mtu yeyote asikudangaanye kuwa kelele KUPITIA keyboard JF na majukwaa mengine hazisikiki, kelele ni kelele. Piga kelele.
NRNE 💪 🔥
Nawasiiisha 🙏
Utapingana na Mimi kama hujawahi simama Katika umma wa wananchi kama kiongozi, ila utakubaliana nami kuwa Katika halaiki yoyote, kelele za umati wa watu kushangilia au kuzomea zina nguvu kubwa sana Katika kuongeza ujasiri au kuingiza hofu kwa kiongozi asimamaye jukwaani.
Niliwahi kushuhudia umma wa wananchi ukimpigia kelele hayati Nyerere alipokuwa jukwaani akimnadi Hayati Mkapa jukwaani, Kila alipojaribu kuongea kelele ziliongezeka, Kila alipoinua kifimbo chake kutuliza sauti zile ,sauti hazikukoma, ilifika time wapiga kelele wale walienda kumchukua mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Kiboko Nyerere Ili aje kuongeza kelele Katika mkutano ule, baada ya kelele kuzidi alipofika ndugu yule, Mwalimu alisikika akisema nilidhani Niko Kenya, na baada ya kusema hayo, aliteremka jukwaani na mkutano uliishia pale. HAYO yalitokea mwaka 1995 kwenye kuanza mfumo mpya wa vyama vingi, Mrema akiwa mgombea wa upinzani uwanja wa Mukendo Primary School.
Mji wa Yeriko uliangushwa kwa kelele za sifa kwa Mungu mkuu, kelele ziliingiza hofu kwa maadui wakakosa Cha kufanya. Hilo linarufunza nguvu ya kupaza sauti kuzomea au kushangilia.
(Zaburi 137:4)
Tutaimbaje wimbo wa BWANA Katika nchi ya ugeni( utumwani),
Nchi inahujumiwa na kufilisiwa, tutaimbaje wimbo wa furaha Katika nchi yetu?
Kuelekea Katika majukwaa mbalimbali ya kisiasa 2025, wananchi wanatakiwa kupiga tu kelele, kelele ni kelele,
Kuimba ni kelele,
Kulia ni kelele pia,
Kuzomea ni kelele pia,
Kushangilia ni kelele pia.
-Martin Luther alipiga kelele Amerika ikasikia,
-Desmond Tutu alipiga kelele, ubaguzi wa rangi ukayeyuka,
-Mwl Nyerere alipiga kelele ya haki, nchi ikazukiwa na Nuru, tukapata uhuru.
-Tundu Antipas Lissu anapiga kelele kutafuta kuondoa haramu ndani ya sanduku la kura. "NO REFORMS, NO ELECTION". Amesikika🔥💪
- Joseph at Gwajima anapiga kelele kudai maono ya nchi yaandikwe ubaoni Ili Kila Rais ajaye asome na kutekeleza maono hayo, SI kila mmoja kuja na lake.
-Rabbon anapambana kuuleta ufalme wa Mungu Katika siasa za nchi yetu, viongozi walevi wa namna mbalimbali wasipate fursa kuongoza watu, haki itawale ,hofu ya Mungu itawale, UOVU utokomee, elimu ishamiri nchi istawi.
Kila asimamaye jukwaani apate kelele anayostahili kulingana na matendo yake.
1. Anayestahili kelele za shangwe, apewe shangwe,
2. Anayestahili kelele za kuzomewa, apewe haki yake.
Karibuni tupige kelele 🙏,
Na hakika adui atakuwa mdogo sana, nguvu zitamwisha, vifundo vya miguu vitakosa nguvu, hatoendelea kutoa hadaa na uongo kwa wananchi Tena.
NOTE: Mtu yeyote asikudangaanye kuwa kelele KUPITIA keyboard JF na majukwaa mengine hazisikiki, kelele ni kelele. Piga kelele.
NRNE 💪 🔥
Nawasiiisha 🙏