Igunga: Mahakama imemhukumu Elius Mgashi kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kubaka mtoto

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Jan 27, 2018
754
3,097
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Igunga mkoani Tabora, imemuhukumu adhabu ya kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kijana wa miaka 20, kwa kosa la kubaka mtoto wa kaka yake wa miaka 14.

Elius Mgashi mkaazi wa Mtaa wa Stoo mjini Igunga, amepewa adhabu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji.

Mwendesha Mashitaka kutoka Jeshi la Polisi wilaya ya Igunga Elimajid Kweyamba, alidai kwamba katika tarehe tafauti kati ya Septemba 14 na 19 mwaka 2018 katika mtaa wa Stoo mjini Igunga, mshitakiwa huyo alifanya mapenzi na mtoto wa kaka yake ambaye ana umri wa miaka 14.

Mbele ya Hakimu wa wilaya ya Igunga Lydia Ilunda, Kweyamba aliifahamisha mahakama kwamba, kutenda hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 130 (1) (2) (e) na 131 (1) vya kanuni ya adhabu sura ya 16, mapitio ya mwaka 2002 inayozuia kutenda makosa kama hayo.

Hata hivyo, baada ya mshitakiwa kusomewa shitaka hilo alikana, ndipo upande wa Jamhuri ulipeleka mahakamani mashahidi watano akiwemo mhanga wa tukio hilo, ambao wote walimtambua mshitakiwa.

Mahakama hiyo baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, Hakimu Lydia Ilunda alisema, pasi na shaka ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa Jamhuri imemuona mshitakiwa Elius Mgashi ana hatia.

Akitoa hukumu ya shauri hilo, Hakimu Lyidia Ilunda alisema kuwa, mahakama inamuhukumu Elius Mgashi kutumikia adhabu ya kifungo cha jumla ya miaka 30 jela, ili iwe fundisho kwa vijana wengine wanaobaka wasichana wadogo na kuwaharibia maisha yao
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora imemuhukumu Elius Mgashi mwenye umri wa miaka 20 mkazi wa Mtaa wa Stoo, kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kumkuta na hatia ya kumbaka Binti mdogo mwenye umri wa miaka 14 ambaye ni Mtoto wa Kaka yake.
Wabakaji si watu wazuri kabisa. Kama mahakama imeridhika pasina shaka na ushahidi uliotolewa basi ni haki yake.
Acha na yeye akabakwe mbele ya safari.
 
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Igunga mkoani Tabora, imemuhukumu adhabu ya kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kijana wa miaka 20, kwa kosa la kubaka mtoto wa kaka yake wa miaka 14.

Elius Mgashi mkaazi wa Mtaa wa Stoo mjini Igunga, amepewa adhabu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji.

Mwendesha Mashitaka kutoka Jeshi la Polisi wilaya ya Igunga Elimajid Kweyamba, alidai kwamba katika tarehe tafauti kati ya Septemba 14 na 19 mwaka 2018 katika mtaa wa Stoo mjini Igunga, mshitakiwa huyo alifanya mapenzi na mtoto wa kaka yake ambaye ana umri wa miaka 14.

Mbele ya Hakimu wa wilaya ya Igunga Lydia Ilunda, Kweyamba aliifahamisha mahakama kwamba, kutenda hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 130 (1) (2) (e) na 131 (1) vya kanuni ya adhabu sura ya 16, mapitio ya mwaka 2002 inayozuia kutenda makosa kama hayo.

Hata hivyo, baada ya mshitakiwa kusomewa shitaka hilo alikana, ndipo upande wa Jamhuri ulipeleka mahakamani mashahidi watano akiwemo mhanga wa tukio hilo, ambao wote walimtambua mshitakiwa.

Mahakama hiyo baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, Hakimu Lydia Ilunda alisema, pasi na shaka ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa Jamhuri imemuona mshitakiwa Elius Mgashi ana hatia.

Akitoa hukumu ya shauri hilo, Hakimu Lyidia Ilunda alisema kuwa, mahakama inamuhukumu Elius Mgashi kutumikia adhabu ya kifungo cha jumla ya miaka 30 jela, ili iwe fundisho kwa vijana wengine wanaobaka wasichana wadogo na kuwaharibia maisha yao
Mungu amsamehe
 
Duuuh! wanaume wenzangu inaonekana hawaogopi miaka 30?
Hii hatari sana.
 
Sheria ibadilishwe
Ukithibitika au Ukikiri umebaka uhasiwe maisha yaendelee
Hiyo iliwahi kuongelewa sana bungeni sijui iliishia wapi tu!

Lakini adhabu hiyo kwa kuwa ilikuwa inamuondelea mkosaji mambo mengi kwa mkupuo: kumuondolea furaha maishani, kuvuruga mfumo wa homoni zake za kiume, kumfanya awe boya nk nk. Je watu wasingeweza kubambikiziana kwa husda ili kuwakata ngebe na viherehere wenzao?

Kuna m1 nchini Drc alibainika kutembea na mchepuko wa Mobutu, halafu akahasiwa, sijui sasa hivi anaishije!
 
Hiyo iliwahi kuongelewa sana bungeni sijui iliishia wapi tu!

Lakini adhabu hiyo kwa kuwa ilikuwa inamuondelea mkosaji mambo mengi kwa mkupuo: kumuondolea furaha maishani, kuvuruga mfumo wa homoni zake za kiume, kumfanya awe boya nk nk. Je watu wasingeweza kubambikiziana kwa husda ili kuwakata ngebe na viherehere wenzao?

Kuna m1 nchini Drc alibainika kutembea na mchepuko wa Mobutu, halafu akahasiwa, sijui sasa hivi anaishije!

Endapo Kama kweli kabisa ametenda kosa hilo kiuhalisia, adhabu aliyopewa ni sahihi NA inatosha.Siungi mkono kabisa kuwa watuhumiwa WA Kesi hizo wahasiwe, ni ukatili mkubwa sana, bora tu umuue kuliko kumuhasi.
 
Endapo Kama kweli kabisa ametenda kosa hilo kiuhalisia, adhabu aliyopewa ni sahihi NA inatosha.Siungi mkono kabisa kuwa watuhumiwa WA Kesi hizo wahasiwe, ni ukatili mkubwa sana, bora tu umuue kuliko kumuhasi.
Mkuu kwa nini unaona bora kifo kuliko maisha bila P?
Mbona kuna watu matowashi wapo wanadunda tu mitaani na tunawafahamu kwa majina?
 
Shida
Hiyo iliwahi kuongelewa sana bungeni sijui iliishia wapi tu!

Lakini adhabu hiyo kwa kuwa ilikuwa inamuondelea mkosaji mambo mengi kwa mkupuo: kumuondolea furaha maishani, kuvuruga mfumo wa homoni zake za kiume, kumfanya awe boya nk nk. Je watu wasingeweza kubambikiziana kwa husda ili kuwakata ngebe na viherehere wenzao?

Kuna m1 nchini Drc alibainika kutembea na mchepuko wa Mobutu, halafu akahasiwa, sijui sasa hivi anaishije!
Ni pale mtuhumiwa ikatokea hakuwa na hatia yaani hukumu ilikosewa na wewe umeshamhasi mtu, je utamrudidhia nyeti zake?
 
Shida

Ni pale mtuhumiwa ikatokea hakuwa na hatia yaani hukumu ilikosewa na wewe umeshamhasi mtu, je utamrudidhia nyeti zake?
Na kwa kesi za mauaji wanaohukumiwa kunyongwa na kisha adhabu kutekelezwa, ikibainika baadaye kuwa alibambikwa, hurejeshewa uhai wao?

Mantiki ni mtu anayebainika kutenda pasina shaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom