If Nyerere was alive...

Rev.Kishoka,

..mbona Kawawa aliendelea kupeta hata baada ya kuboronga ktk operesheni vijiji?

..mbona Sokoine aliendelea kupeta hata baada ya kumpa Mwalimu ushauri mbaya kuhusu matatizo ya uchumi/wahujumu uchumi? Waliompa ushauri mzuri wakina Mtei wakafukuzwa kazi?

..mbona yule Mkuu wa Mkoa aliyeshtakiwa na wananchi kwa kuzini na watoto wa shule hakufukuzwa kazi na Baba wa Taifa? halafu mnashangaa ya babu seya.

..mbona yule Afisa wa Polisi alipelekwa Ubalozini baada ya kubainika kwamba alikanyaga na kuua mtu kwa gari? leo mnashangaa ya Ditopile.

..Kassim Hanga alionekana kwa mara ya mwisho akiwa hai ktk mkutano wa hadhara ambapo Mwalimu alimtukana kama mtoto mdogo. Hanga ametoweka, inasemekana aliuawa. Kaburi lake liko wapi? Katika watu wote "waliopotelea" Zenj nadhani Mwalimu had to account for Kassim Hanga.

..Labda Kanisa Katoliki watueleze alipozikwa Kassim Hanga kabla ya kumsimika Utakatifu Mwalimu Nyerere.

Ukishapata majibu, utabadilisha msimamo?
 
1. Mkapa would not have had a second term in 2000!
2. A Zanzibari would have succeded Mkapa (Salim or Sheni)
3. Lowassa would have been gone out of picture compoletely and his attmpts to Join Upinzani in 1998-99 that led to Mkapa handing him Uwaziri would not have worked machoni na puani mwa Mwalimu
4. RA, JK would have had to wait until 2010 to make their move and by that time, none of them would have had any political capital.
5. Funny names like Karamagi or Msabaha would have been Majina ya Vijiweni and so is Chenge!
6. Malecela would have retired ealier from CCM
7. Upinzani would have had at least 30% seats in the parliament, due to msukumo wa kuboresha upinzai na si kukandamiza
8. Sitta would never had been a speaker
9. Sinclair, Andrew Young, Barrick, ABSA, SAA, and all wawekezaji haramu would not have been holding 99% control of their investments!
10. Takrima would have been banned
11. Emmanuel Nchimbi would have been a nobody!
12. No talk of Muafaka would have been in place, Serikali of Mseto would have been in existance in Zanzibar!
13. We would not have seen continuation or Radar, Ndege or IPTL saga. RDC, Kiwira would have been ndoto mbovu. Mikopo for Meremeta, Mwananchi Green and Tangold would not have been sign. Balali would have been in Dar working dilligently and not laying on death bed!
14. Simba would have lost every game to Yanga :)

Jamani kwa mwenye taarifa za mtu huyu,kaadimika sana!
 
Rev.Kishoka,

..mbona Kawawa aliendelea kupeta hata baada ya kuboronga ktk operesheni vijiji?

..mbona Sokoine aliendelea kupeta hata baada ya kumpa Mwalimu ushauri mbaya kuhusu matatizo ya uchumi/wahujumu uchumi? Waliompa ushauri mzuri wakina Mtei wakafukuzwa kazi?

..mbona yule Mkuu wa Mkoa aliyeshtakiwa na wananchi kwa kuzini na watoto wa shule hakufukuzwa kazi na Baba wa Taifa? halafu mnashangaa ya babu seya.

..mbona yule Afisa wa Polisi alipelekwa Ubalozini baada ya kubainika kwamba alikanyaga na kuua mtu kwa gari? leo mnashangaa ya Ditopile.

..Kassim Hanga alionekana kwa mara ya mwisho akiwa hai ktk mkutano wa hadhara ambapo Mwalimu alimtukana kama mtoto mdogo. Hanga ametoweka, inasemekana aliuawa. Kaburi lake liko wapi? Katika watu wote "waliopotelea" Zenj nadhani Mwalimu had to account for Kassim Hanga.

..Labda Kanisa Katoliki watueleze alipozikwa Kassim Hanga kabla ya kumsimika Utakatifu Mwalimu Nyerere.


JokaKuu,

Lazim nikubali yakua kumbe kitambo kingi hata nawe pia ulikua ukitoa misimamo objective and/or constructive criticism kiasi hiki!?

Sasa haya yoote yamepotolea wapi Mkuu!?

Mbona hivi sasa sisi wangine tukigusia tu jina la "Mwalim",inakua tunapewa shutuma na kashfa nyingi mno!? Daah!


Nisingalipenda kulinganisha baya kwa baya...lakini linalontatiza mie binafsi linakuja pale wengi ya Wanajamvi wanapomzungumzia Nyerere aka "Baba wa Taifa" au ku-criticise awamu nyangine zilofuata badala yake...yaani wanaweka mbele mno emotions zao na kutoangalia reality au ukweli wa kihistoria ya siasa za nchi yetu!!

Kwa mfano jina la Nyerere pale linapotumika kama myth,mystical figure and/or Saint ambae labda hakuwahi kufanza makosa ya aina yoyote kwenye utawala wake...wakti kiuhakika ni kuwa makosa yake mangi mno yamekua kama mzimu mpaka kesho bado yanalitafuna Taifa letu changa na kuwaadhibu Wananchi wenzetu walio wangi mno!

Yeye ndo binafsi aloshiriki kwa kiasi kikubwa kuasisi/kushinikiza hata hii katiba iliyomo kwenye mchakato hivi sasa...ambayo hata wakti huo pia ilijulikana yakua ilikua mbovu,isiyojitosheleza na iliyokua imepitishwa kimabavu bila ya ridhaa sio tu ya Wanataaluma wa Katiba bali hata hao Wananchi wenyewe iliodaiwa yakua ati ndo ilikua inahitajika ili kuwawakilisha!? Daah!

Sina haja ya kwenda mbali mno/nje ya mada!

Kwa kifupi mambo haya yoote tuitayo ati ndo machafu na yalotokea/yatokeayo hivi sasa kwenye Taifa letu changa kama; ufisadi,Viongozi kutowajibika katika nyadhifa/nafasi zao,ubadhilifu ulokubuhu wa mali za umma,upendeleo wa kikabila/nepotism na kidini,ubovu wa Elimu,Mawaziri mizigo kubebwa/kubebana na mangineyo mangi mno...mbona hivi vyoote vilianzia kwenye ule utawala wa awamu ya mwanzo wa Nyerere aka "Baba wa Taifa"...nae haklusita kuyafumbia macho takriban yoote hayo!?

Sasa kwanini sisi wangine inakua haturuhusiwi au tunashutumiwa tuzungumziapo hivi vitu,tena kwenye majadiliano ya kawaida kwa tija ya Taifa letu!?...Tafadhali hapa sikulaumu weye binafsi asilan ndugu yangu,unafahamu fika jinsi gani ninavyokustahi na kukupenda!

Kuna haja gani ya wengi yetu kujaribu ku-glorify pasi kiasi yule Nyerere,wakti mweyewe binafsi alikiri tena mara kadhaa hadharani yakua amefanza makosa mangi mno kwenye kipindi cha utawala wake wa takriban zaidi ya miaka-20!?...hivi kweli tutakua tunajitendea haki sisi wenyewe kama Taifa au hata yule Nyerere mwenyewe...ikiwa tunajibana kumjadili kwa yoote kwenye kipindi/utawala wake!? Na tutajifunza vipi ikiwa hatutaki/tunakataza kurejea nyuma na kuchungulia historia yetu na tulipotokea!? Daah!

Nafahamu kiundani yakuwa realistically,ni tabu mno kulinganisha degree ya makosa yalotendeka katika vipindi/nyakati tafauti za Watawala/Marais tafauti!...sababu zipo kadhaa wa kidhaa!

Lakini kitaaluma hiyo si tabu,na wala pia kikawaida hilo pia si crime/criminal offence!

Sasa Mkuu JokaKuu...naona weye umeweka list ya majambo yako kiduchu hapo...nami pia nina list yangu kiduchu hapa kwa kumalizia!

Embu chungulia hawa baadhi tu ya Mawaziri waliokua mizigo pasi kiasi enzi ya "Mwalimu"/awamu tafauti za Rais Nyerere aka "Baba Wa Taifa"!

Hawa wengi wao walifanza ubadhilifu,uzinzi maofisini na majumbani mwao,rushwa,ubadhilifu/ufisadi wa mali za umma,upendeleano wa kikabila makazini na upuuzi mwangineo mwingi tu!

Lakini Nyerere aka "Baba Wa Taifa" huyu huyu,hakuwahi kuwaondoa madarakani kwa haraka au kuwawajibisha mara moja!

Wengi wao walidumu madarakani kwa kitambo kingi wakibadilishwa Wizara,vyeo au ajira na kujifaidia jasho adimu la Wananchi!

Kuna wengi mno,lakini kwa leo nakutajia hawa kiduchu ambao mie binafsi nikiwajua/nawafahamu kiundani vituko vyao mpaka kesho na families zao!

Joseph Rwegasira...Embu kumbuka japo kiduchu jinsi gani alivyokivuruga kile kiwanda cha nguo cha Urafiki-Ubungo alipokua GM pale kwa ukabila,uzinifu ulokubuhu kwa Wafanyakazi wa ngazi za chini,upendeleo wa kikabila(nafikiri wafahamu jinsi gani wakti wa Rwegasira jinsi gani palijaa Wahaya pale kuliko Kamachumu! Daah!),ubadhilifu na ufujaji wa mali na pesa za kiwanda na mangineyo mangi mno!

Nalistaajabu mno...Rais Ali Mwinyi nae ati alipoingia madarakani akampa Foreign Ministry mtu kama Rwegasira!? Hivi hao Viongozi wa Kiafrika huwa wanatumia mantik na Vetting za aina gani jamani!? Looh! Teeh! Teeh! Teeh!

Mzee Kida - Utakua bado wakumbuka jinsi gani yule Mchaga alivyoangamiza kile kiwanda cha pembejeo za kilimo UFI-Ubungo kwa myaka mingi mno wakti wa Nyerere,na aliweza kujilimbikizia foreign currency kubwa mno! Daah!

Na hawa wapuuzi wangine pia wakti huo...Arcado Ntagazwa,Alfred Tandau na Ibrahim Kaduma!

Hivi jamani ni kweli Ibrahim Kaduma kwa upuuzi wake woote ule na kutojua kwake kazi/kutowajibika...ati pia akapelekwa pale Mlimani-UDSM ati kuwa Vice Chancelor!? Daah! Maskini Tanzania!!

Alex Nyakyoma - Huyu nafikiri mie binafsi na Mkuu Jasusi tulishawahi kumgusia kiduchu nae Jasusi aliwahi kuniunga mkono kiduchu kwalo!

Huyu Nyakyoma,ndo alozidi kuwatajirisha hao METL na mpaka kesho ati ndo wanatajwa kwenye FORBES! Duuh! Kweli Tanzania nchi ya comedy jamani!

Wakti Mzee Lawrence Gama/TISS formely Usalama Wa Taifa na Zakaria Maftah/TAKUKURU fomerly Anti-Coruption Squad...walipopinga/waliposhauri hiyo vetting ya Nyakyoma asipewe GAPEX from the begining...Nyerere binafsi ndo ali-over rule that! Duuh! Baadae pia walipotaka/waliposhauri aondolewe...ni Nyerere mwenyewe alipinga tena,mpaka ile GAPEX ilopifikia kuangamia maskini!! Daah!

Kwa kifupi haya ya Gapex na Nyakyoma ni Topic ndefu mno na yenye kukera na kuhuzunisha mno...italazim labda tuirejee siku nyangine tukipata fursa njema!

Augustine Mwingira - Huyu nae vituko vyake na "Lord"Rajpar pale Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi havisemeki! Sasa embu tazama jinsi gani Nyerere alivyositasita kumfukuza kazi mara moja au ashitakiwe mahakamani!? Daah!

Huyu Mzee namfahamu uzuri mno na wanae takriban woote...wakti huo akitumia ile nyumba yake ya Mjimwema kama Weekend Lodge tu...na wakti ule wala pale Mjimwema hapajaitwa ati "kwa Mwingira"! Teeh! Teeh! Teeh!

Bhoke Munanka - Ufisadi na ubadhilifu alofanza na kuzidi kuliibia Taifa kwa kujilimbikiza mali nje ya nchi bila kuulizwa chohcote au kuwajibishwa! Huyu nafikiri alijichotea foreign currency zaidi alipokua pale Waziri wa nchi/Usalama!!?

Nicholas Kuhanga - Embu angalia huyu nae jinsi perfomance yake ilivyokua mahoka alipokua Waziri wa Elimu!? Duuh!

Lakini Nyerere hakuchoka asilan kuwahamisha/kuwasogeza sehemu nyangine za ulaji na wakaharibu zaidi kwingineko,wale takriban Viongozi wenzie woote wa awamu yake!

Labda ndo maana Marais waliofutaia awamu nyangine nao wameamua/waliamua kufuata mfano mwema wa "Baba wa Taifa"!? Teeh! Teeh! Teeh!

Baadae Kuhanga nae ati akapewa Vice Chancelor Mlimani-UDSM...na Rais Mwinyi akamalizia ati kwa kumpa zawadi ya Ubalozi Zaire!? Jamani,Daah!!

Aaron Chiduo na hata kile kibabu cha kizungu Leader Stirling - Nao pia mahoka na upuuzi wao ulikua mkubwa mno pale Wizrara ya Afya na kuzorotesha takriban mfumo wetu mzima wa afya wakti ule na labda ndo msingi tunaondelea nao mpaka kesho!?

Julie Manning - Huyu Mama nae alikua ndo mbovu kabisa...Judicial System yoote ilikua ni mahoka tupu!

Kuna mangi mno ya kuzungumzia na rushwa,unyama ulokubuhu wa Polisi wakti ule,mateso kwa Wananchi walokua hawana hatia na vituko vingine vingi mno...nafikiri hata nawe umegusia kiduchu hapo kwenye hiyo bayana yako!

Kwa kifupi yaani huyu Julie Manning, alishindwa asilan kurekebisha ile mifumo mibovu aloikuta kwenye hiyo inherited/Colonial Judicial System na pia alishindwa asilan kufanza effective implementation ya yale mema yalokuwapo!

Chediel Mgonja - Utamaduni na Vijana!? Teeh! Teeh! Teeh!

Abel Mwanga - Maendeleo na Utumishi.....Looh! Teeh! Teeh! Teeh!

Tabitha Siwale - Ardhi,Nyumba na Maendeleo mijini!? Looh!ahahaaaa!!

Mzee Isaack Sepetu - Ati Habari na Utangazaji!...nafikiri naliwahi kukwambia vituko vyake wakti ule akiwa Balozi ati anawakilisha Tanzania katika zile Eastern Block Countries!? Looh!

Hawa Samwel Sitta na John Malecela...nafikiri hawa mpaka leo ati bado wanajitahidi kuendeleza utumbo/upuuzi wao katika siasa za nchi hiyo...nafikiri itakua weye mwenzangu wawafahamu zaidi na nakwachia weye umalizie! Teeh! Teeh! Teeh!

Kwa kifupi hao nao pia katia ya yale matangopori mangine alotuachia Nyerere huyu huyu tunaeshinda mitandaoni kum-glamourise pasi kiasi!

Mie binafsi ni kati ya Wa-Tanzaia wachache mno nafikiri,ambao wala sistaajabu yakua kwanini leo nchi yetu imefikia hapo ilipo...kwani nafahamu yakuwa haijawahi kupata quality inayohitajika kwa mtu kuwa Kiongozi/Viongozi...hapa nazungumzia katika nyanja/nyadhifa takriban zoote za utawala na utumishi wa umma na hata mashirika binafsi pia!

We may need to avoid selective Memory!

Shukran kwa kunisikiza.

Ahsanta.

CC;Ritz
 
gombesugu, Rev. Kishoka,

..ninachopinga mimi ni huu utaratibu wa kumzushia Mwalimu Nyerere ambao umeibuka siku za karibuni.

..kwa mfano unakuta mtu anakuja hapa na kudai Mwalimu alikuwa mlarushwa!! REALLY?

..au mwingine anadai Mwalimu alikuwa mdini au mkabila, na anatetea madai yake kwa ushahidi wa kuungaunga, au uzushi wa waziwazi kabisa. mtu kama huyo lazima tumpinge kwasababu uko ushahidi wa wazi kabisa wa juhudi za Mwalimu ktk kupinga ubaguzi wa kidini, kikabila, rangi, na kijinsia hapa Tanzania.

..YES, wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere kulikuwa na mawaziri na viongozi ambao tunaweza kuwaita mizigo.

..tofauti ya Mwalimu Nyerere na maraisi waliomfuatia ni kwamba yeye alijiweka mbali kabisa na rushwa.

..pia Mwalimu alikuwa mkali, na hakutetereka, ktk kutetea maslahi ya Tanzania dhidi ya mataifa ya nchi, haswa mataifa makubwa.

NB:

..Kassim Hanga hakuuwawa na Mwalimu Nyerere, aliuawa na wa-Znz wenzake. Pamoja na hayo, mara ya mwisho Kassim Hanga kuonekane ilikuwa ni kwenye ule mkutano wa hadhara ambapo aliadhiriwa na Mwalimu Nyerere. Kwa msingi huo Mwalimu Nyerere needed to do or say something about Hanga's disappearance.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom