Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,539
- 4,854
IFUATAYO NI SEHEMU NYINGINE YA SHAIRI LILOANDIKWA NA IDD NINGA.
INGAWA MAUDHUI YA SHAIRI HILI YAMEJIFICHA LAKINI NI MARAHISI KUYAELEWA
1>ni majanga na balaa,nyoka anajibabua.
Kwa ndugu na majamaa,ngozi yeye ajivua.
Alozika ujamaa,dhambi anaijutia.
Simba atamla simba,nyumbu aliwa na mbugo.
2>machoni wamezubaa,mende atawazibua.
Itatumika sanaa,uongo kuufumua.
Msuko wa kitambaa,wenye ladha ya halua.
Simba atamla simba,nyumbu aliwa na mbugo.
3>panzi wanawahadaa,kwa kasi wanapumua.
Machoni wamezubaa,wamepakwa ndimu mua.
Wamemezeshwa miraa,bila kusoma barua.
Simba atamla simba,nyumbu aliwa na mbugo.
Shairi=SIMBA ATAMLA SIMBA.
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0755519736 au 0655519736
INGAWA MAUDHUI YA SHAIRI HILI YAMEJIFICHA LAKINI NI MARAHISI KUYAELEWA
1>ni majanga na balaa,nyoka anajibabua.
Kwa ndugu na majamaa,ngozi yeye ajivua.
Alozika ujamaa,dhambi anaijutia.
Simba atamla simba,nyumbu aliwa na mbugo.
2>machoni wamezubaa,mende atawazibua.
Itatumika sanaa,uongo kuufumua.
Msuko wa kitambaa,wenye ladha ya halua.
Simba atamla simba,nyumbu aliwa na mbugo.
3>panzi wanawahadaa,kwa kasi wanapumua.
Machoni wamezubaa,wamepakwa ndimu mua.
Wamemezeshwa miraa,bila kusoma barua.
Simba atamla simba,nyumbu aliwa na mbugo.
Shairi=SIMBA ATAMLA SIMBA.
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0755519736 au 0655519736