Idd Ninga kufuli ( shairi)

Idd Ninga kufuli ( shairi)

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,539
Reaction score
4,854
-----kufuli-----
=nyumbani alipofika,mke wangu
kamusia.
Kwa maneno ya hakika,baba
akamuambia.
Mumeo atapofika,usiache
mgusia.
Kufuli abadilishe,nyumba ije
kupendeza.
=mke nae kaneleza,baba
alichomwambi.
Nyumba itaja pendeza,tena itaja
vutia.
Ila nikija kucheza,maisha
nitajutia.
Kufuli yanitatiza,bado
sijaielewa.
=nyumba yangu ya kitasa,wala
haina kufuli.
Nimewaza hadi sasa,najihisi
nimefeli.
Napata majibu tasa,yaumizayo
akili.
Kufuli yanitatiza,bado
sijaielewa.
=nawaomba washairi,mnipe jibu
makini.
Nisije kupata shari,nikaumia
nyumbani.
Baya likaja kujiri,nikalia
maishani.
Kufuli kufuli gani,mimi
linanitatiza.
~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~ ~
 
Yaonesha u-mtembezi. Watumia mguu wa tatu.
Tia nyumbayo kufuli.
Baya lisijekupata!
 
Chagua nzuri kufuli,badae sije kujuta,ifate ikiwa mbali,nyumbani ndani kuleta,siulize mswahili,shimoni aje kutupa,tafuta kufuli bora,ulinzi kwa nyumba yako.
 
Duuh yan mlango wako wa ktasa afu unaambiwa ubadilishe kufuli haaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom