bullet proof
Member
- Sep 19, 2012
- 57
- 35
Zoezi linaloendelea nchini, la kuwakamata na kuwafukuza nchi wahamiaji haramu, limenifanya nifikiri juu ya ufanisi na hata uhalali wa idara hii nchini.
Taarifa zinaonyesha idadi kubwa ya wahamiaji haramu waliokamatwa katika msako unaondelea. Hili limenifanya ni hoji uhalali wa kuendelea kuwa na idara hii nchini, kwanini isivunjwe tu na shughuli za idara hii zifanywe na idara au vikosi vingine kama ilivyokuwa mwanzo katika jeshi la polisi?
Taarifa nyingi za uhamiaji hutolewa na jeshi la polisi nchini. Ukisikia sehemu wamekamatwa wahamiaji basi huwa wamekamatwa na polisi. Wale wanaokamatwa na Uhamiaji hufanywa "deal" tu na ndo maana tunaona rundo hili la wahamiaji haramu nchini.
Nashauri shughuli za idara hii zihamishiwe ofisi nyingine hasa ya usalama wa taifa au polisi kama zamani shughuli hizi zilivyokuwa zikifanywa na jeshi la polisi. Ulinzi wa mipaka utafanywa na jeshi la wananchi ambao ndio wenye dhamana ya kulinda mipaka na utoaji wa vibali mbalimbali vya uhamiaji kama vile passports, resident permits nk zitolewe na (kitengo) cha uhamiaji ambacho kitakuwa ndani ya usalama wa taifa/polisi hii ni kama ilivyo katika nchi nyingi duniani i.e huduma za uhamiaji na uraia ziko katika idara ya usalama wa taifa/polisi
Taarifa zinaonyesha idadi kubwa ya wahamiaji haramu waliokamatwa katika msako unaondelea. Hili limenifanya ni hoji uhalali wa kuendelea kuwa na idara hii nchini, kwanini isivunjwe tu na shughuli za idara hii zifanywe na idara au vikosi vingine kama ilivyokuwa mwanzo katika jeshi la polisi?
Taarifa nyingi za uhamiaji hutolewa na jeshi la polisi nchini. Ukisikia sehemu wamekamatwa wahamiaji basi huwa wamekamatwa na polisi. Wale wanaokamatwa na Uhamiaji hufanywa "deal" tu na ndo maana tunaona rundo hili la wahamiaji haramu nchini.
Nashauri shughuli za idara hii zihamishiwe ofisi nyingine hasa ya usalama wa taifa au polisi kama zamani shughuli hizi zilivyokuwa zikifanywa na jeshi la polisi. Ulinzi wa mipaka utafanywa na jeshi la wananchi ambao ndio wenye dhamana ya kulinda mipaka na utoaji wa vibali mbalimbali vya uhamiaji kama vile passports, resident permits nk zitolewe na (kitengo) cha uhamiaji ambacho kitakuwa ndani ya usalama wa taifa/polisi hii ni kama ilivyo katika nchi nyingi duniani i.e huduma za uhamiaji na uraia ziko katika idara ya usalama wa taifa/polisi