Idara ya Uhamiaji Arusha imejaa uozo, mamlaka husika ichunguze

Idara ya Uhamiaji Arusha imejaa uozo, mamlaka husika ichunguze

LESIRIAMU

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2008
Posts
9,213
Reaction score
14,924
Nimelazimika kuandika kuhusu Idara ya Uhamiaji Arusha kutokana na mwenendo wao wa kazi.

Wahudumu wa counter katika hali ya kawaida wanatakiwa wawe Customer Care wazuri kwa wanao hitaji huduma mahali popote.

Cha ajabu wahudumu walipo counter za Uhamiaji Arusha hawana Customer Care. Pia ni wala rushwa wakubwa.

Nijuavyo kuijaza for kuomba hati ya dharura unatakiwa kulipa 20,000/ tena upewe control namba ukalipe mwenywe
Lakini wahudumu wa Arusha hudai shs 30,000/ na kukuambia ufuate pass baadae au kesho yake.

Kama ni Passport kubwa 20,000/ unalipa kwenye mtandao. Ukipeleka pale uhamiaji unadaiwa 230,000/ yaani malipo ya pass 130,000/ na 100,000/ anachukua anae kuhudumia.

Najiuliza, hivi TAKUKURU ARUSHA wapo? TISS ARUSHA wapo!! Zaidi je Ofisa Uhamiaji Mkoa haoni haya yanayo endelea mbele ya macho yake.

Naomba Waziri wa mambo ya ndani aangalie kwa jicho la karibu huu wizi unaoendelea hapa Uhamiaji Arusha.
 
...we have wrong people in right places thats how we operate...
 
...we have wrong people in right places thats how we operate...
The issue is .. Do we need them to serve us?? Are they not paid by Goverment? We have Regional IMMAGRATION officer to manage them. What is he/she doing? Or he is a part of the circle??
 
Nimelazimika kuandika kuhusu Idara ya Uhamiaji Arusha kutokana na mwenendo wao wa kazi.

Wahudumu wa counter katika hali ya kawaida wanatakiwa wawe Customer Care wazuri kwa wanao hitaji huduma mahali popote.

Cha ajabu wahudumu walipo counter za Uhamiaji Arusha hawana Customer Care. Pia ni wala rushwa wakubwa.

Nijuavyo kuijaza for kuomba hati ya dharura unatakiwa kulipa 20,000/ tena upewe control namba ukalipe mwenywe
Lakini wahudumu wa Arusha hudai shs 30,000/ na kukuambia ufuate pass baadae au kesho yake.

Kama ni Passport kubwa 20,000/ unalipa kwenye mtandao. Ukipeleka pale uhamiaji unadaiwa 230,000/ yaani malipo ya pass 130,000/ na 100,000/ anachukua anae kuhudumia.

Najiuliza, hivi TAKUKURU ARUSHA wapo? TISS ARUSHA wapo!! Zaidi je Ofisa Uhamiaji Mkoa haoni haya yanayo endelea mbele ya macho yake.

Naomba Waziri wa mambo ya ndani aangalie kwa jicho la karibu huu wizi unaoendelea hapa Uhamiaji Arusha.
Kwa hiyo unakua unajua hiyo Tshs kwenye passport 100,000 ni cha juu. Hivi ukigoma kuwapa hiyo Tssh 100,000 watafanya nini, wakati hiyo Tshs 130,000 humkabidhi mkononi unaenda kuilipia kwa kutumia benki au Mpsa? Watakurudishia form zako?

Mara nyingine kutoa rushwa ni tabia tumejijengea wenyewe. Naelewa kumpa rushwa trafiki ambae amenikamata na kosa ili asiniandikie faini. Lakini nikupe rushwa kwenye haki yangu wakati kila document inayohitajika ninayo? Sikupi I say, hata ulie. Tena nitaenda kumwambia Regional Migration Officer umekataa kupokea form zangu unataka cha juu.
 
Watanzania ifike mahali tubadilike, nilipoona post hii nimepitia mtandao wa Uhamiaji kuhusu utoaji wa pasipoti...kila kitu katika mfumo huo kinafanywa electronically...unafanya maombi kwa njia ya mtandao na baadaye unalipia elfu ishirini na Kisha ukifika ofisini unalipa laki moja na 30 nayo pia unalipa benki au kwa mtandao wa simu. Katika mazingira Kama haya mtu anayekwenda kuwapa hao maafisa fedha cash analenga Nini? Unapodaiwa fedha tofauti na maelekezo yaliyowekwa na serikali unakuwa umedhamiria kutoa Rushwa.

Hata hati za dharura nazo unalipa kwa njia ya mtandao ofisi zao ni Kama zimesitisha kabisa kupokea fedha cash, wewe hizo unazotoa unalipia huduma gani?

Tuache kuwasumbua watendaji wa serikali, ifike mahali tuwe na nidhamu na tutambue anayepokea na anayetoa rushwa wote ni watuhumiwa.

Tukiendelea kulalamika wakati serikali imeshaweka utaratibu wa fedha zake zote kuingizwa kwenye akaunti tutakuwa hatutendi haki.

Lakini pia katika nchi yetu ipo tabia ya watu kutaka huduma za haraka Jambo linalowapelekea kuangukia mikononi mwa vishoka, wewe unajua una safiri mwezi ujao kwann usitafute hizo pasipoti mapema?

Lakini pia kuhusu watendaji wa uhamiaji upo umuhimu wa wao kuheshimu kilichoandikwa kwenye sheria, wasichana na vijana hawapewi pasipoti kwa wakati lakini wanakuwa na vigezo. Hali hii inachangia Rushwa , mwenye sifa ya kupewa pasipoti apewe pasipoti Mambo ya mdhamini wa serikali sijui vyeti vya shule huku tunamaombi ya safari binafsi siyo sawa na hakuna sehemu kwenye sheria imeandikwa hivyo vitu.

Mwisho niwapongeze idara ya uhamiaji kwa kweli ni moja ya idara iliyojirekebisha Sana awamu ya tano, pasipoti ndani ya wiki umepata. Utaratibu wameuweka wazi na kila mtu anaweza kupata huduma kwa urahisi.

Hongera Dr. Makakala ila washughulikie hao wachache wanaotia kitumbua chako mchanga.
 
Kwa hiyo unakua unajua hiyo Tshs kwenye passport 100,000 ni cha juu. Hivi ukigoma kuwapa hiyo Tssh 100,000 watafanya nini, wakati hiyo Tshs 130,000 humkabidhi mkononi unaenda kuilipia kwa kutumia benki au Mpsa? Watakurudishia form zako?

Mara nyingine kutoa rushwa ni tabia tumejijengea wenyewe. Naelewa kumpa rushwa trafiki ambae amenikamata na kosa ili asiniandikie faini. Lakini nikupe rushwa kwenye haki yangu wakati kila document inayohitajika ninayo? Sikupi I say, hata ulie. Tena nitaenda kumwambia Regional Migration Officer umekataa kupokea form zangu unataka cha juu.
Ndugu yangu jaribu kwenda pale uone huo muziki. Anakuambia network iko down acha pesa ikirudi nitakulipia. Ukiwa mjanja utalipia mwenyewe ila utaweza kukaa miezi pasport hupati
Maana yake process zitasimama. Kufika Dar docs zako utasikia kwenye bomba. Kuna victims wengi wa aina hiyo
 
Watanzania ifike mahali tubadilike, nilipoona post hii nimepitia mtandao wa Uhamiaji kuhusu utoaji wa pasipoti...kila kitu katika mfumo huo kinafanywa electronically...unafanya maombi kwa njia ya mtandao na baadaye unalipia elfu ishirini na Kisha ukifika ofisini unalipa laki moja na 30 nayo pia unalipa benki au kwa mtandao wa simu. Katika mazingira Kama haya mtu anayekwenda kuwapa hao maafisa fedha cash analenga Nini? Unapodaiwa fedha tofauti na maelekezo yaliyowekwa na serikali unakuwa umedhamiria kutoa Rushwa.

Hata hati za dharura nazo unalipa kwa njia ya mtandao ofisi zao ni Kama zimesitisha kabisa kupokea fedha cash, wewe hizo unazotoa unalipia huduma gani?

Tuache kuwasumbua watendaji wa serikali, ifike mahali tuwe na nidhamu na tutambue anayepokea na anayetoa rushwa wote ni watuhumiwa.

Tukiendelea kulalamika wakati serikali imeshaweka utaratibu wa fedha zake zote kuingizwa kwenye akaunti tutakuwa hatutendi haki.

Lakini pia katika nchi yetu ipo tabia ya watu kutaka huduma za haraka Jambo linalowapelekea kuangukia mikononi mwa vishoka, wewe unajua una safiri mwezi ujao kwann usitafute hizo pasipoti mapema?

Lakini pia kuhusu watendaji wa uhamiaji upo umuhimu wa wao kuheshimu kilichoandikwa kwenye sheria, wasichana na vijana hawapewi pasipoti kwa wakati lakini wanakuwa na vigezo. Hali hii inachangia Rushwa , mwenye sifa ya kupewa pasipoti apewe pasipoti Mambo ya mdhamini wa serikali sijui vyeti vya shule huku tunamaombi ya safari binafsi siyo sawa na hakuna sehemu kwenye sheria imeandikwa hivyo vitu.

Mwisho niwapongeze idara ya uhamiaji kwa kweli ni moja ya idara iliyojirekebisha Sana awamu ya tano, pasipoti ndani ya wiki umepata. Utaratibu wameuweka wazi na kila mtu anaweza kupata huduma kwa urahisi.

Hongera Dr. Makakala ila washughulikie hao wachache wanaotia kitumbua chako mchanga.
Naona hukunielewa, sija laumu idara yote ya Uhamiaji
Mimi binafsi kwa Dar nimewahi kupata pasport chini ya siku tatu. Soma kichwa cha habari. Hapa nalalamikia Arusha. Kuna watu wana zaidi ya miezi miwili bila kupata pasport na taratibu zote wame fanya.. Uhamiaji Arusha kama hujulikani sahau huduma nzuri. Nimezungumzia wanao toa huduma kaunta ila kuna walio vitengo vingine ni wazuri I can even mention them. Naongea kitu nilicho kutana nacho. Kama uko Arusha just go there. Ndio maana nauliza taasisi husika ziko wapi..
Ni issue ya marekebisho tuu. Mbona Polisi na idara nyingine marekebisho yalifanyika na mambo yanaenda? hawa wamezowea kazi.
 
Ndugu yangu jaribu kwenda pale uone huo muziki. Anakuambia network iko down acha pesa ikirudi nitakulipia. Ukiwa mjanja utalipia mwenyewe ila utaweza kukaa miezi pasport hupati
Maana yake process zitasimama. Kufika Dar docs zako utasikia kwenye bomba. Kuna victims wengi wa aina hiyo
Mkuu, hakuna hela ya passport au kitu chochoe inapaswa kulipwa kwa Uhamiaji. Hilo liliondolewa kuziba kuwapa cha juu. Na kama hiyo network iko down basi ni kwa wote, nmaana si mnakuwa wengi. Basi nitamwambia nitasubiri. Hivi vitu lazima tukomae kuvimaliza
 
Nimelazimika kuandika kuhusu Idara ya Uhamiaji Arusha kutokana na mwenendo wao wa kazi.

Wahudumu wa counter katika hali ya kawaida wanatakiwa wawe Customer Care wazuri kwa wanao hitaji huduma mahali popote.

Cha ajabu wahudumu walipo counter za Uhamiaji Arusha hawana Customer Care. Pia ni wala rushwa wakubwa.

Nijuavyo kuijaza for kuomba hati ya dharura unatakiwa kulipa 20,000/ tena upewe control namba ukalipe mwenywe
Lakini wahudumu wa Arusha hudai shs 30,000/ na kukuambia ufuate pass baadae au kesho yake.

Kama ni Passport kubwa 20,000/ unalipa kwenye mtandao. Ukipeleka pale uhamiaji unadaiwa 230,000/ yaani malipo ya pass 130,000/ na 100,000/ anachukua anae kuhudumia.

Najiuliza, hivi TAKUKURU ARUSHA wapo? TISS ARUSHA wapo!! Zaidi je Ofisa Uhamiaji Mkoa haoni haya yanayo endelea mbele ya macho yake.

Naomba Waziri wa mambo ya ndani aangalie kwa jicho la karibu huu wizi unaoendelea hapa Uhamiaji Arusha.
Nimeomba hati ya dharura arusha wiki iliyopita. Kwa kweli sijaombwa rushwa yoyote. Nimelipa tu hiyo elfu ishirini baada ya kupata control number. Inawezekana wanakuchek umeenda vipi, wakiona mrugaruga wanakupiga. Ila hawaombi directly.

Kuhusu customer care ni kweli jamaa hawaelekezi vizuri. Wamebandika katangazo kao, ukiuliza chochote wanakwambia kasome ukutani. Nahisi ni sababu ya uwingi wa watu nao wanachoka explaining the same shit all day. They are human after all.
 
Mtoa mada tuelimishane, yapo mapungufu katika ofisi za umma ila tusipoyajadili tutadili na watu wasiohusika, issue ya network down ni tatizo hata benki lipo.

Lakini pia umewatuhumu ofisi nzima kwa issue yako binafsi, unasema ulitoa laki tusaidie ulitoa kwa ajili ya huduma gani? May be ninyi ndo bado mnapesa nyingi za kuonga wakati sisi hatuna hata buku. Mkiwepo watoa laki mnatufanya nasisi tukoseshwe huduma Hadi tutoe pesa.

Takukuru badala wanapaswa wawakamate ninyi watoa rushwa
 
Mtoa mada tuelimishane, yapo mapungufu katika ofisi za umma ila tusipoyajadili tutadili na watu wasiohusika, issue ya network down ni tatizo hata benki lipo.

Lakini pia umewatuhumu ofisi nzima kwa issue yako binafsi, unasema ulitoa laki tusaidie ulitoa kwa ajili ya huduma gani? May be ninyi ndo bado mnapesa nyingi za kuonga wakati sisi hatuna hata buku. Mkiwepo watoa laki mnatufanya nasisi tukoseshwe huduma Hadi tutoe pesa.

Takukuru badala wanapaswa wawakamate ninyi watoa rushwa
Naona una tetea hongo. Ninge kuwa nimetoa nisinge lalamika. Nasema nendeni pale mkaone mchezo unao fanywa pale. Najua taratibu zote za malipo ya serikali kwa sasa. Ila nimesema kuna tatizo la watumishi kwenye hiyo idara. Kabla ya kuninyooshea kidole taasisi zipo zifuatilie utendaji wa watumishi pale. Na nimesema, kuna baadhi wanatoa huduma nzuri.
 
Watanzania ifike mahali tubadilike, nilipoona post hii nimepitia mtandao wa Uhamiaji kuhusu utoaji wa pasipoti...kila kitu katika mfumo huo kinafanywa electronically...unafanya maombi kwa njia ya mtandao na baadaye unalipia elfu ishirini na Kisha ukifika ofisini unalipa laki moja na 30 nayo pia unalipa benki au kwa mtandao wa simu. Katika mazingira Kama haya mtu anayekwenda kuwapa hao maafisa fedha cash analenga Nini? Unapodaiwa fedha tofauti na maelekezo yaliyowekwa na serikali unakuwa umedhamiria kutoa Rushwa.

Hata hati za dharura nazo unalipa kwa njia ya mtandao ofisi zao ni Kama zimesitisha kabisa kupokea fedha cash, wewe hizo unazotoa unalipia huduma gani?

Tuache kuwasumbua watendaji wa serikali, ifike mahali tuwe na nidhamu na tutambue anayepokea na anayetoa rushwa wote ni watuhumiwa.

Tukiendelea kulalamika wakati serikali imeshaweka utaratibu wa fedha zake zote kuingizwa kwenye akaunti tutakuwa hatutendi haki.

Lakini pia katika nchi yetu ipo tabia ya watu kutaka huduma za haraka Jambo linalowapelekea kuangukia mikononi mwa vishoka, wewe unajua una safiri mwezi ujao kwann usitafute hizo pasipoti mapema?

Lakini pia kuhusu watendaji wa uhamiaji upo umuhimu wa wao kuheshimu kilichoandikwa kwenye sheria, wasichana na vijana hawapewi pasipoti kwa wakati lakini wanakuwa na vigezo. Hali hii inachangia Rushwa , mwenye sifa ya kupewa pasipoti apewe pasipoti Mambo ya mdhamini wa serikali sijui vyeti vya shule huku tunamaombi ya safari binafsi siyo sawa na hakuna sehemu kwenye sheria imeandikwa hivyo vitu.

Mwisho niwapongeze idara ya uhamiaji kwa kweli ni moja ya idara iliyojirekebisha Sana awamu ya tano, pasipoti ndani ya wiki umepata. Utaratibu wameuweka wazi na kila mtu anaweza kupata huduma kwa urahisi.

Hongera Dr. Makakala ila washughulikie hao wachache wanaotia kitumbua chako mchanga.

Kiukweli uhamiaji wamebadilika sana
 
Back
Top Bottom