I had a dream, nimeota ndoto

I had a dream, nimeota ndoto

Joined
Sep 3, 2025
Posts
5
Reaction score
3
Ni usiku ulio gubikwa na ndoto, ndoto zilizo na matukio mengi mithilli ya maisha halisi zilinifanya nifikirie sana ila kuna hii ndoto ilichukua muda mpaka kufikiria ni nini nimeota au niliona kwa uhalisia?

Nimeota ndoto, ndoto ya mtu aliye na majukumu mazito, yalio tokana na harakati fulani za muda mfupi, ni majukumu anayo fanya mwenyewe na mengine ya kuelekezwa, mtu mwenye haki alie pewa mzigo mzito abebe japo alipenda awe huru kwa sasa, "nilimuona amesimama ndani ya chumba chenye meza ya mbao yenye rangi ya udongo akiinamisha shingo chini, akisema moyoni amechoka", sijajua kama ameshaeleza wengine maana ni nafasi nzito na ya kuaminiwa sana

Siku zote nakuona binadamu ulie na upendo, nimekuona na toka nikuone nilionaa upendo, usikivu na faraja yako binafsi kwa watu wengine, huenda wasielewe kwa sasa ila una upendo, mwenye enzi akulinde kiongozi

Binafsi naelewa uzito huu mwenye enzi hii akupe nguvu awape hekima wote wanao kuzunguka ni mazito jipe moyo kiongozi wangu, naimani hili litapita omba mungu sana, kwa nafasi ulio aminiwa ni nafasi nzito, nashindwa niandike nini ila ukiona moyo na nafsi havitaki kabisa tafuta hekima ili uwe na amani

Kweli huenda ni ndoto, I had a dream...
 
Ikitumika hekima na busara kiongozi wangu, basi Tanzania itakuwa salama na watanzania watafikiria juu ya msamaha wa kweli
 
Back
Top Bottom