Ninachotaka kusisitiza hapa ni kwamba, wale wanaoomba nafasi ya urais hawapaswi kutuhumiwa kwa jambo lolote. Hawapaswi kutiliwa mashaka kuhusu uadilifu wao. Wanapaswa kuaminiwa kuhusu dhamira yao ya kupiga vita ufisadi na rushwa.
Na wagombea hawa tunaweza kuwajua kutokana na hulka au tabia za marafiki zao Watanzania tukumbuke kwamba utumishi wa umma ni dhamana na fursa adhimu kwa ajili ya kulinda na kutetea maslahi ya wananchi wote. Na ni dhahiri kuwa kwa sifa hizo JOHN POMBE MAGUFULI ndiye anatufaa kama watanzania na ni kiongozi asiye tiliwa shaka kwa namna yeyote ile. ‪
#‎HapaKaziTu‬‪#‎Tumekusikia‬
Wewe ndiye unaeamini kuwa Magufuli ni kiongozi asiyetiliwa shaka. Mimi siamini hivyo, We mpe kura yako Magufuli mi nampa kura yangu Lowassa. Simple tu. Bado maamuzi ni yangu wala sihitaji ushawishi kama huu.
MAGUFULI MSHINDANI WAKE SI LOWASSA,WANAPISHANA KWA MBALI SANA UADILIFU NA SIFA,HIVYO JPM NI MSHINDI TU,NA YEYE NI MUADILIFU ZAIDI YA lowassa ,HAPA KAZI TU
Nyakati hizi kuna watu wataukwaa utakatifu kwa mitazamo ya aina hii . Yaani mtu anaweza akajilinganisha na anaeitwa msafi akajiona yeye ni mtakatifu kabisa.
Inapendez kuona watanzania wengi bado tunajitambua na tunajali mustakabari wa nchi yetu. Wale walio pofushwa akili tunawaombea kwa Mungu ila HATUTAWAANGUSHA. Watanzania wengi tumeshaamua na tutawachagulia rais ambaye mtajivunia na mtakuja kutushukuru siku za mbele. HUU NDO UKWELI AMBAO WATANZANIA WENGI TUNAUJUA NA NDIO TULIVYOAMUA, TUTAMCHAGUA JPM KUWA RAIS WA JMT, WATANZANIA WENGI TUMEAMUA HIVYO.
Hatuwezi yumbishwa na kugeuzwa geuzwa kama chapati na watu wasio na msimamo na wasio jitambua.
Tanzania tumeamua HIVYO.
Hakika kama kweli upinzani ukishindwa kushika dola mwaka huu sioni kama kuna wakati mwingine watu watakuwa na muamko kama sasa.....Watu wamepikwa wakaiva kutaka mabadiliko cha msingi tu mipango mikakati iwekwe dhabiti ya kudhibiti wizi wa kura ama ubatilishaji wa matokeo ya kura.