habari zenu wapendwa, kuna kaka mmoja alinipigia sim lakini akawa amekosea namba baada ya kujua kua kakosea akaniomba samahani nami nikaendelea na zangu, kilichonishangaza alinipigia tena na kunambia kuwa kavutiwa na sauti yangu hivyo kanipenda vyovyote nilivyo na lengo lake ni kuoana, sikumpa jibu rasmi ikawa tunaendelea kuwasiliana akaomba aongee na mama nikamkubalia sasa alipoongea nae akajitambulisha kuwa mimi ni mpenzi wake anataka kuja ili wajuwane, basi akafahamishwa mpaka nyumbani akaja akakaribishwa vizuri, sasa baada ya kuondoka akanitumia sms na kusema kuwa kazidi kuchanganyikiwa anaomba nisimtose nimkubalie tu ili aniowe, swali lipo hapa huyu jamaa hajawahi kunihuduia hata sent zaidi ya vocha nimaneno matupu hivi nikweli ana mapenzi yakweli? nisaidieni jamani nisijejuta kwa uamuzi nitakaotoa.