jamani nishaurini vizuri sitaki nipendeze lakini angalau angeonesha vijidalili hali yangu ya maisha anaijua na anajua sina wa kunihudumia lakini pengine anadharau hata hivyo suala la kunionja asiweke akilini mwake hata angenihudumia kiasi gani natunza heshma yangu
akuhudumie kwani we kiwete?
mimi si kiwete nashkuru ila nilimueleza historia ya maisha yangu na zaidi nahitaji kusoma tangu afariki baba nimekosa msaada wa kifamilia ila ukweli baada ya kumuona nilimpenda kweli lakini sasa ananirudisha nyuma
Kama unaona hakufai achana naye...na kama unampenda mwambie aache ubaili akutwae uwe mwandani wa yeye.
Wanaume sie tunachelea kuwagharamia maana hamchelewi kugeuka nyie akina Amina..na kutafuta makuu zaidi.mimi si kiwete nashkuru ila nilimueleza historia ya maisha yangu na zaidi nahitaji kusoma tangu afariki baba nimekosa msaada wa kifamilia ila ukweli baada ya kumuona nilimpenda kweli lakini sasa ananirudisha nyuma
habari zenu wapendwa, kuna kaka mmoja alinipigia sim lakini akawa amekosea namba baada ya kujua kua kakosea akaniomba samahani nami nikaendelea na zangu, kilichonishangaza alinipigia tena na kunambia kuwa kavutiwa na sauti yangu hivyo kanipenda vyovyote nilivyo na lengo lake ni kuoana, sikumpa jibu rasmi ikawa tunaendelea kuwasiliana akaomba aongee na mama nikamkubalia sasa alipoongea nae akajitambulisha kuwa mimi ni mpenzi wake anataka kuja ili wajuwane, basi akafahamishwa mpaka nyumbani akaja akakaribishwa vizuri, sasa baada ya kuondoka akanitumia sms na kusema kuwa kazidi kuchanganyikiwa anaomba nisimtose nimkubalie tu ili aniowe, swali lipo hapa huyu jamaa hajawahi kunihuduia hata sent zaidi ya vocha nimaneno matupu hivi nikweli ana mapenzi yakweli? nisaidieni jamani nisijejuta kwa uamuzi nitakaotoa.