Huyu Engineer wa Wilaya ya Kinondoni bure

Huyu Engineer wa Wilaya ya Kinondoni bure

Megawatt B

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2011
Posts
259
Reaction score
69
Inasikitisha sana. Barabara inayotengenezwa kutoka Namanga hadi Kondo pale Tegeta haina hata vijimfereji.

Wameshindilia udongo vizuri, sawa, lakini kama hakuna mifereji ya kupitisha maji ni bure kabisa.

Mvua zikija udongo wote barabarani utaondoka. Utaaalamu gani huu?
 
Udongo??? Hii kali! Ninavyofahamu mie barabara hazijengwi kwa udongo.Wanatumiaga gravel material ya kiwango G3, 7, 15, or above!
 
Unashangaa nini sasa BekaNurdin? Ndiyo hivyo, kuna barabara moja nayo iko wilaya ya Kinondoni pia yaani ni majangaa tu, kila mwaka barabara ya mpigi magoye
 
Last edited by a moderator:
Mkuu unashangaa Kinondoni? Mbona ndio barabara nyingi za Kitanzania zinavyojengwa?

Ndiyo maana Dar ikinyesha mvua maji kila mahali, hakuna proper drainage system.

Kwa hiyo usimlaumu huyu pekee, ndio mainjinia wetu walivyo.
 
mkuu unashangaa kinondoni? Mbona ndio barabara nyingi za kitanzania zinavyojengwa?

Ndiyo maana dar ikinyesha mvua maji kila mahali, hakuna proper drainage system.

kwa hiyo usimlaumu huyu pekee, ndio mainjinia wetu walivyo.
kwa kiswahili.....
 
Megawatt B

Kumbe mainjinia wa majina sio kwetu tu hata kwenu wapo.
Tuwe pole.
 
Last edited by a moderator:
Megawatt B

Budget zakuunga unga na irrational decisions ndo zinazowaangusha Mainjinia wa halmashauri au manispaa, ndo maana utaalamu wao unatiliwa shaka...Politic is running tz everywhere!
 
Last edited by a moderator:
sio engineer wa kinondoni peke yake..
wengi ujuzi\uzoefu wao unatia mashaka hasa ktk ubunifu, usimamizi na utaalamu wao.
 
Inasikitisha sana. Barabara inayotengenezwa kutoka Namanga hadi Kondo pale Tegeta haina hata vijimfereji.

Wameshindilia udongo vizuri, sawa, lakini kama hakuna mifereji ya kupitisha maji ni bure kabisa.

Mvua zikija udongo wote barabarani utaondoka. Utaaalamu gani huu?

Alilipwa kiasi gani ? Usijeshangaa amekopwa na humo humo 10% unadhani atafanya kazi ya kiwango?
 
Udongo??? Hii kali! Ninavyofahamu mie barabara hazijengwi kwa udongo.Wanatumiaga gravel material ya kiwango G3, 7, 15, or above!

Hivi hiyo gravel (au changarawe kwa kiswahili) siyo udongo mkuu? Mbona tukisoma kidogo tunajitoa ufahamu na kujiona kama tunajua saaaaaaana. Ndugu yangu huo ni udongo unaochimbwa ardhini na kwenda kusambazwa barabarani kwa grader na kisha kushindiliwa kwa roller. Huwezi kutuambia gravel materials siyo udongo!!! ukisema gravel materials ya kiwango sijui G3, 7, 15, or above ni kama vile materials fulani zimetengenezwa kiwandani???? Huo ni udongo tu ambao umekua selected kwa sababu ya properties zake kwamba unakua compacted tofauti na mchanga.
 
Hivi hiyo gravel (au changarawe kwa kiswahili) siyo udongo mkuu? Mbona tukisoma kidogo tunajitoa ufahamu na kujiona kama tunajua saaaaaaana. Ndugu yangu huo ni udongo unaochimbwa ardhini na kwenda kusambazwa barabarani kwa grader na kisha kushindiliwa kwa roller. Huwezi kutuambia gravel materials siyo udongo!!! ukisema gravel materials ya kiwango sijui G3, 7, 15, or above ni kama vile materials fulani zimetengenezwa kiwandani???? Huo ni udongo tu ambao umekua selected kwa sababu ya properties zake kwamba unakua compacted tofauti na mchanga.

Imekuuma ee? Walioku-like wamesoma soil science kama wewe!
 
Ungefanya uchunguzi kwanza na kujua kilichopelekea barabara hiyo kujengwa hivyo kabla ya kukurupuka na kumlaumu Mhandisi wa ujenzi wa kinondoni.Inaweza kuwa yeye hakuhusika au Bajeti ilikuwa ndogo n.k
 
Back
Top Bottom