Huu ni mkono wa nani?

Huu ni mkono wa nani?

Criterion

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2008
Posts
11,797
Reaction score
11,899
Awiii Uwiii Awoo! ni vilio kila kona.
Viiana, wazee nao, alo salama hakuna,
Nchi ni maombolezo, mazikoni twapishana.
Tumwendee Mungu Baba, yeye ni mwenye rehema.

Awali tunakumbuka, virusi vilisheheni,
Pamoja tulianguka, tukaenda magotini,
Pasipo kuwa na shaka, pembezoni na mijini,
Mungu aliturehemu, dunia kuishangaza.

Imetupasa kujua, Mungu ndiye mwenye haki,
Huponya tukimwendea, ila uovu hataki,
Ataondoa balaa, na salama tutabaki,
Tukimrudia Baba, taifa litaokoka.

Sisi sote tumekosa, tumefanya machukizo.
Uovu tumetakasa, hila tumefanya nguzo.
Kila kukicha ni visa, uharifu ni gumzo,
Kwa macho yetu twaona, mwisho wa wetu uovu.

Wanaume wanawake, kabila na rangi zote,
Mungu na tumkumbuke, hata tukiwa fungate,
Akunje upanga wake, la sivyo twaisha sote.
Tukimwomba na kutubu, Mungu ataturehemu.

 


Awiiiiii Uwiiiiiiiiii awoooooooooooo, ni vilio kila kona.
Vihana, wazee nao, aliye salama hakuna,
vilio maombolezo, mazikoni twapishana.
Tumwendee Mungu Baba, yeye ni mwenye rehema.

Awali katika tunakumbuka, virusi vilisheheni,
Pamoja tulianguka, tukaenga magotini,
Pasipo kuwa na shaka, pembezoni na mijini,
Mungu aliturehemu, dunia kuishangaza.

Imetupasa kujua, Mungu ni mwenye haki,
Huponya tukimwendea, ila uovu hataki,
Ataondoa balaa, na salama tutabaki,
Tukimrudia Baba, taif litaokoka.

Sisi sote tumekosa, tumefanya machukizo.
Uovu tumetakasa, hila tumefanya nguzo.
Kila kukicha ni visa, uharifu ni gumzo,
Kwa macho tunayaona, malipo ya wetu uovu.

Wanaume wanawake, kabila na rangi zote,
Mungu na tumkumbuke, hata ukiwa fungate,
Ashushe upanga wake, la sivyo twaisha sote.
Tukimwomba na kutubu, Mungu ataturehemu.


Noma kweli
 
Za asubuhi habari, huu ni wangu ujumbe,
Wengi huita shairi, kwa pamoja na tuimbe,
Tuko katika hatari, mwambie hata mjumbe,
Tumililie Muumba, aiponye yetu nchi.
Mm naweza kufanya video music, kama audio iko tayari bc tufanye kazi mzee
 
Back
Top Bottom