Huu ndio utaratibu unapoingia kwenye Gari ya mtu

Zemanda

JF-Expert Member
Jan 10, 2021
6,835
14,328
Gari ni kitu nyeti na cha pekee sana kwa wanaume na hivyo kukipenda ni sehemu ya ibada ya kiume ili kuishi vizuri na kupata heshima kwenye jamii. Mapenzi ya gari kwa mwanaume hayawezi mithirika kuna muda anaweza kulipenda gari na kulitunza kushinda namna anavyomtunza mke.

Usije mlaumu mwanaume kwa hili ni asili yetu, magari huwa tunayaita toys kwasababu hii. They are part of our being.

Yafuatayo ni masharti nitakudokeza ambayo utatakiwa kufuata unapoingia kwenye gari ya mwanaume na uyazingatie ili akuone wewe ni sehemu ya familia.

1. Fungua mlango wa gari kwa adabu, usitumie hasira, kisirani wala kiherehere kufungua mwanaume atajua maana ukiligusa gari lake mifumo yake ya fahamu yote itakusoma kujua kuwa unaligusaje. Kuwa makini sana unapogusa kitasa kile na kufungua, fungua kama unafungua mlango wa chumbani kwa mkweo, au kitasa cha mlango wa ofisi ya raisi pale ikulu. Kuwa na adabu.

2. Unaona hapo ukishafungua mlango, kuna kakizimba sijui tuite kamuinuko ka frame ya mlango wa gari, ile sehemu ambayo unyayo wako utaivuka ili kukanyaga ndani. Ile sehemu watu wengi aidha kwa makusudi au bahati mbaya hujikuta wameburuta mguu pale na kuacha mchanga, tope, vumbi au tope. Ni bora umpake mwanaume mkaa usoni kuliko kufanya hicho kitendo. Hakikisha mguu wako kwanza ni msafi na haugusi kale kasehemu mwenye gari atakuchukia trust me na ukishuka atakulaani.

3. Ukishazingatia usafi wa mguu wako then hautakuwa na shida kuweka pale kwenye ile foot floor mat. Itazame kwa umakini kama ni ya pamba/sufi/kapeti na mguu wako ni mchafu ni bora uvue viatu tu kwasababu hutaki kujua mwanaume atakufikiriaje akiona unakanyaga na mamiguu yako machafu sehemu takatifu kama ile. Ukiona ameweka ya plastic the shukuru amekurahisishia kazi ila bado isiwe sababu ya kuingia na miguu michafu ukiweza isafishe kabla haujapanda, mwanaume atakupenda.

4. Unapofunga mlango funga kama unaweka glass kwenye meza ya kioo, usitumie nguvu, kile kishindo kinaweza kumpa mwanaume stroke especially kama gari yenyewe tunayozungumzia ni toleo linalokimbiza mjini na ni plate namba E. Kuwa makini. Narudia tena, usibamize mlango kwasababu yoyote ile funga taratibu kama mwizi anataka kutoka sehemu alipoiba. Mwanaume ukilipenda gari lake anaweza kukupa hela bila sababu sababu unathamini kitu anachothamini hata kama ni mkewe.

5. Ukiingia kwenye gari utulivu ni kanuni muhimu sana ya kushika. Acha mapepe na kutumia vibaya uhuru wa kufanya chochote utakachojiskia, gari sio lako ni la mwanaume kaa kwa kutulia. Kwann unakuwa na maamuzi sehemu isiyo kuwa yako.

6. Acha kujifanya unajua Audio au video navigation kwa kuanza ujuaji wa kuongeza au kupunguza sauti ya redio, kubadilisha channel, kupeleka mbele au kurudisha nyuma muziki, kuconnect simu yako kwa Bluetooth kwasababu unataka kusikiliza nyimbo za kwenye simu yako eti za mwenye gari ni mbaya na kadhalika.

Mwenye gari anapokuwa ametune vitu vyake katika entertainment section yake ni kosa kubwa sana kumtoa katika program yake aliyokuwa ameweka, unaweza muhairibia siku au kumharibia mood ndani ya gari lake na atakuona kero na siku nyingine hatotamani uwepo kwenye gari lake hata siti ya nyuma.

7. Acha kukaa mikao kama upo beach kwa kupandisha miguu kwenye dashboard, siti au kuikalia au kujitanua kiasi kwamba anaona wazi kabisa huyu mtu anajaribu kuvimba katika gari yangu, hiyo haina tofauti na kumshikashika mke wake hatofurahia hizo tabia. Acha mara moja.

8. Acha kulalamika kuhusu AC unless ni joto sana na unasweat au ni baridi sana hadi unaisikia kwenye mfupa. Trust me yeye atajua hata usiposema ataona tu unaweweseka au unasweat utaona ameshusha speed ya AC au atapandisha vioo awashe Ac kama kuna joto sana. Usijipe mamlaka ya kuamua hilo ndani ya dakika chache ukishaingia ndani ya gari.

9. Usije ukathubutu kuchungulia dashboard kutazama milage, meter ya mafuta au chochote hiyo siyo kazi yako ndio maana waliweka hizo vitu kwenye upande wa dereva na hata gari ambazo zimeweka katikati pale usitazame kwa kutumia nguvu tazama kwa wizi sana na usicomment chochote.

10. Usije ukathubutu kumpa maelekezo ya namna ya kuendesha au wapi pa kupita mwanaume anapoendesha gari yake sababu atakuchukia sana na unaweza msababishia mfadhaiko wa kuendesha gari asifurahie uwepo wako muda huo na ukishuka atajilaumu sana.

11. Acha kuuliza bei ya gari au taarifa za gari kama bima usajiri. Sio kila m'miliki anapenda kushare taarifa nyeti. Wengine gari zao ni za bei ila taarifa zao za kuzipata sio rahisi kushare so tuliza kitenesi.

Na kadhalika.

Acha kumkera mwanaume kwenye gari lake.
 
Namba 4 hiyo ilifanya nilimpatia moto rafiki yangu nikamuuliza kwanza ni makusudi au ni bahati mbaya umefanya, ni nani alikwambia kufunga lazima ubamize mlango kwa nguvu kiasi hiki hana majibu, sasa hivi anafunga kama anaweza glass kwenye meza ya kioo
 
Back
Top Bottom