Wewe kibaka na huyo Polepole mtueleze Ben Rabiu Saanane mlimfanyia yote yale kwa sababu gani , wakati alitoa maoni binafsi kama katiba inavyompa mtu uhuru kutoa maoni .
Polepole hajamaliza baada ya hili aombe radhi kwa yaliyofanywa akiwa kwenye kile kiti enzi za dikteta wa Chato.
Leo hii Chato ni kama Gbadolite kwa Joseph Mobutu.
Madaraka ni kitu cha kupita usiumize watu kisa madaraka hata huyu Samia atapita na kutoka hapo juu kuna watu watakuja kujifanya wasafi baada ya kuwa nje ya viti vya maamuzi wakati kipindi wapo walivitumia kuumiza watu.
Maisha anayoishi mjukuu wa mzee Kibao tangu mwaka jana sio sawa na anayoishi mjukuu wa Samia naye aitwaye Samia maana yule wa mzee Kibao tuliomuona kwenye picha akiwa na babu yake hana babu tena wa kucheza nae na kumsimulia hadithi wakati wa Samia anaishi katika raha bila kuwaza hata kuna kutekwa ,kutolewa macho na kumwagiwa tindikali maana anaye babu anayelindwa 24/7 huku akisikia kauli ya kishenzi kwamba babu yake amekufa sababu kifo ni kifo.
Wajukuu hawa wawili daima wakikutana nadhani hakutakuwepo na usalama wala amani huko siku za usoni tukijaliwa kuwepo utaweza kusikia sasa vile visasi vya kifamilia kama amabvyo tuliwahi sikia kwa nchi jirani hakika huu haukuwa utamaduni wa mtanzania hapo kabla.
Kwenye hili bado Polepole anadaiwa madeni yake ya awamu ya 5.