lubano jr
Member
- Apr 25, 2019
- 67
- 118
Utaratibu wa mjamzito kuanza kliniki zimekua na changamoto kubwa kwa hasa wananchi wa kipato cha chini. Nimehudhuria kliniki kwa mara ya kwanza nikiwa na mke wangu kama taratibu zao zinavyosema kwenye hospitali ya serikali ya Tandale lakini utaratibu wanasema umebadilika.
Kuanza kupata huduma ni lazima ulipie kuanzia kadi ya kumuona daktari Tsh 2000/= akuandikie vipimo vyote zaidi ya 6 ambayo gharama yake ni Tsh 15,000/= ndio mjamzito aanze kliniki, kama huna uende nyumbani.
Sasa nimejiuliza kwa hawa wenzangu na mimi wasiokuwa na kipato watahudumiwa na nani? Serikali iliangalie hili kupitia Wizara ya Afya watoto wengi watazaliwa majumbani tena wakiwa na matatizo kibao ambapo serikali itakuja kutumia nyingi kununua chanjo na madawa.
Kuanza kupata huduma ni lazima ulipie kuanzia kadi ya kumuona daktari Tsh 2000/= akuandikie vipimo vyote zaidi ya 6 ambayo gharama yake ni Tsh 15,000/= ndio mjamzito aanze kliniki, kama huna uende nyumbani.
Sasa nimejiuliza kwa hawa wenzangu na mimi wasiokuwa na kipato watahudumiwa na nani? Serikali iliangalie hili kupitia Wizara ya Afya watoto wengi watazaliwa majumbani tena wakiwa na matatizo kibao ambapo serikali itakuja kutumia nyingi kununua chanjo na madawa.