Huduma za mwendokasi

uchumi2018

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2018
Posts
2,087
Reaction score
2,993
Salaam wakuu,
kama kichwa kinavyojieleza,kiukweli mimi binafsi nilikuwa na matumaini makubwa na huduma ya mwendokasi kwamba atakuwa mkombozi wahuduma za usafirishaji jijini Dar. Miaka ya nyuma nilikuwa naishi Maeneo ya Tabata kwa hiyo sikuwa mtumiaji wa huduma hii,lakini niliamini itasaidia sana watumiaji hasa mida ya asubuhi wakati wa kwenda kazini.

Sasa baada ya kuhamia Maeneo ya mbezi ya kimara,kwa kweli huduma hii ni mateso matupu hasa kwa route za kkoo na posta maana asubuhi ni mateso matupu, Napendekeza zianzishwe dala dala za kutokea mbezi kwenda kariakoo na posta wakati wamiliki wa mwendokasi wanajipanga kihuduma ili kutupunguzia mateso sisi watumiaji wa usafiri kutoka mbezi kwenda kati kati ya jiji.

Je,mkazi wa mbezi ya kimara,nini maoni yako juu ya hili?
karibuni.
 
Huo mradi ndio uhalisia wa kila sekta kwenye hii awamu na bibi yupo anacheka cheka tu
Dah,kiukweli wananchi tunateseka sana.ukitaka kuona ninalolisema nenda kituo cha kimara kuanzia saa kumi na mbili asubuhi hadi saa moja,watu wanasukumana hovyo kama unaumwa unaweza anguka na kukanyagwa.
ndo maana nikashauri kama ni kweli kuna upungufu wa magari,waruhusu wamiliki wa dala dala waanzishe route za mbezi kariakoo na posta ili kusaidia wananchi wakati huyo mwekezaji anajipanga.
 
Hivi ajuza NI tusi....Kama sio linafaa litumike sehemu ya chorus kwa Wana praise timu...
 
Wao wanafikiri wakirudisha ruti za daladala kwenda kariakoo (maana zilikuwepo) wataua biashara ya mwendokasi, jambo ambalo si kweli.
 
Wao wanafikiri wakirudisha ruti za daladala kwenda kariakoo (maana zilikuwepo) wataua biashara ya mwendokasi, jambo ambalo si kweli.
Mambo mengine inabidi kukubaliana na hali halisi badala ya kuangalia faida wakati uwekezaji ni almost zero.
Walianzisha route ya kibaha na mabasi yalikuwa yanajaza nyomi,wakasema wanasitisha kwa muda,huo muda ndo imekuwa moja kwa moja.Na hakuna mabasi ya kuja mjini kama zamani.
 
Hivi sababu ya kusitisha ruti ya Kibaha ilikuwa ni ipi? Na je ni kwa nini mpaka sasa barabara ya mwendo kasi kutoka Kimara kwenda Mbezi na Mloganzila haitumiki wakati ilishakamilika toka mwaka 2021 na hakuna ujenzi wowote unaoendelea? Dkt. Gwajima D
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…