Ghost Worker
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 1,412
- 1,868
Tunashukuru sana kwa serikali ya awamu ya tatu kwa kuanza kufuatilia ubora wa elimu inayotolewa na taasisi zetu za elimu katika harakati za kuitafuta Tanzania tunayoitaka.
Japo hatua zimeshachukuliwa kwa baadhi ya vyuo vinavyotoa elimu ya tiba vilivyokuwa vinatoa elimu chini ya viwango vinavyohitajika, tunaiomna serikali iunde tume maalum kufuatilia hata wale watumishi wa sekta ya afya ambao walihitimu vyuo hivi na wengineo wote waliopo mahospitalini (hasa za umma) wachunguzwe kama wana sifa za kuendelea kutibu binadamu.
Wengi wa hawa wataalamu kutoka vyuo hivi ndio wanatutibu sisi masikini tusio na mahali pa kusemea wala uwezo wa Kwenda India na South Africa. Hali ni mbaya SANA SANA kwenye hospitali za umma. Uzembe, maadili mabovu na Rushwa kwa wataalamu wetu wa afya vinatuua jamani. Malalamiko ni mengi mno sijui tuyapeleke wapi!
Hospitali za umma si vituo vya tiba tena ni vituo vya kuongeza maradhi na wakala wa mtoa roho. Kwa mfano nimekuwa likizo nyumbani Mbinga kwa mwezi mzima, sasa hivi hospitali ya Wilaya ukipata tatizo linalolazimu upasuaji basi ndugu wanaanza kuandaa matanga. Tumeshazika wawili katika kadhia na mazingira ya namna hii (ninaowafahamu), sasa sijui kwa nchi nzima hali ikoje.
Mimi si mtaalamu wa haya mambo ya afya, kwa hiyo siwezi kuuzungumzia tatizo lilivyo kiundani zaidi. Jambo la msingi serikali itafute namna ya kuwasikiliza raia wake katika hili ili itambue ukubwa wa tatizo na kulifanyia kazi hali si nzuri hata kidogo.
Japo hatua zimeshachukuliwa kwa baadhi ya vyuo vinavyotoa elimu ya tiba vilivyokuwa vinatoa elimu chini ya viwango vinavyohitajika, tunaiomna serikali iunde tume maalum kufuatilia hata wale watumishi wa sekta ya afya ambao walihitimu vyuo hivi na wengineo wote waliopo mahospitalini (hasa za umma) wachunguzwe kama wana sifa za kuendelea kutibu binadamu.
Wengi wa hawa wataalamu kutoka vyuo hivi ndio wanatutibu sisi masikini tusio na mahali pa kusemea wala uwezo wa Kwenda India na South Africa. Hali ni mbaya SANA SANA kwenye hospitali za umma. Uzembe, maadili mabovu na Rushwa kwa wataalamu wetu wa afya vinatuua jamani. Malalamiko ni mengi mno sijui tuyapeleke wapi!
Hospitali za umma si vituo vya tiba tena ni vituo vya kuongeza maradhi na wakala wa mtoa roho. Kwa mfano nimekuwa likizo nyumbani Mbinga kwa mwezi mzima, sasa hivi hospitali ya Wilaya ukipata tatizo linalolazimu upasuaji basi ndugu wanaanza kuandaa matanga. Tumeshazika wawili katika kadhia na mazingira ya namna hii (ninaowafahamu), sasa sijui kwa nchi nzima hali ikoje.
Mimi si mtaalamu wa haya mambo ya afya, kwa hiyo siwezi kuuzungumzia tatizo lilivyo kiundani zaidi. Jambo la msingi serikali itafute namna ya kuwasikiliza raia wake katika hili ili itambue ukubwa wa tatizo na kulifanyia kazi hali si nzuri hata kidogo.