Hongo ya maneno imetufikisha hapa

pambe samanini

JF-Expert Member
Oct 27, 2015
368
169
Taifa lenye ngonjera, majigambo, vioja, ulojo, fitina, usaliti, udhalimu, ghirba, ulafi, umangimeza, fikra chakafu, nk kwa wasomi na wananchi wetu wanatuhadaa mashujaa wa siasa na wakombozi wetu, hawa hawafai kwa sababu Vita ikifika mashambulizi yakizidi wanaungana na maadui kutushambulia sisi wenyewe.

Walisema wameachana na siasa kumbe wanataka kuchuma kwanza halafu sasa wako njaa wanataka kurudi na maneno matamu yenye halufu ya manukato kumbe wao ni majini. Eti wameandaa watu wa kuunga mkono kurudi kwao kwa kudai kuwa tumewataka warudi tamthiliya zingine za ajabu na ss wananchi tunashabikia kurudi kwao, kwanini hatuwaulizi walitoka kwa nini na wameona nini tena utamu wetu hadi wanajua midomo yao ilivyokuwa michafu. Hawa watu hawatufai ni wasomi wajinga na sisi ni wanachama masalia tunaonunulika kwa maneno na chenji ndogo.

CCM wakisema chama vya upizani ni taasisi za watu binafsi tunabisha, leo hii imedhihilika wenye taasisi unarudiwa nani wa kupinga? Tusubili kuandamanishwa mabarabarani na kupigwa na polisi maana akili zetu zipo likizo.

Polisi wakitupiga kwa kuandamanishwa na kuaminishwa kuwa tunapigania haki wakati haki na wajibu wetu hatuujui tokea mwanzo tunafanya makosa ya kizembe, kama akili zetu tumeziweka mfukoni ni wakati wa kuzitoa na kutilia zingine tutakuwa mitaji ya watu na taasisi zao. Kwa hili lipumba hafai cuf na taifa lote.

I can say, ' he is traitor and dishonest to all Tanzanian as well as intellectual society.
 
Back
Top Bottom