Betterhalf
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 2,882
- 2,561
Habari za leo wana JF.
Poleni kwa mihangaiko ya kutwa nzima.
Leo tunaelekea kuuaga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka 2018.
Pamoja na majukumu mengine, Azam Media wameandaa kitu muhimu,mahsusi na cha kipekee kwa Watanzania na watazamaji na wafuatiliaji wa vipindi vyao kote ulimwenguni(ambako matangazo yao yanafika).
Kupitia Azam Two, wameendesha program ya pekee tangu majira ya saa 2 asubuhi kupitia studio zao za muda pale Mlimani City.Hongereni sana kwa hili.
Kupitia chaneli hiyo, wamekuwa na mahojiano na makundi mbalimbali wakiwamo wanasiasa,wachumi,wasanii,watu maarufu ambao wamefanyiwa interview ya wazi kupitia timu ya watangazaji mahiri wa Azam Media chini ya Comrade Tido Mhando.
Ama kweli mko vizuri sana na hongereni kwa ubunifu ambao umeonesha namna mnavyojali wateja wenu.
Vipindi vya leo vimekuwa na mtazamo tofauti.Wapo walioona kuwa ni sehemu ya kuwapumzisha wateja wenu kwa kuwapa ladha tofauti kutoka yale waliyoyazoea siku zote.Wengine, wamechukulia tukio hili kama sehemu ya kufanya muhtasari wa yale yote yaliyojiri mwaka 2017 kupitia vipindi vyenu kwenye maeneo ya siasa,uchumi,michezo,starehe na burudani pamoja na nyanja nyingine za kijamii.
Nawashauri wengine muige yale yafanywayo na Azam Media kuanzia na hili.
Hongereni sana Azam Media na staff nzima ya Uhai Production.
Kongole kwenu...!
Poleni kwa mihangaiko ya kutwa nzima.
Leo tunaelekea kuuaga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka 2018.
Pamoja na majukumu mengine, Azam Media wameandaa kitu muhimu,mahsusi na cha kipekee kwa Watanzania na watazamaji na wafuatiliaji wa vipindi vyao kote ulimwenguni(ambako matangazo yao yanafika).
Kupitia Azam Two, wameendesha program ya pekee tangu majira ya saa 2 asubuhi kupitia studio zao za muda pale Mlimani City.Hongereni sana kwa hili.
Kupitia chaneli hiyo, wamekuwa na mahojiano na makundi mbalimbali wakiwamo wanasiasa,wachumi,wasanii,watu maarufu ambao wamefanyiwa interview ya wazi kupitia timu ya watangazaji mahiri wa Azam Media chini ya Comrade Tido Mhando.
Ama kweli mko vizuri sana na hongereni kwa ubunifu ambao umeonesha namna mnavyojali wateja wenu.
Vipindi vya leo vimekuwa na mtazamo tofauti.Wapo walioona kuwa ni sehemu ya kuwapumzisha wateja wenu kwa kuwapa ladha tofauti kutoka yale waliyoyazoea siku zote.Wengine, wamechukulia tukio hili kama sehemu ya kufanya muhtasari wa yale yote yaliyojiri mwaka 2017 kupitia vipindi vyenu kwenye maeneo ya siasa,uchumi,michezo,starehe na burudani pamoja na nyanja nyingine za kijamii.
Nawashauri wengine muige yale yafanywayo na Azam Media kuanzia na hili.
Hongereni sana Azam Media na staff nzima ya Uhai Production.
Kongole kwenu...!