Karimama
Member
- Jul 11, 2015
- 13
- 4
Habari kwamba wasanii maarufu wa Bongo wamemfanyia 'semnd-off' JK na kumualika pia mgombea urais wa CCM, JP Magufuli, inaamsha hisia za huzuni kubwa kwangu na pia kwa wengine wenye mtazamo mpana.
Kwa tathimini ya chini kabisa, juu ya maandalizi ya 'send-off' ile, ni lazima wasanii hao walitumia si chini ya sh. milioni 250 kwa ajili ya maandalizi ya vitu vyote vilivyogharimu shuhuli ile iliyoandaliwa ghafla mno.
Kiasi hicho, ambacho ni kikubwa mno kwa mapato ya wasanii wanaolialia kila siku kwa ukata, kinatokana na gharama za kukodi ukumbi, chakula, mapambo na hata jukwaa achilia mbali ile picha waliyomkabidhi JK.
Wajuaji hawaamini kuwa gharama zile zilitolewa na wasanii wenyewe, kwa sababu kumshaanza kuwepo malalamiko toka baadhi ya wasanii kutolipwa fedha walizoahidiwa na waandaaji halisi wa shughuli ile. Fedha za malipo ya kutumbuiza.
Lakini tukubaliane kuwa hafla ile iliandaliwa na wasanii kwa fedha za mifukoni mwao kama wanavytoaka tuaamini. Ila wakati tukiamini hayo, tujiulize pia hivi kufanya seherehe ya mamia ya mamilioni ya fedha kama ile kuna tija mno kuliko maisha ya wasanii wenzao?
Nakumbuka:
Mikaka michache iliyopita, msanii maarufu wa maigizo, mzee Small Ngamba alifariki dunia kutokana na maradhi ya kupooza huku akilalamika kuwa hana pesa za matibabu.
Kabla ya hapo, Sajuki, msanii mwingine wa Bongo Movie, naye alifariki kwa ugonjwa wa kansa ya damu baada ya kukosa matibabu kwa wakati. Naye ilikuwa hiyo, alikosa pesa za matibabu mpaka pale Zitto Kabwe alipopitisha kwa mbinde michango kwa ajili ya matibabu yake.
Inakumbukwa pia mzee Kipara na mzee Pwagu, wasanii maarufu zaidi wa nchi hii, nao pia walikufa vifo vibaya vya maradhi kwa kukosa fedha za matibabu kwa maradhi ambayo pengine yasingesababisha umauti wao iwapo wangepeta fedha za matibabu.
Wasanii hao wote, Mungu awaweke mahali pema, mara kadhaa walizungumzia hali ya maradhi yao na kuomba msaada wa fedha kwa wasanii wenzao lakini hawakupata msaada uliostahiki.
Ndorooobo nyie!
Kwa mazingira hayo, iwapo kweli wasanii maarufu wa CCM walichangia shughuli ile, basi watakuwa 'mandorooobo' wasiojielewa wala kutafakari mustakabali wa 'maisha yao ya kuigiza' ambayo pindi yanapokuja matatizo ya kiasili kama maradhi huanza kutapata.
Lakini kwa vile inajulikana fedha zile si zao, ni vyema wafahamu kuwa walichofanya usiku ule kimewanufaisha zaidi wale waliopewa tenda ya kuwakusanya wao na kisha kuwatumia kama mambumbumbu wanaoweza kutumiwa kukampeni kwa ujira wa ubwabwa na juisi ya usiku mmoja.
Kwa tathimini ya chini kabisa, juu ya maandalizi ya 'send-off' ile, ni lazima wasanii hao walitumia si chini ya sh. milioni 250 kwa ajili ya maandalizi ya vitu vyote vilivyogharimu shuhuli ile iliyoandaliwa ghafla mno.
Kiasi hicho, ambacho ni kikubwa mno kwa mapato ya wasanii wanaolialia kila siku kwa ukata, kinatokana na gharama za kukodi ukumbi, chakula, mapambo na hata jukwaa achilia mbali ile picha waliyomkabidhi JK.
Wajuaji hawaamini kuwa gharama zile zilitolewa na wasanii wenyewe, kwa sababu kumshaanza kuwepo malalamiko toka baadhi ya wasanii kutolipwa fedha walizoahidiwa na waandaaji halisi wa shughuli ile. Fedha za malipo ya kutumbuiza.
Lakini tukubaliane kuwa hafla ile iliandaliwa na wasanii kwa fedha za mifukoni mwao kama wanavytoaka tuaamini. Ila wakati tukiamini hayo, tujiulize pia hivi kufanya seherehe ya mamia ya mamilioni ya fedha kama ile kuna tija mno kuliko maisha ya wasanii wenzao?
Nakumbuka:
Mikaka michache iliyopita, msanii maarufu wa maigizo, mzee Small Ngamba alifariki dunia kutokana na maradhi ya kupooza huku akilalamika kuwa hana pesa za matibabu.
Kabla ya hapo, Sajuki, msanii mwingine wa Bongo Movie, naye alifariki kwa ugonjwa wa kansa ya damu baada ya kukosa matibabu kwa wakati. Naye ilikuwa hiyo, alikosa pesa za matibabu mpaka pale Zitto Kabwe alipopitisha kwa mbinde michango kwa ajili ya matibabu yake.
Inakumbukwa pia mzee Kipara na mzee Pwagu, wasanii maarufu zaidi wa nchi hii, nao pia walikufa vifo vibaya vya maradhi kwa kukosa fedha za matibabu kwa maradhi ambayo pengine yasingesababisha umauti wao iwapo wangepeta fedha za matibabu.
Wasanii hao wote, Mungu awaweke mahali pema, mara kadhaa walizungumzia hali ya maradhi yao na kuomba msaada wa fedha kwa wasanii wenzao lakini hawakupata msaada uliostahiki.
Ndorooobo nyie!
Kwa mazingira hayo, iwapo kweli wasanii maarufu wa CCM walichangia shughuli ile, basi watakuwa 'mandorooobo' wasiojielewa wala kutafakari mustakabali wa 'maisha yao ya kuigiza' ambayo pindi yanapokuja matatizo ya kiasili kama maradhi huanza kutapata.
Lakini kwa vile inajulikana fedha zile si zao, ni vyema wafahamu kuwa walichofanya usiku ule kimewanufaisha zaidi wale waliopewa tenda ya kuwakusanya wao na kisha kuwatumia kama mambumbumbu wanaoweza kutumiwa kukampeni kwa ujira wa ubwabwa na juisi ya usiku mmoja.