Hongera Samia kwa dira ya Taifa ya maendeleo 2050

Hongera Samia kwa dira ya Taifa ya maendeleo 2050

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
464
Reaction score
687
Tunasoma katika Mithali 29:18 "Pasipo maono, watu huacha kujizuia" Huu ni ukweli usiopingika linapokuja swala la maendeleo ya mtu mmoja mmoja au taifa kwa ujumla.

Eneo moja lililotughalimu kama nchi ni kukosekana kwa mwendelezo wa mipango yetu ya maendeleo kutoka awamu moja kwenda awamu nyingine. Chukulia mfano wa mradi wa Dege Kigamboni. Mradi ulitekelezwa kwa kasi katika awamu ya nne, ilipofika awamu ya tano mradi ukasitishwa. Fedha nyingi zilizowekezwa pale zimepotea, labda itokee siku moja aje rais mwingine kunusuru.

Kuwepo kwa dira ya taifa ya maendeleo kutatoa mwongozo wa vipaumbele vya shughuli za Serikali jambo ambalo litatuletea muunganiko wa vipaumbele vya awamu zinazokuja za serikali zetu. Hili ni jambo zuri na kwakweli Rais Samia na timu yake iliyotekeleza mpango huu wanastahili pongezi. Hongera sana Rais.
 
Tatizo kubwa ni kuwa na katiba ambayo inapelekea likichwa limoja kuongoza kila kitu

Ukitaka muendelezo wa maendeleo inatakiwa rais apunguziwe madaraka,hvyo tunahitaji katiba mpya bila hvyo zitabak kuwa porojo
 
Back
Top Bottom