Hongera KKKT Mabibo External

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2008
Posts
4,773
Reaction score
2,383

Nilihudhuria ufunguzi wa Kanisa la KKKT Mabibo External jumapili hii.
Kwa kweli wamejitahidi sana na kanisa linapendeza.
Askofu Dr Alex Malasusa ali endesha misa na kuliweka kanisa wakfu.
Kati ya wachungaji waliohudhuria ni pamoja na Mchungaji Gehaz Malasusa, babayake na Askofu Malasusa.

Vile vile nilifurahishwa na salamu za Mbunge wa Ubungo John Mnyika aliyetoa salamku kutoka hapa:
Zaburi 15

1 Bwana, ni nani atakayekaa Katika hema yako? Ni nani atakayefanya maskani yake Katika kilima chako kitakatifu?
2 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake,
3 Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala hakumtenda mwenziwe mabaya, Wala hakumsengenya jirani yake.
4 Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa, Bali huwaheshimu wamchao Bwana Ingawa ameapa kwa hasara yake, Hayabadili maneno yake.
5 Hakutoa fedha yake apate kula riba, Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia. Mtu atendaye mambo hayo Hataondoshwa milele.

Nakufagilia Bw Mnyika maana hata Neno limekaa moyoni.
 
Mfumo kristo ha ha ha ha ha.
 
Nakufagilia Bw Mnyika maana hata Neno limekaa moyoni.

Hilo jengo mbona lina giza hivyo Limejengwa kwa kutumia ujenzi wa gothic archtechture unaotumika maeneo ya ulaya yenye baridi kali na kunakoweka madirisha madogo kuhifadhi joto ndani.

Tatizo la ujenzi hapo ni kwanza hamna hewa ya kutosha na madirisha ni madogo ukilinganisha na idadi ya watu inalobidi iwameze.mwanga wa kutoka nje ni mdogo ni bili za taa za tanesco kwenda mbele.Kwa kulitizama tu ramani hizo ni zile za ku-paste and copy za ulaya ambazo mjenzi hazingatii hali ya hewa ya jengo lilipo.Humo ndani kama hakuna umeme kila muumini itapidi aende na kitambaa cha kufuta jasho hasa kama feni hazifanyi kazi na kutakuwa na giza sana.Anyway something is better than nothing hongereni.
 
Jamaa wale wasije wakalichoma moto
 
Asante kwa observation mkuu.
Lakini picha hiyo ni manjonjo ya mpiga picha, na jengo limekaa vizuri sana.
Unachoona ni madhabahu na sijaweka side elevations.
Pembeni mwa jengo kuna kuta zilizo wazi toka juu hadi chini mfano wa lovre iliyosimama.
ndani ya kanisa hakuna joto kabisa, na kuthibisha hilo mimi nilivaa suti-na ni mwesi huu wa Octoba.

Giza ulilliona ni effects za camera ,pamoja na ukweli kuwa Architect alifanya kazi yake vizuri sana kutumia mwanga wa nje.
Madhabahu iko illluminatrd naturally, kitu ambacho kinaleta hisia ya mahali patakatifu.

Mkuu fika hapo, na sala yako nawe utaamini.
 
Ruzuku za serikali zinajenga hayo mahekalu yenu! We ngoja apatikane kiongozi mkorofi! Mtapiga haleluyah mpaka asubuhi lkn hampewi kitu.
 
Mungu akusamehe mana hujui usemalo

Mungu unaemuongelea hapa yupi?
Ni yule mnaesema alipigwa mpaka akalia halafu akauawa! Au kuna mwingine!
Manake huyo aliye uwawa hakuweza kujionea huruma mwenyewe! Ataweza kunionea huruma mimi?
 
Mungu unaemuongelea hapa yupi?
Ni yule mnaesema alipigwa mpaka akalia halafu akauawa! Au kuna mwingine!
Manake huyo aliye uwawa hakuweza kujionea huruma mwenyewe! Ataweza kunionea huruma mimi?
Naona shetwain anakutafuta, kujiokoa juhudi yako.
 
Naona shetwain anakutafuta, kujiokoa juhudi yako.

Teh teh teh teh!
Shetwain ndio nani? Huyu lzm atakuwa myahudi flani! Nyie wagalatia mmeanza kuota ndoto miaka mingi mno! Huu ni wakati wa kuamka! Acheni kijidanganya kuwa mungu ni mtu au alijifanya mtu halafu akubali kujiua ili abebe madhambi ya wale wabakaji na wizi na waliberali na wachafu woote!
Mkifa na imani hii mtaingia motoni woote!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…