Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,773
- 2,383
Nilihudhuria ufunguzi wa Kanisa la KKKT Mabibo External jumapili hii.
Kwa kweli wamejitahidi sana na kanisa linapendeza.
Askofu Dr Alex Malasusa ali endesha misa na kuliweka kanisa wakfu.
Kati ya wachungaji waliohudhuria ni pamoja na Mchungaji Gehaz Malasusa, babayake na Askofu Malasusa.
Vile vile nilifurahishwa na salamu za Mbunge wa Ubungo John Mnyika aliyetoa salamku kutoka hapa:
Zaburi 15
1 Bwana, ni nani atakayekaa Katika hema yako? Ni nani atakayefanya maskani yake Katika kilima chako kitakatifu?
2 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake,
3 Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala hakumtenda mwenziwe mabaya, Wala hakumsengenya jirani yake.
4 Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa, Bali huwaheshimu wamchao Bwana Ingawa ameapa kwa hasara yake, Hayabadili maneno yake.
5 Hakutoa fedha yake apate kula riba, Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia. Mtu atendaye mambo hayo Hataondoshwa milele.
Nakufagilia Bw Mnyika maana hata Neno limekaa moyoni.