rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 18,070
- 25,745
Milan waachane na mambo ya historia timu yetu ilianza kurudi kwenye form lakini kitendo cha kuwauza Thiago silva na kushindwa kutafuta replacement kitaendelea kuwagharimu tumesajili wachezaji wengi lakini hawana ubora mmiliki wetu anatumbua pesa nyingi kwa vimada badala ya kuwekeza kwenye timu wanasingizia sheria ya uefa wakati psg na chelsea wamefanya kinyume uongozi umejisahau na kuridhika na mafanikio ya kipindi cha nyuma wachezaji wengi waliopo hawastahili milan ilikuwa timu bora idara zote lakini angalia wachezaji kama abate,antonini wengi walitakiwa wawe pale kujifunza kwa wachezaji mahiri ili watakapopata nafasi waonyeshe umahiri wao.
milan ili offload wachezaji wengi kwa namna nyingine iliokoa pesa nyingi za mishahara kwani wengi walikuwa wachezaji wa kiwango cha juu hatukuhitaji kusajili wachezaji wengi wachache wenye ubora badala ya kuwa na wachezaji wengi wasiokuwa na ubora wa kuchezea Milan na pia tunahitaji kocha wa kiwango cha juu kocha tuliyenaye haimudu hii timu tusimlinganishe na arrigo sachi
milan zilipendwa, hata kufunga goli haiwezi eti sasa wanataka kumpa mviziaji pipo inzaghi timu!
Report: AC Milan's Massimiliano Allegri rows with Filippo Inzaghi - ESPNFC
Nitafurahi siku nikipata ripoti kuwa Allegri katimuliwa.
Jamaa si wa hadhi ya Milan.
niliyasema haya kabla na nitayasema daima, na ndio maana seniors woote wako pembeni wanamuangalia tu.
acha visingizio, nasikia udinese wamewapiga bao leo - ni kweli?
Ndugu yangu ni kweli na niko natembelea web na blog za Soka...nahisi ntakutana na ile habari nayoisubiri ya Allegri kutimuliwa.
wakati milan mnaendeleza siasa mwenzenu ibracadabra anacheka na nyavu huko psg!
Pole kaka naona inakula kwako au mwaka wa shetani nini kwako huu?Ndugu yangu ni kweli na niko natembelea web na blog za Soka...nahisi ntakutana na ile habari nayoisubiri ya Allegri kutimuliwa.
Pole kaka naona inakula kwako au mwaka wa shetani nini kwako huu?
[ok...Naomba uwaorodheshe hapa hao wasiokuwa na hadhi ya kuchezea Milan...Asante kwa mawazo yako pia.]
Kama umefatilia milan kwa musa mrefu utakumbuka Milan ni timu iliyokuwa inaongoza duniani kwa kuwa na beki bora Franco Baresi aliamua kujiuzulu baada ya kuridhika Desaily anaweza kuziba pengo lake,kuna kipindi wakina Robert Ayala pamoja na ubora waliokuwa nao walipoondoka hawakuacha pengo lolote sasa beki wa kiwango cha dunia tuliyekuwa naye ni Thiago Silva ambaye tumemuuza waliobaki ni kiwango cha kawaida hakuna hata mmoja unayeweza kumweka katika first eleven ua ulaya au dunia kwa upande wa viungo tumewahi kutoa viungo bora kabisa duniani lakini baada ya kuwauza Pirlo,Kaka tumeshindwa kuziba mapengo yao Ambrosin ni mzuri kwa kuzuia lakini alitakiwa apate watu wenye uwezo kumsaidia pamoja na uzuri wa KPB,Norcelino,De jong na Montolvo bado wana safari ndefu kufikia level ya kina boban,rui costa,Albetin,Frank Ricard kuwataja wachache wachezaji kama Antonini,Abate hawana hadhi ya kuchezea milan tunaoijua kuna kipindi tulikuwa na wachezaji kama Rivaldo,Tommason ambao walikuwa benchi na walipoingia unaona mabadiliko kama unakumbuka mechi ya Ajax na Milan San siro au Gilardino kama unakumbuka mechi ya man u na Milan San siro ya Man u kulala 3 kwa bila lakinisasa hivi hata watokea benchi hawana mabadiliko yoyote
Daniel Bonera ni mzuri kama akicheza beki namba 2 lakini siku zote akiwekwa beki wa kati ama atasababisha penati au goli
allegri a.k.a aleji
Haya kaka,ila kesho dalili inaonyesha ushindi upo kwako!wakati Derby Della Madoninna ikiwa ni kesho klabu ya AC Milan tukiwa nyumbani huku tukiwa na rekodi mbovu ya kuanza Ligi vibaya takriban miongo kadhaa inajitupa katika uwanja wake wa Nyumbani kukwaana na Inter Milan ambao nao hawako sawa saana kufuatia matokeo kadhaa ya ligi ambayo si mazuri.
katika tifuatifua hili ni wazi kuwa timu itakayoshinda basi itakuwa imeamsha Morali wa ushindi.
Nikiwa kama mpenzi wa Soka la Taifa la Italia natabiri mechi hii kuisha kwa AC Milan kuibuka na ushindi wa jumla ya Goli 3-1 huku wachezaji si chini ya wawili toka timu zote wakilambwa kadi nyekundu.
NB:
Ni kawaida kwa mechi hii mpira kusimama mara kwa mara kutokana na ubabe na vurumai kwa timu wachezaji na hata washabiki wa timu zoote mbili.
Upande wa jukwaa la hadhi Milan atakuwepo Mmiliki mwenye mafanikio katika Soka hapa ulimwenguni Silvio Berlusconi akiambatana na swahiba wake wa miaka miingi sana hapa namzungumzia Adriano Galiani.
Wakati kwa upande wa Inter atakuwepo Milionea wa visima vya mafuta hapa namzungumzia Masimo Moratti.
Forza Milan
Haya kaka,ila kesho dalili inaonyesha ushindi upo kwako!
bianconeri kibibi cha turin wazee wa ndefu,bingwa mtetezi wa serie A na anayetarajiwa kuwa bingwa mpya wa klabu za ulaya!Juventus wanataka kumsajili Gang chomba kuwa mshabiki wao baada ya chama lake kuwa goma la mtaa kila msela anajipigia!