Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
Tunafahamu kuwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Wakili Msomi mwenzangu na Rais wangu wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika Tundu A.M. Lissu ameshambuliwa kwa risasi katik viunga vya nyumbani kwake huko Area D,Dodoma. Kwasasa, Lissu anapokea huduma za kitabibu huko Nairobi, Kenya.
Kwa wingi wetu, tunaendelea Lissu kuomba ili arejee kwenye afya yake njema na kurejea kwenye majukumu yake ya Ubunge, uongozi wa TLS, uongozi wa CHADEMA na Uwakili. Tunafahamu sasa kuwa Jeshi la Polisi tayariu limeanza uchunguzi kuwabaini wahusika wa shambulio la Lissu ili waweze kufikishwa kwenye mikono ya sheria.
Kunaibuka kwa kasi malumbano yasiyo na tija (kwa maoni yangu) juu ya nani hasa analipia au amelipia matibabu ya Lissu kule Nairobi kuanzia kusafirishwa kwake na hata sasa. Sioni mashiko ya hoja hii kwakuwa suala lililopo ni Lissu kupata matibabu. Mchangiaji yeyote, awe wa chama chake au chama kingine au asiye na chama wa ndani na nje ya Tanzania, aweza kuchangia matibabu ya Lissu na kusiwe na hoja.
Kwa hali ilipofikia, mambo ya uvyama yanazidiwa nguvu na mambo ya ubinaadamu na uhai wa mtu kwa ujumla. Hoja iliyo mbele yetu, na mikononi mwa Jeshi la Polisi, ni akina nani walihusika na shambulio la Lissu na walisukumwa na jambo gani hasa. Majibu ya hoja hiyo yatatufunza na kutuimaisha kimaisha, kisiasa, kiusalama na kiutawala.
Pray for Hon. Tundu A.M. Lissu to quickly recover!
Kwa wingi wetu, tunaendelea Lissu kuomba ili arejee kwenye afya yake njema na kurejea kwenye majukumu yake ya Ubunge, uongozi wa TLS, uongozi wa CHADEMA na Uwakili. Tunafahamu sasa kuwa Jeshi la Polisi tayariu limeanza uchunguzi kuwabaini wahusika wa shambulio la Lissu ili waweze kufikishwa kwenye mikono ya sheria.
Kunaibuka kwa kasi malumbano yasiyo na tija (kwa maoni yangu) juu ya nani hasa analipia au amelipia matibabu ya Lissu kule Nairobi kuanzia kusafirishwa kwake na hata sasa. Sioni mashiko ya hoja hii kwakuwa suala lililopo ni Lissu kupata matibabu. Mchangiaji yeyote, awe wa chama chake au chama kingine au asiye na chama wa ndani na nje ya Tanzania, aweza kuchangia matibabu ya Lissu na kusiwe na hoja.
Kwa hali ilipofikia, mambo ya uvyama yanazidiwa nguvu na mambo ya ubinaadamu na uhai wa mtu kwa ujumla. Hoja iliyo mbele yetu, na mikononi mwa Jeshi la Polisi, ni akina nani walihusika na shambulio la Lissu na walisukumwa na jambo gani hasa. Majibu ya hoja hiyo yatatufunza na kutuimaisha kimaisha, kisiasa, kiusalama na kiutawala.
Pray for Hon. Tundu A.M. Lissu to quickly recover!