PakiJinja
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 7,687
- 15,841
Kwa mbwembwe za yule babu wa Uganda, hatukutarajia aingie mitini na kutokomea.
Kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki, anajulikana kama "SHUJAA WA VITA ZA KISHOGA", na amefanikiwa kujizolea umaarufu na makiki kila pande [Maujiko].
Hivi majuzi alikabidhiwa kusaini sheria tata ya kishoga, huku wapambe na wafuasi wake wakimjaza na kumpampu upepo ndani ya kichwa chake cha kidikteta.
Ghafla akatokomea shimonii baada ya mabeberu kumpiga mkwara kiduchu tu. Akatimka na hajaonekana hadharani wiki ya tatu sasa.
Tunajiuliza kama kale kababu kameshatepeta na kulegezwa na mabeberu ya Washington? Na ataambia nini wafuasi wake wanaompampu kichwa chake cha kidikteta?
Kama hivyo ndivyo, je, sisi watanganyika tuna maoni gani?
HOJA JADILIFU.