Smart-brain
Senior Member
- Mar 17, 2014
- 101
- 62
Habari wakuu;
Nikizungumzia upande wa Tanganyika, tumebarikiwa kuwa na katiba, sheria, kanuni, taratibu, pamoja na miongozo (licha ya mapungufu) mbalimbali ili kutufanya tuishi kwa utaratibu na amani.
Lakini kwa upande mwingine hatuoni sheria hizi zikiwashughulikia wahusika kikamilifu au kupendelea kundi la watu kwa manufaa yao.
Mh. Dr Ndalichako(W.Elimu) amefanikisha kupeleka Mahakamani na kushtakiwa kwa Walimu walioonekana kukiuka maadili ya kazi, eg Mwl. aliyempiga Mwanafunzi kwa fimbo na kupelekea kufariki kwake. Hili alilofanya Mh. Waziri ni jema kuhakikisha Walimu wanakumbuka mipaka yao ya namna ya kutoa adhabu.
Wizara ya Mambo ya Ndani, nasikitika imefeli kabisa kuwashughulikia wavunjaji wa sheria kwa kuwapeleka Mahakamani (au kwa taratibu zingine) ili kuweka utendaji uliotukuka kwa Watumishi hawa wa Umma. Hapa ninalenga zaidi JESHI LA POLISI. Hili jeshi linautaratibu wake wa kushughulikia wavunjaji wa kanuni za kijeshi, haziendi kinyume na taratibu, huwa hata anayeshughulikiwa nazo, kweli hujiona ni mkosaji hasa.
Lakini, tunaona baadhi ya Polisi hawa(sijui ni kwa maagizo au la) jinsi wanavyokiuka Haki za Binadamu hata kupelekea kunakosemekana "Kuua Raia Wasio na Hatia au Kujeruhi kwa RISASI za Moto nk", (ref: Mbeya, Tabora, Dar Es Salaam). Kinachotia tashwishwi ni pale "tukio linapoonekana kutendwa na wao" lakini tunaona mambo yakifunikwa tu na kuacha MASWALI MENGI KULIKO MAJIBU. Kama Mh. Lugola na Mh. Insp. wa Jeshi la Polisi wangefuata "nyayo" za Mh. Ndalichako , jeshi letu lisingepakwa matope! Mh. Lugola, katika hili VAA MASK!!!!
"Mh. Lugola ebu pia kata ngebe za mgambo wanaojiona ni Mafarao sasa, bila hivyo ....!!!"
Nikizungumzia upande wa Tanganyika, tumebarikiwa kuwa na katiba, sheria, kanuni, taratibu, pamoja na miongozo (licha ya mapungufu) mbalimbali ili kutufanya tuishi kwa utaratibu na amani.
Lakini kwa upande mwingine hatuoni sheria hizi zikiwashughulikia wahusika kikamilifu au kupendelea kundi la watu kwa manufaa yao.
Mh. Dr Ndalichako(W.Elimu) amefanikisha kupeleka Mahakamani na kushtakiwa kwa Walimu walioonekana kukiuka maadili ya kazi, eg Mwl. aliyempiga Mwanafunzi kwa fimbo na kupelekea kufariki kwake. Hili alilofanya Mh. Waziri ni jema kuhakikisha Walimu wanakumbuka mipaka yao ya namna ya kutoa adhabu.
Wizara ya Mambo ya Ndani, nasikitika imefeli kabisa kuwashughulikia wavunjaji wa sheria kwa kuwapeleka Mahakamani (au kwa taratibu zingine) ili kuweka utendaji uliotukuka kwa Watumishi hawa wa Umma. Hapa ninalenga zaidi JESHI LA POLISI. Hili jeshi linautaratibu wake wa kushughulikia wavunjaji wa kanuni za kijeshi, haziendi kinyume na taratibu, huwa hata anayeshughulikiwa nazo, kweli hujiona ni mkosaji hasa.
Lakini, tunaona baadhi ya Polisi hawa(sijui ni kwa maagizo au la) jinsi wanavyokiuka Haki za Binadamu hata kupelekea kunakosemekana "Kuua Raia Wasio na Hatia au Kujeruhi kwa RISASI za Moto nk", (ref: Mbeya, Tabora, Dar Es Salaam). Kinachotia tashwishwi ni pale "tukio linapoonekana kutendwa na wao" lakini tunaona mambo yakifunikwa tu na kuacha MASWALI MENGI KULIKO MAJIBU. Kama Mh. Lugola na Mh. Insp. wa Jeshi la Polisi wangefuata "nyayo" za Mh. Ndalichako , jeshi letu lisingepakwa matope! Mh. Lugola, katika hili VAA MASK!!!!
"Mh. Lugola ebu pia kata ngebe za mgambo wanaojiona ni Mafarao sasa, bila hivyo ....!!!"