Rose Mayemba
JF-Expert Member
- May 7, 2012
- 721
- 1,017
Tazama,
Wote wamepigwa upofu, hakuna anayeona mbele,kina mmoja anakaza mwendo kuelekea kusikojulikana, si wakubwa wala wadogo wote wanahangaika.
Hawakuwahi kufikiri kama haya yoye yangetokea, walijisahau, wakafanya mambo mengi kwa hila wakiamini hakuna anayeona, walitumia neema iliyoshushwa na Mwenyezi Mungu kwa nufaa ya matumbo yao, wala hawakuwahi kuwakumbuka waliotembelea tumbo kutafuta riziki zao..
Mungu asingekaa kimya, pengine alihuzunishwa sana na mwenendo mbaya uliokithiri wa mabwana hawa, akakasirika, amemwamsha kila aliyekuwa katika usingizi mkali wenye mateso yasiyo simulika ili kuushuhudia uozo wao, naye aliyetoka usingizini amefurwa na hasira, anauchungu wa kuishi taabuni muda mrefu huku hazina yake wakigawana wachache, sasa amedhamiria kufanya mapinduzi...
masikini...
Hakuna hata mmoja kati yao anayeliona anguko lao, wengi wanatabiri tu, na wengine kujifariji kama bado neema i upande wao. Mambo yanaharibika kila kunavyokucha lakini wapi, MUNGU amekwisha kuwaondolea ufahamu wao, ili wasije wakafunguka , kisha wakaongoka...
HAKUNA MSHAHARA UNAOZIDI MATENDO, MALIPO HUFANYIKA KWA KADRI YA JUHUDI YA KAZI ULIYOPEWA.
Wote wamepigwa upofu, hakuna anayeona mbele,kina mmoja anakaza mwendo kuelekea kusikojulikana, si wakubwa wala wadogo wote wanahangaika.
Hawakuwahi kufikiri kama haya yoye yangetokea, walijisahau, wakafanya mambo mengi kwa hila wakiamini hakuna anayeona, walitumia neema iliyoshushwa na Mwenyezi Mungu kwa nufaa ya matumbo yao, wala hawakuwahi kuwakumbuka waliotembelea tumbo kutafuta riziki zao..
Mungu asingekaa kimya, pengine alihuzunishwa sana na mwenendo mbaya uliokithiri wa mabwana hawa, akakasirika, amemwamsha kila aliyekuwa katika usingizi mkali wenye mateso yasiyo simulika ili kuushuhudia uozo wao, naye aliyetoka usingizini amefurwa na hasira, anauchungu wa kuishi taabuni muda mrefu huku hazina yake wakigawana wachache, sasa amedhamiria kufanya mapinduzi...
masikini...
Hakuna hata mmoja kati yao anayeliona anguko lao, wengi wanatabiri tu, na wengine kujifariji kama bado neema i upande wao. Mambo yanaharibika kila kunavyokucha lakini wapi, MUNGU amekwisha kuwaondolea ufahamu wao, ili wasije wakafunguka , kisha wakaongoka...
HAKUNA MSHAHARA UNAOZIDI MATENDO, MALIPO HUFANYIKA KWA KADRI YA JUHUDI YA KAZI ULIYOPEWA.