HIzi chuki za wana CCM kwa Lissu zinasababishwa na nini?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,301
33,920
Baada ya kukutana na hii Posti na nyingine nyingi hapa JF, nimejiuliza ni kitu gani hasa Lissu alichowafanyia wana CCM na baadhi ya marafiki zao kufikia kumchukia kiasi hiki?

Hivi kwa akili zako unaweza ukaombea mpuuzi mmoja uache Rais wa Taifa zima!!
Huyu mwenye hili bandiko alikuwa anajibu hoja ya habari iliyoandikwa kwenye Mwanahalisi na Ansbert Ngurumo kwamba kati ya Lissu na Rais Magufuli nani anastahili kuombewa.

Siku ya kwanza Lissu aliposhambuliwa tuliona "huruma" za wana CCM kwa Lissu, lakini kadri tunavyoambiwa kwamba hali ya Afya ya Lissu inazidi kuimarika ndipo tunaona zile chuki na hasira za wana CCM na marafiki zao dhidi ya Lissu zinarudi kwa kasi ya ajabu.

Humu JF sasa kumesheheni mabandiko yanayoandika wazi wazi kwamba Lissu kajitakia kushambuliwa na hakuna faida yoyote ile atakayoipata zaidi ya familia yake kupata shida. Mengine yanaashiria kwamba Lissu alikuwa "kibaraka" wa wazungu hivyo kwa nini leo hawamsaidii badala yake CHADEMA wanataka serikali ndiyo ibebe gharama za kumtibia wakati Lissu alikuwa anaipinga!

Kila ukisoma mabandiko ya wana CCM hata ya yule kijana mzee W. J. Malecela al maarfu Le mutuz unapata picha kwamba kama Lissu angeuawa siku ile kuna watu wangeweka na sherehe majumbani mwao kusheherekea kifo cha Lissu.

Lakini swali la kujiuliza ni kwa nini CCM wana hasira na chuki kwa Tundu Lissu kwa kiwango hiki. Ni nini hasa alichowafanya hadi wanamchukia kiasi cha kuona mateso anayokabiliana nayo hivi sasa si kitu?
 
Mara nyingi wanaojifanya Kulia sana Msibani na kuomboleza ndio Wachawi Wenyewe!, na kazi Yao kubwa ni kujifanya kuzuga Watu kwa kuuliza Watu hisia zao kuhusu Nani ni Mbaya wa Marehemu

Bavicha wanajifanya wameguswa na Mkasa wa Lissu kuliko Familia yake
 
Miaka imeenda na hawana pa kutokea,ahadi walizotoa zinazidi kuota mbawa lazima watafute mkwamishaji kwa kuchochea chuki kwa kila anaekosoa njia wanazopita wanambandika uchawi kwa kutumia raia wajinga wasio wajibika kufikiri.
Dereva wewe kondakta wako iweje abiria alaumiwe kwa kukosekana mapato?
 
Kuna watu wanafikiri kumchukia mtu anayekuzidi uwezo ni sawa na haki!! Lissu ana uwezo wa kisheria kuzidi wanasheria wengi wa serikali na ccm kwa ujumla. Wanadhani kwa kumchukia watamfikia!! Hii ni baada ya kuwa anawagaragaza ktk kesi nyingi za uchaguzi na za kawaida

Pili Lissu ni mkweli na kwake Nyeupe ni nyeupe, na hicho ni kitu serikali na ccm wasingependa wananchi kuelezwa ukweli wowote e.g. Mikataba mibovu , Bomberdia kukamatwa kwa sababu gani?! ,

Tatu ni kuwa Lissu ni mbunge, ambayo amewa ovashado wabunge wengi, hasa wa ccm na mawaziri wao, na mfano ni mchango wake dakika 30 kabla hajashambuliwa. Kwa ujumla ni mahiri na hilo kwao ni chukizo.
 
Hata yeye huyo Lissu ana chuki na wana CCM tena chuki ya wazi wazi ambayo hata kwa kujaribu ameshindwa kuizuia chuki yake. Kwa hiyo usiwashangae wana CCM kumchukia Lissu, ndiyo maisha yalivyo, tulia vivo hivyo.
Unamchukia anaekuonyesha udhaifu wako?! Aahh hii balaa, bila Lissu ungejuwa kama Bomberdia inashikiliwa kwa sababu ya maamuzi yetu mabovu ?! nk WaTz tumerogwa si bure, nadhani hizi shule za kata zimeleta balaa
 
Mimi ni ccm ila simchukii Lissu japo huwa simuelewi Kama ni kiongozi au ni mnyapara huko chadema. Bado sijafahan dhamana aliyonayo ndani ya hicho chama.

Hii sintofaham yangu kwa lissu ni kutokana na Hekima Na busara ndogo aliyonayo kwa wakubwa Na wadogo wanaomzunguka katika Jamii yetu.

Msikilize lissu anapozungumza iwe bungeni, mahakamani, mkutanoni au hata nje ya hapo, utapata picha halisi kuwa lissu amejaliwa akili na maarifa lakini alinyimwa busara Na Hekima.

Kwa sifa hizi yatosha basi kuwa nyapara Na si kiongozi kwa viwango vyovyote vile.

Hakuna kiongozi asiye Na Hekima wala busara. Ukimkuta wa hivyo hata awe Na akili nyingi Na maarifa, huyo ni mnyapara.

Ni Hekima Na busara gani aliyoitumia lissu ya kuita waandishi wa habari Mara 2 kwa nyakati tofauti na kuonyesha dharau ya hali ya juu kwa tume 2 za raisi kuhusu uchunguzi wa makinikia ya dhahabu?

Zile tume zilikuwa za wataalamu bobezi baadhi wakiwa professors kwenye eneo husika la Madini.

Nilishangaa Sana Na akaiita report yao eti rubbish...(takataka).

Frankly speaking that's high Level of stupidity I have never seen in my life.
 
Hii nchi la saba wengi...hao uliowataja hawahusiani na uzi huu
Hii nchi la saba wengi...hao uliowataja hawahusiani na uzi huu
Rafiki, heri ya darasa la 7 kuliko NGUMBARU au MMEMKWA...!
Inaonekana unavamia mitandao na hujuii unataka kuchangia nini!!!!Lissu amepigwa risasi kisingizio ni kuwa anatetea wezi wa madini...........Lakini niliowataja hapa ni wana CCM waliosainisha mikataba ya KIFISADI....!!!!!!!So nani msalitii kati ya TL na Wana CCM...??????!!!
 
Mimi ni ccm ila simchukii Lissu japo huwa simuelewi Kama ni kiongozi au ni mnyapara huko chadema. Bado sijafahan dhamana aliyonayo ndani ya hicho chama.

Hii sintofaham yangu kwa lissu ni kutokana na Hekima Na busara ndogo aliyonayo kwa wakubwa Na wadogo wanaomzunguka katika Jamii yetu.

Msikilize lissu anapozungumza iwe bungeni, mahakamani, mkutanoni au hata nje ya hapo, utapata picha halisi kuwa lissu amejaliwa akili na maarifa lakini alinyimwa busara Na Hekima.

Kwa sifa hizi yatosha basi kuwa nyapara Na si kiongozi kwa viwango vyovyote vile.

Hakuna kiongozi asiye Na Hekima wala busara. Ukimkuta wa hivyo hata awe Na akili nyingi Na maarifa, huyo ni mnyapara.

Ni Hekima Na busara gani aliyoitumia lissu ya kuita waandishi wa habari Mara 2 kwa nyakati tofauti na kuonyesha dharau ya hali ya juu kwa tume 2 za raisi kuhusu uchunguzi wa makinikia ya dhahabu?

Zile tume zilikuwa za wataalamu bobezi baadhi wakiwa professors kwenye eneo husika la Madini.

Nilishangaa Sana Na akaiita report yao eti rubbish...(takataka).

Frankly speaking that's high Level of stupidity I have never seen in my life.

Matokeo yake amevunjwa vipande vipande...na waliokuwa wanamshangilia wapo pembeni...wwngine wanachangishana ili awekwe sawa...tatizo ni kuwa mbowe ameswallow michango hiyo amnunulie wema...BMW new modern...kufa kufaana
 
Isitoshe basi kwenye bunge la katiba akasimama hadharani kwa kukosa hekima , lissu akasikika akisema Nyerere aliishi kwa kuzoea vya kunyonga vya kuchinja hakuviweza Na kwamba aliunganisha Tanganyika Na Zanzibar bila ya mkataba wowote ule.

Ni sehemu tu ya muendelezo wa kukosa Hekima na busara kwa wazee wako ambao ni sawa Na wazazi wako kisa ni mwanasheria Na wakili.
 
Back
Top Bottom