Hivi yule "Baba wa Demokrasia" wa kuigwa na TZ kutoka nchi jirani ni NANI TENA?

Hawezi kuwa baba wa democrasia tena imedhiirika

kwamba ni mnafiki na akishindwa uchaguzi sidhani

kama atakubali kuachia kiti huyu.
 
Mbona unakuwa kipofu kaka

ama ndio unajaribu kutuonyesha

love to death kwa Uhuru????
 
Unamjua ni nani alimuingizia Chief Justice Maraga KSh. 500,000,000 kwenye akaunti yake siku ya Alhamisi mchana - siku moja kabla ya uamuzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wewe kichwa Maji kweli, tofautisha kati ya July Bali uamuzi Wa mahakama na kuheshimu uamuzi Wa mahakama. alichokifanya Kenyatta ni kuheshimu uamuzi wa mahakama sio kukubali maamuzi yake. pili taasisi yoyote ya uma ipo wazi kushutumiwa na kupongezwa vilevile, hiyo ndo nature ya demokrasia. mahaka is not an exception, it is open to criticisms by any disgruntled person. hii tabia ya kukosoa taasisi ya uma sio dhambi au kosa la jinai kama vile unavyodhani. kumsweka mtu ndani kisa amekosoa taasisi ya uma ni ikoloni mambo leo na ujinga wa karne ya 18
 
Sasa kwa nini anaitishia mahakama kuwa watakiona akichaguliwa. Katika demokrasia inakuwaje mhimili wa URAISI utishie uhuru wa mhimili wa MAHAKAMA?

Sent using Jamii Forums mobile app
I88
 
Sasa kwa nini anaitishia mahakama kuwa watakiona akichaguliwa. Katika demokrasia inakuwaje mhimili wa URAISI utishie uhuru wa mhimili wa MAHAKAMA?

Sent using Jamii Forums mobile app
I88
usikurupe mkuu, isikilize hiyo clip vizuri, alichokisema ni kwamba wata revisit hiyo judgement baada ya huu uchaguzi, kurevisit ina maana kuangalia dosari za kisheria zilizotokea katika hayo maamuzi ili kurekebisha pia kisheria. pili hakuwatishia majaji, alichokisema ni kwamba kama asingekua mpenda amani na demokrasia wangekiona cha mtema kuni maana angeweza kuhamasisha wafuasi wake kutokuheshimu maamuzi ya mahakama kama alivofanya raila baada ya matokeo yalipotangazwa.
 
No no no!

Amerudia rudia kwenye jukwaa mpaka nikafikiri amelewa.

Unadhani ni kwa nini raisi wa mawakili wa Kenya, LSK (sawa na Lissu hapa) alimuonya Uhuru asiwatishie majaji na mahakama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mantiki ya mtoa post sijaielewa, hilo kongamano lililo fanyika ud hujatuambia lemezungumzia nini.. then unawaambia wa2 wafuate hayo mawazo, kweli watanzania tuna2mia asilimia 1 ya ubongo wetu
 
Kama serikali yako inafanya Mamb ya kipumbavu na nani wapumbavu unataka kushabikie vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mantiki ya mtoa post sijaielewa, hilo kongamano lililo fanyika ud hujatuambia lemezungumzia nini.. then unawaambia wa2 wafuate hayo mawazo, kweli watanzania tuna2mia asilimia 1 ya ubongo wetu
Usiwe mvivu na kupenda kulishwa kwa kijiko. Majadiliano ya hilo kongamano yamezagaa bwerere mitandaoni. Katafute.

Mantiki ya bandiko ni kuwaasa msikimbilie kusifia kila kipya cha nje na kukikashifu kile chenu. Imekuwa hulka ya wapinzani siku hizi kuwa chetu siku zote ni kibaya na vya nje ndio vizuri.

1. Walikimbilia kusifia uchaguzi wa Kenya kuwa wa kuigwa.

2. Mahakama ikaona kuwa ulikuwa batili , wakasifia mahakama.

3. Uhuru akakubali uchaguzi urudiwe, wakamuita "Baba wa Demokrasia" na wa kuigwa.

4. Sasa Uhuru amecharuka na anawatukana majaji na kuitishia mahakama na majaji kuwa watakiona kama atachaguliwa.

Ndio maana nikauliza, hivi ni huyu huyu Uhuru alieitwa Baba wa Demokrasia ndie anaeutishia mhimili huru wa MAHAKAMA kama akichaguliwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama serikali yako inafanya Mamb ya kipumbavu na nani wapumbavu unataka kushabikie vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa Tume Huru Ya Uchaguzi ya Kenya imefanya werevu kuipoka Kenya demokrasia kwa kuchakachua matokeo ya uchaguzi kwenye seva zao?

Je, ni werevu kwa Uhuru anaewania nafasi ya ukuu wa taasisi ya URAIS (mhimili huru) kutishia kuishughulikia taasisi ya MAHAKAMA (mhimili mwengine huru) katika mfumo wa kidemokrasia?

Je, bado TZ tunapaswa kuiga yaliyofanywa na tume huru ya uchaguzi ya Kenya.

Je, ni vema kwa Rais wa TZ kuitishia Mahakama asipokubaliana nayo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Mkuu mbaya zaidi ametoa ahadi ya kuwashughulikia. Anadai CJ Maraga hawezi kumchezea yeye bado ni Rais.

Jana nimeona Umoja wa Mahakimu na Majaji nchini KE wamelani vikali matamshi ya UHURU na wamedai hawawezi kutishwa wataendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria. Najiuliza je hapa TZ mahakimu wanaweza kutoa tamko la kulaani pale Rais anapoingilia uamuzi wa mahakama?
 
Binafsi sijawahi msifia Uhuru bali naona katiba yao ndo kitu bora . Hivyo Tanzania yatakiwa kuwa na katiba itakayoendana na wakati kama ilivyo kwa majirani zetu, separation of power is inevitable in todays world
 
Sasa kuna kitu gani kuzuri kuhusu Demokrasia hapa Tz?
 

Sijui kama hapa TZ majaji wanaweza kulaani tamko la Rais hadharani kama hawakubaliani nalo.

Pengine hapa TZ watu (hii mihimili mitatu) ni wastaarab na kuwa majaji hutoa ushauri wao kwa Rais katika faragha na sio barabarani.

Hii pia ni kweli kwa upinzani wetu. Pengine ushauri mwingi walionao wapinzani Rais angeufuata kwa moyo mweupe kama ungewasilishwa kwake kwa njia ya kistaarabu.

Kinachotokea hapa TZ ni kuwa upinzani ukiwa na wazo la kumuelekeza Rais basi hupanda majukwaani na kumdhalilisha Rais na serikali yake. Rais asipowapatiliza wanasema "haambiliki".

Hata wewe mkuu, kama nikija nyumbani kwako na kuanza kuponda kila ulichonacho kuanzia viti, baskeli yako, rangi uliopaka, n.k., unafikiri utanisikiliza ushauri wangu wa nini cha kufanya kuboresha maandhari yako?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona unakuwa kipofu kaka

ama ndio unajaribu kutuonyesha

love to death kwa Uhuru????
hapa ni "Love to Death kwa Democracy!" kitendo cha kutii maamuzi ya Mahakama japo hakubaliani nayo, siyo cha kawaida katika Afrika. Angalia mfano wa haya Mabaradhuli ya hapa kwetu, Mahakama imezuia ubomoaji yenyewe yanabomoa tu, mpaka yazuiwe na yule baradhuli mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sijawahi msifia Uhuru bali naona katiba yao ndo kitu bora . Hivyo Tanzania yatakiwa kuwa na katiba itakayoendana na wakati kama ilivyo kwa majirani zetu, separation of power is inevitable in todays world
You are absolutely right.

Katiba ya Kenya imenyoosha mambo mengi sana ya mwenendo wa nchi. Na sisi tunapaswa kuikamilisha ya kwetu.

Suala la muungano ni changamoto kubwa sana kwetu ambalo Kenya hawakuwa nalo walipokuwa wanarekebisha katiba yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…