Hivi UN bado ipo au ilishakufa?

Hivi UN bado ipo au ilishakufa?

Wazolee

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2018
Posts
3,924
Reaction score
4,521
Habari zenu Wana JF

Sababu za kuundwa UN ni kuzuia vita na madhara yake Duniani
Lakini Cha kushangaza watu wanaanzisha vita vya makusudi na UN ipo kimya tu hili kidogo linashangaza

Vita vya Ukraine na Urusi UN wameshindwa kuizuia isitokee pia wameshindwa kuingilia kati na kuamua

Vita vya Gaza na Israel UN walishindwa kuvizuia visitokee na wakashindwa kuingilia kati kuvimaliza

Vita vya Iran na Israel UN walishindwa kuvizuia visitokee na wakashindwa kuvimaliza

Marekani ameivamia Venezuela kapindua utawala na Sasa anaiba mafuta ya Venezuela UN wapo kimya

Na Sasa Marekani anataka kuanzisha Vita na Irani Ili apate nafasi ya kuiba mafuta , Gasi na Uranium ya Irani UN wapo kimya

Maana yake ni kwamba vita vya Dunia vinakaribia maana UN kazi ya kuzuia vita duniani imewashinda
 
Back
Top Bottom