Hivi tunakwenda wapi?

Nsaji Mpoki

JF-Expert Member
Nov 5, 2007
396
65
Majuzi tuliona spika na naibu wake wakifinyanga haki bungeni na wakatakiwa kujiuzulu. Mara yakaanza mauaji yanayohusiana na sababu za kidini tukataka waziri wa mambo ya ndani ajiuzulu.

Haukupita muda waziri wa maji naye akatakiwa kujiuzulu kwasababu haiingii akilini miaka 50 watu hata wa jiji kama la dar es salaam wakose maji safi na salama. Wakati hilo likiendelea watoto zaidi ya laki 3 wakafeli mtihani wa kidato cha nne tukataka waziri mhusika ajiuzulu.

Hivi sasa kuna mgogoro mwingine, hatari kama ule wa mizozo ya kidini ambao unachochewa na waziri mwenye dhamana ya michezo.

Huyu nae badala ya kusimamia haki amejitosa kuhakikisha kambi moja inashinda. Kwenye taarifa za habari za jana zilizorushwa na vituo vya televisheni mmeona wale vijana wanaosadikiwa kukutwa na meno ya tembo walivyouawa na wananchi wenye hasira.

Leo asubuhi kwenye kipindi cha tuongee asubuhi cha star tv mmemsikia nape akisema muundo wa wizara zetu unachangia kwa kiasi kikubwa kutokuwa na mtiririko mzuri wa kushughulikia masuala ya vijana na ajira. Huyu ni msemaji mkuu wa chama tawala.

Kama hali ni hii tumebaki na nini sasa ambacho tunaweza kujivunia? Na kwanini mhe. Rais asiamue tu kuwapumzisha kazi viongozi hawa badala ya kuendelea kuunda tume za kutafuna fedha?

Wakati umefika kwa waliopewa dhamana ya kuongoza taifa hili kuona kuwa madaraka waliyonayo yanatoka kwa wananchi na kwamba wanapaswa kuwajibika kwa makosa yaliyotokea.
 
Umesema vema ila tatizo ni kuwa wahusika ni vipofu kwenye suala la uajibikaji.
 
CCM (Chama cha Mafisadi) ni JANGA LA TAIFA.
Tunataka watufanyie nini ndipo tuelewe huu ujumbe?
Ndugu Mtanzania Mzalendo chukua hatua kila uchaguzi unapotokea ili tuweze kumuondoa MKOLONI MWEUSI a.k.a CCM kwenye UONGOZI wa nchi la siyo nchi itaendelea kuangamia kama unavyoona sasa !!!
 
Majuzi tuliona spika na naibu wake wakifinyanga haki bungeni na wakatakiwa kujiuzulu. Mara yakaanza mauaji yanayohusiana na sababu za kidini tukataka waziri wa mambo ya ndani ajiuzulu.

Haukupita muda waziri wa maji naye akatakiwa kujiuzulu kwasababu haiingii akilini miaka 50 watu hata wa jiji kama la dar es salaam wakose maji safi na salama. Wakati hilo likiendelea watoto zaidi ya laki 3 wakafeli mtihani wa kidato cha nne tukataka waziri mhusika ajiuzulu.

Hivi sasa kuna mgogoro mwingine, hatari kama ule wa mizozo ya kidini ambao unachochewa na waziri mwenye dhamana ya michezo.

Huyu nae badala ya kusimamia haki amejitosa kuhakikisha kambi moja inashinda. Kwenye taarifa za habari za jana zilizorushwa na vituo vya televisheni mmeona wale vijana wanaosadikiwa kukutwa na meno ya tembo walivyouawa na wananchi wenye hasira.

Leo asubuhi kwenye kipindi cha tuongee asubuhi cha star tv mmemsikia nape akisema muundo wa wizara zetu unachangia kwa kiasi kikubwa kutokuwa na mtiririko mzuri wa kushughulikia masuala ya vijana na ajira. Huyu ni msemaji mkuu wa chama tawala.

Kama hali ni hii tumebaki na nini sasa ambacho tunaweza kujivunia? Na kwanini mhe. Rais asiamue tu kuwapumzisha kazi viongozi hawa badala ya kuendelea kuunda tume za kutafuna fedha?

Wakati umefika kwa waliopewa dhamana ya kuongoza taifa hili kuona kuwa madaraka waliyonayo yanatoka kwa wananchi na kwamba wanapaswa kuwajibika kwa makosa yaliyotokea.

Kwa maana nyingine ni kwamba, "NAPE ANAPONDA MPANGILIO WA WIZARA ULIOUNDWA NA MWENYEKITI WAKE". Kwa nini asimkosoe wanapokutana pale Lumumba au Ikulu kwenye vikao vyao?
 
Kwa maana nyingine ni kwamba, "NAPE ANAPONDA MPANGILIO WA WIZARA ULIOUNDWA NA MWENYEKITI WAKE". Kwa nini asimkosoe wanapokutana pale Lumumba au Ikulu kwenye vikao vyao?
mwenye kutoa ushauri huyo darasa la saba, maana form four alifeli, sasa sijui ana zungumzia kazi gani, kama za kujisemea semea tu sawa anaweza
 
Bahati mbaya zaidi Mawaziri wetu hawajui lugha ya kujiuzulu, wamejaa viburi na dharau utafikiri wako juu ya sheria.
 
Mapangaji wa safu ya uongozi ni Bwana Mkubwa mwenyewe. Gharama za kuchaguana kwa uwahiba, uanamtandao na undugu unaligharimu taifa. Tusikwepe kuwa wawazi kwamba Bwana mkubwa aachie ngazi. Vinginevyo hadi mwaka 2015 nchi itakuwa na hali mbayaaaaaaaaaaaa mno.
 
Tunasikia kule wizara ya michezo kuna mkubwa kavuta kidogodigo toka kwa malinzi ndio sababu yuko tayari fifa ituumbue
 
Back
Top Bottom