Hivi TMA mnajua sana kiingereza!

Hivi TMA mnajua sana kiingereza!

Enzymes

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2013
Posts
4,332
Reaction score
3,018
Binafsi nashangazwa sna na nchi hii ya Tanzania! Taifa linalojidai kuwa Lugha yake ya Taifa ni Kiswahili.

Mikataba English, Makabrasha Ofisini English, Kadi za Matibabu Eng, kila kitu Eng.

Nazidi kuishangaa hii Mamalaka ya Hali ya Hewa Tz. Taarifa yake ina lenga kila mtanzania hasa anae jua kusoma na kuandika.

Na Taarifa hizi husambazwa kwa haraka sn kupitia kurasa mbalimbali. Mf za vyombo vya habari kama ITV, EATV, JAMII FORUMS, na magroup ya Whatsapp, Instagram, na fb.

JPM mwenye hii Ngeli haipendi balaaaa . Iweje mumuandikie Mkulima wa Katavi ngeli?

Ebu taasisi zote za serikali, TRA, UTUMISHI, TANROADS, POLICE, TMA, badilikeni. Ebu acheni ushamba wa akina Wema Sepetu!!
30c864db586d1de23a73fae2d9d39014.jpg
 
nifasilie

level of confidence kwa kiswahili kulingana na muktadha wa kilicho andikwa hapo

nimemuuliza rafiki yangu mkalimani na mfasili kanipa majibu yafuatayo
IMG_20171027_195109_373.JPG
 
nifasilie

level of confidence kwa kiswahili kulingana na muktadha wa kilicho andikwa hapo

nimemuuliza rafiki yangu mkalimani na mfasili kanipa majibu yafuatayoView attachment 618697
Mkuu, wao wangejua lugha au maneno fasaha nacsahihi ya kutumia. Mf. taarifa zote za Ikulu ni Kiswahili tena fasaha.
 
nifasilie

level of confidence kwa kiswahili kulingana na muktadha wa kilicho andikwa hapo

nimemuuliza rafiki yangu mkalimani na mfasili kanipa majibu yafuatayoView attachment 618697
Nadhani wewe ni wale mnaoshindwa kutafsiri lugha kwa njia fasaha na badala yake mnafanya tafsiri sisisi.

Level of confidence kwa muktadha huo ni kiwango cha uhakika au kwa kifupi "uhakika wa utabiri" husika, ambapo wao wamesema ni asilimia 70.

Nyie ndio mkiona maneno "go on" mnasema maana yake ni "nenda juu" badala ya "endelea" na kudhani ni vigumu kutafsiri kingereza kumbe mnatumia google translate badala ya kutumia fikra
 
Wewe una bahati mbaya umepata ya kiingereza, ipo ya kiswahili, na mara zote maandiko yote ya hali ya hewa hutolewa kwanza kwa ligha ya kiswahili.
 
NILIENDA TABATA PALE ROMAN CATHOLIC KULE NDANI KUNA SHULE.KUNA UKUMBI.KRISTO MFALME.KA BLA YA KUFIKA KUNA KIBAO.SPEAK ENGLISH. NIKAJIULIZA KWA.Kama taifa kuna tulikokosea kwnye elimu.ona Uganda, Kenya sis mmmm English Shida
 
Binafsi nashangazwa sna na nchi hii ya Tanzania! Taifa linalojidai kuwa Lugha yake ya Taifa ni Kiswahili.

Mikataba English, Makabrasha Ofisini English, Kadi za Matibabu Eng, kila kitu Eng.

Nazidi kuishangaa hii Mamalaka ya Hali ya Hewa Tz. Taarifa yake ina lenga kila mtanzania hasa anae jua kusoma na kuandika.

Na Taarifa hizi husambazwa kwa haraka sn kupitia kurasa mbalimbali. Mf za vyombo vya habari kama ITV, EATV, JAMII FORUMS, na magroup ya Whatsapp, Instagram, na fb.

JPM mwenye hii Ngeli haipendi balaaaa . Iweje mumuandikie Mkulima wa Katavi ngeli?

Ebu taasisi zote za serikali, TRA, UTUMISHI, TANROADS, POLICE, TMA, badilikeni. Ebu acheni ushamba wa akina Wema Sepetu!!
30c864db586d1de23a73fae2d9d39014.jpg


Nadhani mwenye matatizo ni wewe, rudia tena kusoma utaona tangazo kama hili kwa lugha ya kiswahili
 
Nadhani mwenye matatizo ni wewe, rudia tena kusoma utaona tangazo kama hili kwa lugha ya kiswahili
Tulijua mtakuja kujitetea.

Ebu tuwekee hapa chapisho la kiswahili. Hata website ni English.
 
Kumbe !!

Nenda juu ya page kuna sehemu wameandika "Kiswahili" bonyeza
Huo ndio ujinga. English ndio inge andikwa hivyo! Ww umeona Tangazo la Kiswahili la hii taarifa?

Nenda China, Japan, Korea au Wapi...National Language ni kils kitu.
 
Huo ndio ujinga. English ndio inge andikwa hivyo! Ww umeona Tangazo la Kiswahili la hii taarifa?

Nenda China, Japan, Korea au Wapi...National Language ni kils kitu.

Tatizo lako ni nini?

Web page yao inasomeka kwa Kiswahili na Kiingereza, chagua lugha unayotaka.
 
Tatizo lako ni nini?

Web page yao inaosomeka kwa Kiswahili na Kiingereza, chagua lugha unayotaka.
Tunataka Lugha ya Taifa iheshimiwe na ithaminiwe. Taarifa zote za Tahadhari zitolewe kwa Kiswahili.

Lugha inayo weza kueleweka kwa kila mtanzania anaejua kusoma na kuandika.

Eng ndio iwe Option.
 
Nadhani wewe ni wale mnaoshindwa kutafsiri lugha kwa njia fasaha na badala yake mnafanya tafsiri sisisi.

Level of confidence kwa muktadha huo ni kiwango cha uhakika au kwa kifupi "uhakika wa utabiri" husika, ambapo wao wamesema ni asilimia 70.

Nyie ndio mkiona maneno "go on" mnasema maana yake ni "nenda juu" badala ya "endelea" na kudhani ni vigumu kutafsiri kingereza kumbe mnatumia google translate badala ya kutumia fikra
ndio maana nimeomba tafsiri kwa sababu mimi binafsi nimeshindwa

hayo mengine ya "nyie ndio wale" ni mbwembwe tu za kutaka uonekane kuwa na wewe umo kwenye kuimudu vyema hiyo lugha.

Ahsante maalimu kwa msaada wako.
 
Kinachonifurahishaga ni hizo email na number za simu, hazipatikani, zikipatikana hazipokelewi... Email ndiyo hazijibiwi kabisa...

Fax ndiyo kabisaaa...


Cc: mahondaw
 
Hivi wanavyosema mvua za 50mm yani hizo 50mm zikidondoka ndo inakua shughuli kama tulivyoziona madaraja kung'oka, njia hazipitiki na nyumba kubomoka
 
Back
Top Bottom