Hivi michepuko wote mko hivi?

HaMachiach

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2015
Posts
3,445
Reaction score
6,208
Habari wanabodi,

Nimekuja kuomba ushauri. Nimeoa mwezi uliopita sasa kuna kamchepuko kangu kamenasa mimba mwezi niliofunga ndoa, sasa kananisumbua balaa kila muda kanataka niwe nako halafu wameungana na dada yake yaani anataka nimthamini kuliko mke wa ndani.

Nikiwa kazini anatuma text njoo nyumbani la sivyo natoa mimba, yaani amekuwa kero kwakweli. Dada yake anamsapoti sana nimechoka.

Juzi nilimwambia nasafiri kikazi nje ya mkoa akataka niende nae nikagoma akaanza kusema yeye basi anatafuta mtu mwingine maana ana genye, nikasema tafuta tu mimi sitaki mahusiano ya kimapenzi na wewe..., akaanza basi mimi natoa mimba siwezi lea kiumbe asiye na faida.

Kwa kweli mchepuko huu ni taabu tu.
 
Wewe??? nakuuliza wewe umeoa??

Unajua maana ya kuoa???

Kama unajua maana ya kuoa, sidhani kama utakuwa umeoa.

Yani wenzako waliooa mwezi uliopita hivi sasa wako honeymoon we uko hapa unatuletea habari za michepuko...

Mi nadhani hujaoa bali umeozeshwa.
 
Achana nae unafikiria alikuwa wako peke yako anakuchanganya uharibu hayo amunganisho yako
 
Na we we..si umwache atoe kwani sh ngapi akaa
 
Mkuu pole na hao viumbe. Nakushauri achana naye mapema atakuja kukusumbua mbeleni, lkn kubwa zaidi ukizid kuwa karibu naye anaweza mpoteza mkeo ili abaki na uhuru wa 100%.
 
Mkuu pole na hao viumbe. Nakushauri achana naye mapema atakuja kukusumbua mbeleni, lkn kubwa zaidi ukizid kuwa karibu naye anaweza mpoteza mkeo ili abaki na uhuru wa 100%.
Nmemwambia atowe tu maana naona ndio tiketi ya kunisumbua
 
Hahahaaaa ameozwa nimecheka sana, kweli kabisa kwa mwezi mmoja amezidi. Ndio maana nilishajiambia nitakuja kuoa siku nikipenda kweli kiasi kwamba hizi story za michepuko iwe kila nikipata kishawishi nikimkumbuka wife home mzuka unakata nanyosha goti nyumbani.
 
 
Upumbavu mwingine mnautafuta wenyewe, we kama umeoa kwann usitulie kwa mkeo na kama umeona umeshindwa umekwenda kwa mchepuko kwanini umpe mimba? Kama vp mwambie atoe baki na mkeo, au kubali kuendeshwa vivyo hivyo, si umeyataka
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…