Hivi Marekani hakuna walemavu?

Hivi Marekani hakuna walemavu?

Zeni2017

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2017
Posts
1,247
Reaction score
534
Kuna kawaida ya watanzania kuposti picha za walemavu kwenye mitandao na kukomenti Amin, Mungu amsaidie, Mapenzi ya bwana yatimizwe na vitu vya aina hiyo.

Sasa najiuliza kutimizwa kwa haya mapenzi ya bwana ni kwa kuteseka walemavu wa Tanzania tu? Mbona kwa wenzetu walemavu wote wana misaada mpaka utafikiri hawapo.

Watu elfu saba badala ya kukomenti Amin wakichanga elfu na mia tano kila mmoja zitapatikana shilingi milioni kumi na laki tano. Pesa ya kutosha kumnunulia mlemavu wheelchair na kumfungulia mfuko wa elimu mpaka chuo kikuu.

Na tunashindwaje kuanzisha shule za walemavu kwa michango ya wananchi? Kwa wenzetu kodi zinatumika kusaidia walemavu sisi tunaweza kujipanga wenyewe kibongo bongo angalau kila mkoa ukawa na vituo/shule moja ya walemavu. Wakuu wa mikoa changamoto hiyo

a2e6eca7aaebe9639acd7029c511ae56.jpg
 
Kinachotuchelewesha sana ni hii tabia mbaya ya kutokuwa na community owned resources,tunasubiri serikali kwa visingizio vya kodi,Tatizo lipo hapo mlipo mkianza kutatua huyo serikali atasapoti kwani matatizo yetu hayafanani. Ndiyo maana tunaletewa miradi ambayo haituhusu kabisa.
 
Usipoangalia unaweza ukajikuta unatengenezea watu dili. Anza wewe na Marafiki hapo ulipo weka mfano wenu kwenye hiyo mitandao na wengine watafata.
Haifai kuwatenga walemavu kwenye shule zao peke yao inatakiwa wajumuishwe na watoto wenzao ili iwe rahisi kusaidiwa.
 
Alafu kule vilema wapo ila wanaamini kuwa japo ni vilema ila bado wanaweza kuwa na mchango kwenye jamii,they have something to make a world a better place kwa watu wote kuishi,sasa huku kwetu mtu akishakuwa kilema ndio anakuwa kilema kweli kweli yaani hata umuwekee fungu la nyanya hapo awauzie hata wapita njia,aah wapi mwingine unakuta ni kilema nayeweza kufanya kitu kikubwa tuu kwenye jamii lakini ameshajiaminisha kuwa yeye ni kilema,ukisema sana utaambiwa unabeza vilema vya wenzio,hapana si kubeza ila kila mtu ana kipaji au kitu mungu amempa kiwasaidie wengine
 
Mtu kukoment anaona rahisi zaid ya kuchangia... Umshauri mtu atoe hela c mchezo
 
Back
Top Bottom