Hivi kuna mtu amewahi ielewa design ya barabara hapa Kimara mwisho?

Hivi kuna mtu amewahi ielewa design ya barabara hapa Kimara mwisho?

Lavit

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
15,849
Reaction score
36,141
Nadhani kila mmoja anaelewa kwa Morogoro road ndiyo njia kuu ya kuingia Dsm, kwa namna yeyote mimi nilitegemea hii barabara ingewezeshwa ili iweze kupitika kwa urahisi muda wote!

Ila kituko kinaanza pale Kimara mwisho, licha ya uwekezaji mkubwa kwenye kituo cha BRT sidhan kama waliwafikiria watumiaji wengine. Kimara muda wote pana folen, na watu wanaotoka mjini wakishavuka pale folen inakuwa imeisha. Pamoja na utanuzi wa barabara wanaofanya mimi sioni kama tatizo linaenda kuisha pale (kwanza barabara yenyewe toka ilivyoanza hata haiishi, hata huo utanuzi wake ni kama wanafanya utani maana barabara bado ni finyu sana kwa pale kimara Terminal.

Kingine licha ya wakazi kutosha pande zote mbili za kimara ila huwezi vuka toka upande mmoja kwenda mwingine moja kwa moja ukiwa na gari, mtu anayetoka upande ilipo TRA na anataka kwenda uelekeo wa bunyokwa basi ni lazima aende mataa yaliyo mbele ya Korogwe ama aende Stopover. Mwanzo palikuwa na round about ambayo inatoa magari upande mmoja tu. Kwa sasa pale wamepavuruga na sijui wanakuja na design gani!

NB: Kama design za kawaida kabisa hizi za barabara zinatutoa jasho, kuna siku tutatoka kweli kwenye huu umaskini wa dunia ya tatu?
 
Kutokana na harakati za ujenzi kuzunguka inabidi stopover au butcher lkn baada ya barabara kukamilika round about kimara itarudi kama awali kwa kuwa hata structure ilipofikia sasa inaonyesha hivyo
 
Pale sahivi inaisha ile jam. Ukifika Kimara mwisho mchawi wa foleni ni daladala na bajaji zinasimama hapo zinaanza kushusha.

Sasa sahivi wao watakua wanaingia kituoni nje kabisa ya barabara. Hafu kwa mbele ile round about inarudi.

Pale ata sahivi saa 4 tukicheki Google Map pana jam. Jau sana.
IMG_0598.png
 
Nadhani kila mmoja anaelewa kwa Morogoro road ndiyo njia kuu ya kuingia Dsm, kwa namna yeyote mimi nilitegemea hii barabara ingewezeshwa ili iweze kupitika kwa urahisi muda wote!

Ila kituko kinaanza pale Kimara mwisho, licha ya uwekezaji mkubwa kwenye kituo cha BRT sidhan kama waliwafikiria watumiaji wengine. Kimara muda wote pana folen, na watu wanaotoka mjini wakishavuka pale folen inakuwa imeisha. Pamoja na utanuzi wa barabara wanaofanya mimi sioni kama tatizo linaenda kuisha pale (kwanza barabara yenyewe toka ilivyoanza hata haiishi, hata huo utanuzi wake ni kama wanafanya utani maana barabara bado ni finyu sana kwa pale kimara Terminal.

Kingine licha ya wakazi kutosha pande zote mbili za kimara ila huwezi vuka toka upande mmoja kwenda mwingine moja kwa moja ukiwa na gari, mtu anayetoka upande ilipo TRA na anataka kwenda uelekeo wa bunyokwa basi ni lazima aende mataa yaliyo mbele ya Korogwe ama aende Stopover. Mwanzo palikuwa na round about ambayo inatoa magari upande mmoja tu. Kwa sasa pale wamepavuruga na sijui wanakuja na design gani!

NB: Kama design za kawaida kabisa hizi za barabara zinatutoa jasho, kuna siku tutatoka kweli kwenye huu umaskini wa dunia ya tatu?
Ni premature kukosoa kinachoendelea pale especially kwa layman kama wewe. Tulia waache wataalamu wamalize kazi.

Miluzi mingi porini humpoteza mbwa
 
Pale sahivi inaisha ile jam. Ukifika Kimara mwisho mchawi wa foleni ni daladala na bajaji zinasimama hapo zinaanza kushusha.

Sasa sahivi wao watakua wanaingia kituoni nje kabisa ya barabara. Hafu kwa mbele ile round about inarudi.

Pale ata sahivi saa 4 tukicheki Google Map pana jam. Jau sana. View attachment 3493124
Hivi na hizi njia mpya zilizotengenezwa ni kwamba wameshindwa kuweka level moja na zile za zamani au ujenzi haujakamilika?
 
Hivi na hizi njia mpya zilizotengenezwa ni kwamba wameshindwa kuweka level moja na zile za zamani au ujenzi haujakamilika?
Walikua hawajaweka layer ya juu nadhani wakawa pushed wafungulie watu watumie
 
Back
Top Bottom