Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,410
- 119,112
Habari wanaJf
Kichwa kinajieleza, hivi hii tabia ina maana gani? Kwa kweli haipendezi hata kidogo, dada yangu Karucee huwa amezoea kusema 'Jf is a jungle, tread carefully'... Kwamba ni lazima uwe makini, si lazima kila anayetaka kujuana na wewe unampa access, lazima uwe selective hata kama imetokea umeinteract na mtu ambae si mwema iwe ni kwa bahati mbaya na sio Jf tu hata katika maisha ya kawaida.
Siku za nyuma kidogo nilipokea messages kutoka kwa watu nisiowajua lakini baada ya kuhojiana nao niligundua ni wanajf wenzangu, katika kumuuliza mmoja mmoja namba yangu mmepata wapi nikatajiwa watu ambao mimi sijawahi kuwapa namba yangu kwa kweli nilishangaa halafu nilikwazwa...naomba nieleweke kwamba kilichonikwaza si wale watu kuwa na namba yangu maana ni watu wema tu wenye heshima zao kwa nje, kuhusu utu wao wa ndani siwezi kujua.
Kilichonishangaza ni mtu kutoa tu namba ya mtu kama vile ya kwake . hum ndani bwana ni kichaka huwezi kujua nani na nani wana uhusiano gani,wengine wapenzi,wengine ma ex, wengine wakewenza, wengine wachawi n.k kwa hiyo unapokuwa unatoa mawasiliano ya mtu hujui yule unayempa ana nia gani na huyo mhusika.
Mtu anapoamua kukupa mawasiliano amekuamini wewe na hata kama ameamua kujilipua amejilipua kwako kwa sababu anazojua yeye na anaona kuwa ni za msingi kwa hiyo please naomba tuheshimu privacy za watu. Kama kwako wewe mawasiliano ni suala jepesi tu sio kwa kila mtu lakini nadhani hata kwenu ipo hivyo maana sijawahi kuona mtu anaweka ovyo ovyo namba kwenye thread.
Ni hayo tu kwa leo
#nohardfeelings
Kichwa kinajieleza, hivi hii tabia ina maana gani? Kwa kweli haipendezi hata kidogo, dada yangu Karucee huwa amezoea kusema 'Jf is a jungle, tread carefully'... Kwamba ni lazima uwe makini, si lazima kila anayetaka kujuana na wewe unampa access, lazima uwe selective hata kama imetokea umeinteract na mtu ambae si mwema iwe ni kwa bahati mbaya na sio Jf tu hata katika maisha ya kawaida.
Siku za nyuma kidogo nilipokea messages kutoka kwa watu nisiowajua lakini baada ya kuhojiana nao niligundua ni wanajf wenzangu, katika kumuuliza mmoja mmoja namba yangu mmepata wapi nikatajiwa watu ambao mimi sijawahi kuwapa namba yangu kwa kweli nilishangaa halafu nilikwazwa...naomba nieleweke kwamba kilichonikwaza si wale watu kuwa na namba yangu maana ni watu wema tu wenye heshima zao kwa nje, kuhusu utu wao wa ndani siwezi kujua.
Kilichonishangaza ni mtu kutoa tu namba ya mtu kama vile ya kwake . hum ndani bwana ni kichaka huwezi kujua nani na nani wana uhusiano gani,wengine wapenzi,wengine ma ex, wengine wakewenza, wengine wachawi n.k kwa hiyo unapokuwa unatoa mawasiliano ya mtu hujui yule unayempa ana nia gani na huyo mhusika.
Mtu anapoamua kukupa mawasiliano amekuamini wewe na hata kama ameamua kujilipua amejilipua kwako kwa sababu anazojua yeye na anaona kuwa ni za msingi kwa hiyo please naomba tuheshimu privacy za watu. Kama kwako wewe mawasiliano ni suala jepesi tu sio kwa kila mtu lakini nadhani hata kwenu ipo hivyo maana sijawahi kuona mtu anaweka ovyo ovyo namba kwenye thread.
Ni hayo tu kwa leo
#nohardfeelings