Hip hop,mistari,misumari,vina vikali (Special thread).

Hip hop,mistari,misumari,vina vikali (Special thread).

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,419
Reaction score
18,368
Usicoment hapa kama huna vina,
hatutafuti majina,
natiririka na vina,mpaka wapinzani wanasimama wima,

Moyo umekua mwepesi, sababu ya vitu vingi tumevitupilia mbali. Wakati wowote ule unapohitaji vitu flani, bidii ni kitu cha lazima.Tanzania ni inchi ya watu wengi wenye makabila mbali mbali. Na wenye mali na hali mbali mbali. Msimamo wangu ni mkali mithili ya pili pili. Ukipita mahala flani unawawacha watu wakilia,nikama wakati vitungu vinatayarishwa.Sitaki kuonekana nikama nimepoteza wanaosoma mawazo haya lakini kuwaelimisha kwa kiwango flani. Ndiyo badaye nisikie flani na flani alibarikiwa kwa kusoma yale maandishi niliyoandika. Lugha ni mgumu mno lakini ni bora kushinda kutosoma ama kuandika mawazo niliyonayo. Nataka niwe marufu kwenye msafara, jina liweze kungara, litambulike kati ya majina marufu duniani. Wakati Professor Jay, Juma Nature na Solo Thang wanapoitwa, jina langu liweze kutajwa wakati huo,mi sio bongo fleva ila najaribu tu kutunza tamaduni iliyo njema
 
Mie ni mganga anaejiganga kiganga bila usinga,vanga wala manyanga mganga naganga njaa
Pia ni mhanga wa majanga ninaeringa kwa kuubaka ujanja kijinga jinga bila kinga hadi wajinga wanashangaa
Na ni machinga nilietokwa na kiranga nilipotembeza khanga kwa mabinti wa kitanga walipo nionesha shanga nikapoteza ushujaaaaaa.......
Hii ni siri sirini msiri jasiri kwa umahiri naitunza
Naistiri kwa siri mtungini kwa uhodari uliothiri wenye siri wanajifunza.......BY Idriss Baraghash
 
mi ndo niko hapa/
nani anajiita snipa/ mtengwa ananikubali mpaka anaapa/
mnajifanya wajeuri ila nawapiga chapa/
na wengi mnaapa/mistari yangu inawachapa/
 
Last edited by a moderator:
Mie ni mganga anaejiganga kiganga bila usinga,vanga wala manyanga mganga naganga njaa
Pia ni mhanga wa majanga ninaeringa kwa kuubaka ujanja kijinga jinga bila kinga hadi wajinga wanashangaa
Na ni machinga nilietokwa na kiranga nilipotembeza khanga kwa mabinti wa kitanga walipo nionesha shanga nikapoteza ushujaaaaaa.......
Hii ni siri sirini msiri jasiri kwa umahiri naitunza
Naistiri kwa siri mtungini kwa uhodari uliothiri wenye siri wanajifunza.......BY Idriss Baraghash
unajiganga ila huna ujanja/
chana mistari uwe mjanja/
wanjanja tunakula mapaja/
 
Mi mweusi roho yangu haifugi chuki,dada anasema usiposoma mdogo wangu utarudi bushi.
 
Hii mike ni shamba na mimi ndo mkulima, navuna ninachopanda na ulimi ndo unalima, hapo utaganda kumbuka huu sio ujima mzazi mwambie mwana mjini si pakupima.
 
Naandika kwenye haka Ka-simu hadi wananiita mganga/ mkali nimeshatia timu Viol anzaga kujipanga/ mweusi wa arusha nawakilisha na hii kasi kazini/ stimu nishazirusha sababu nimezilipia dukani/ kwenye jukwaa la michano, niite moderata/ hapa mambo mswano, ama vipi majita/
 
NIPE midundo inipe tafu

Sihitaji mdundo, wakunipa tafu/ utozi nauweka kando, nahitaji kaya pafu/ mistari imeenda jando, dada ako ataisifu/ jide binti komando, mtengwa kijana mhalifu/
 
matumizi bila akiba, fedha hazitatui ukiumia
usupastaa ni mzigo wa mwiba, ukiubeba utaumia
hii dunia ina mambo, kama wasemavyo watu pori
ndo mana nikipata mpira basi kinachofuata goli
ujanja ukiuzidisha, si muda mfupi utaitwa mshamba
nilianza rap enzi hizo Sinza watu wanauziwa viwanja
unga ukamfunga kamba, mc hukatikia
pembamba
mwenzetu yule anaigiza, anauliza huu
wapi mwanga
sasa kwa ubishi na hasira kama Squizer mimi naja
kwa mshindo wa haja kama mvunjiko wa bawaba
nikienda chimbo haipiti wiki,yaani haizidi siku saba
huyu jamaa anaitwa muda, siyo raafiki wa mwanadamu
atakukosesha mavumba kama hauko on time
aaminiae kwa mdomo, siku zote haishi kutema
asante mola kwa hi sauti ya busara leo nasema
maisha kama kioo, ukiyachekea nayo yanacheka
na hii mipaka bila uhuru Afrika ni utumwa wa kifikra
chagua ufe Kijerumani anguke na tai shingoni
au Mchaga anayeshinda njaa wakati anazo hela mfukoni
huu sio wakati wa kujaribu, wenzako wanafanya kweli
au hujui bahari tulivu haimpimi nahodha wa meli
ona wasio na hatia wanapelekwa gerezani
halafu wavunjaji wa sheria wanaachwa wa jazane uraiani
we unadhani, nuru bandia za shetani zitaharibu imani
za wale wanaougua na kulia juu ya makosa ya mtu fulani
maneno yangu mi ni ya moto, na mdomo wangu hauna friji
yananitoka bila yakupooza, najiuliza nimeyameza vip

By fid q
 
unajiganga ila huna ujanja/
chana mistari uwe mjanja/
wanjanja tunakula mapaja/
mapaja? waza mema sio mabaya/ ukijidai mjanja nitakududubaya/ natisha sura jeusi mithili ya vampaya/ the don dollar emcee mbaya/ ona nina vina vimesanda ni vibaya/ natukana matusi mi ni baba ubaya/ nauza unga mtaani mi saplaya......... oi
 
safi sn nakumbuka freestyle za mawingu . Back in days hip hop for life.
 
Baraka na neema za jah/
Asubuh ya michano vina n furaha//
class navunzwa mfalme usiwe juha//
Marijan rajabu msako mpenz zurekha//
 
Mie ni mganga anaejiganga kiganga bila usinga,vanga wala manyanga mganga naganga njaa
Pia ni mhanga wa majanga ninaeringa kwa kuubaka ujanja kijinga jinga bila kinga hadi wajinga wanashangaa
Na ni machinga nilietokwa na kiranga nilipotembeza khanga kwa mabinti wa kitanga walipo nionesha shanga nikapoteza ushujaaaaaa.......
Hii ni siri sirini msiri jasiri kwa umahiri naitunza
Naistiri kwa siri mtungini kwa uhodari uliothiri wenye siri wanajifunza.......BY Idriss Baraghash

Dah, nimekuelewa sana. Lol.
 
Back
Top Bottom