Hili nalo neno

Hili nalo neno

ni nini hizi
avatar112514_3.gif

Hizo nyingi ni United States Dollars na hizo nyekundu zinaonekana chache ni Tanzanian Shillings
 
Vijana wa siku hizi ndo maana tunakufa mapema..Hatuwajali wazazi tunaendekeza sana starehe...
Mungu amekubariki umepata kazi nzuri angalau,mkumbuke mama yako japo umbadilishie Kitenge chake kilichochakaa..Mkumbuke Babako japo na kiatu,kila akikivaa ajisikie kweli ana mtoto...Kumbuka wadogo zako japo na Uniform mpya uwapunguzie mzigo wazazi kwa vitu vidogo vidogo..

Sasa wewe ni Bar tu,Bata tu,kila mahali unajifanya we ndo wewe wakati wazazi wamekusomesha kwa shida,walijinyima ili uwe na maisha mazuri,umewasahau..

Unajidai wa kishua sana mtaani wakati nyumba yenu imeezekwa na bati la msaada limeandikwa KORIE mafuta bora ya kupikia na kenchi za miti...Kumbukeni mlikotoka,kidogo ulichonacho jaribu ku-improve maisha ya nyumbani kwenu.

Wazazi wakikubariki hata mambo yako yatakunyookea.,Tunakosa baraka hivi hivi kwa kujifanya wajuaji..Ushauri tu wa Bure...Love your parents.........
Ni kweli,mtu anajidai ana kazi nzuri,ana piga mizinga watu,anapenda muda wote awe na maisha makubwa huku wazazi wakiwa na maisha ya ajabu kijijini.kuna watu humu wazazi wao inawezekana hawataona wajukuu zao/ wanaoweza kuwasimulia wao walikuwa wanaishi vipi,
Ukiwajali wazazi utaishi miaka mingi,mtu anasahau hata kwao walikuwa wanaishi vipi,jamani,ukijua hali ya nyumbani utakuwa mstaarabu sana sana kwa wote.
 
Back
Top Bottom