Hili la Mbunge Lijualikali ni dogo,alichokifanya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu alistahili lupango

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,739
32,874


Wakati mwingine ukikaa na kutazama "siasa" za Afrika na hususani Tanzania kama nchi mama,unapata kigugumizi cha fikra na aina ya maisha ambayo sisi kama wa Waafrika na Taifa kwa ujumla tunayaishi.

Wanayoyaongea wanasiasa sio yale wanayatenda.Unaweza kuwa unamuheshimu sana Rais,Mbunge au diwani,lkn ukitazama matendo yake na nia juu ya wananchi wake unabaki "kumdharau" sana.Hata kama ni dharau za nyuma ya keyboard ili kunusuru uhai wako,lkn bado uamdharau tu.

Kuwa na siasa za upinzani(vyama vingi) katika Afrika ni unafiki sana.Na sijui hawa watu huyo Mungu wao wanaomwabudu huwa wanamwambia nini wawapo katika usiri wa kiroho.

Mwaka 2010,kwenye jimbo la Maswa Mashariki,mgombea wa CCM wakati huo,ndugu Simon Kisena ambaye ndiye mmiliki wa UDA na UDART.Mgombea huyo alimpiga "ngwara" Kamanda wa Wilaya.Afande alikula ngwara mbele za watu na vijana wake.Kisena ndio huyo anadunda na UDA ya magumashi na UDART yenye usanii.

Usiongelee juu ya Job Ndugai na Chilongani.Na ili kumpoza bwana Chilongani,basi mamlaka zikampa Ukuu wa Wilaya ili asahau kipigo cha fimbo ya kichwa.

Kali ya mwaka ni ile ya Dr Titus Kamani,wakati huo akiwa mbunge na Waziri wa Mifugo,huyu kila mahali alionekana akiwafanyia fujo watangaza matokeo na kuwasukuma polisi huku na kule.Hili nalo lilipita.

Watawala wanataka kutuaminisha kuwa kuna kundi linaloweza kuadhibiwa likivunja sheria na lingine hapana.

Ndio maana Selukamba alivyotamka fu*** bungeni aliendelea kudunda tu.Haya yote watu wanayanukuu na kuacha yapite kwa muda,ila siku wakichoka watayafukunyua.

Haki huinua Taifa.
 
Kama hayo yaliotokea Maswa bado hayatengenezi uhalali kosa la Lijualikali.. Inawezekana mahakama umeona bora kutoa fundisho kwa wanasiasa.. Maana matukio ya kisena na ilo la Maswa yametokea kabla ya hili la kilombero.. Inawezekana hukumu hii imetaka kutoa fundisho
 
Hilo la Kisena huko Maswa lilinishangaza zaidi pale polisi walipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu hatua zitakazochukuliwa msemaji wao akaishia kusema ni suala binafsi kati ya Kisena na OCD; watamalizana wenyewe! Tangu pale nilijua Kisena ni "untouchable".
 
Mkuu mleta UZI hayo yote unayo yasema yametokea KIPINDI CHA ZAMA za yule MZEE WA WATU mliyekuwa mna muita DHAIFU ambaye leo hii mna MUONA ni HERO wetu na HAKUNA kesi ambayo ipo MAHAKAMANI juu ya HAO ULIOWATAJA mpaka sasa...na kama zingekuwepo ungeona ambacho KINGEWATOKEA kama wangekutwa na HATIA katika AWAMU hii.....KUKUSAIDIA tu AWAMU hii atuangalii mtu usoni...Mfano mdogo WE MSIKILIZE MKUU WA NCHI ASIVYO NA SONI juu ya watu wanaotenda UPUUZI....sasa msitake kuhararisha UPUUZI wa huyo MBUNGE kuwa alichofanya si KOSA.....SOMENI ALAMA ZA NYAKATI........kibaya zaidi WATANZANIA hatujui ni nini TUNACHOTAKA...tuna UNAFIKI...UVIVU...WA MBEA NA KUPENDA SANA VYA BURE.......ndio maana unakuta TOTO ZIMA LA KIUME NA NGUVU ZAKE LINA LIA LIA ETI MAISHA MAGUMU na hapo unamkuta amekaaa tu.....Mwisho wa siku wananunuliwa VIROBA na kuja KUANDIKA PUMBA HUMU
 
Alipofanya hivyo, nawe ukashuhudia, ULIENDA KUSHITAKI? Mahakama haiwezi kuhukumu ama kutoa adhabu kwa kesi isiyoletwa mezani kwake
 
Mkuu mleta UZI hayo yote unayo yasema yametokea KIPINDI CHA ZAMA za yule MZEE WA WATU mliyekuwa mna muita DHAIFU ambaye leo hii mna MUONA ni HERO wetu na HAKUNA kesi ambayo ipo MAHAKAMANI juu ya HAO mpaka sasa...na kama zingekuwepo ungeona ambacho KINGEWATOKEA kama wangekutwa na HATIA katika AWAMU hii.....KUKUSAIDIA tu AWAMU hii atuangalii mtu usoni...Mfano mdogo WE MSIKILIZE MKUU WA NCHI ASIVYO NA SONI juu ya watu wanvyotenda UPUUZI....sasa msitake kuhararisha UPUUZI wa huyo MBUNGE kuwa alichofanya si KOSA.....
Sasa unataka kutuaminisha kwamba hayo ni maagizo kutika juu
 
Mkuu mleta UZI hayo yote unayo yasema yametokea KIPINDI CHA ZAMA za yule MZEE WA WATU mliyekuwa mna muita DHAIFU ambaye leo hii mna MUONA ni HERO wetu na HAKUNA kesi ambayo ipo MAHAKAMANI juu ya HAO ULIOWATAJA mpaka sasa...na kama zingekuwepo ungeona ambacho KINGEWATOKEA kama wangekutwa na HATIA katika AWAMU hii.....KUKUSAIDIA tu AWAMU hii atuangalii mtu usoni...Mfano mdogo WE MSIKILIZE MKUU WA NCHI ASIVYO NA SONI juu ya watu wanaotenda UPUUZI....sasa msitake kuhararisha UPUUZI wa huyo MBUNGE kuwa alichofanya si KOSA.....SOMENI ALAMA ZA NYAKATI........kibaya zaidi WATANZANIA hatujui ni nini TUNACHOTAKA...tuna UNAFIKI...UVIVU...WA MBEA NA KUPENDA SANA VYA BURE.......ndio maana unakuta TOTO ZIMA LA KIUME NA NGUVU ZAKE LINA LIA LIA ETI MAISHA MAGUMU na hapo unamkuta amekaaa tu.....Mwisho wa siku wananunuliwa VIROBA na kuja KUANDIKA PUMBA HUMU

Aliyeamua na kutoa hukumu ni Magu au mahakama? Mbona una hoja dhaifu mno? Na wewe ni mtz msomi kbs? Duh
 
Kama hayo yaliotokea Maswa bado hayatengenezi uhalali kosa la Lijualikali.. Inawezekana mahakama umeona bora kutoa fundisho kwa wanasiasa.. Maana matukio ya kisena na ilo la Maswa yametokea kabla ya hili la kilombero.. Inawezekana hukumu hii imetaka kutoa fundisho
Mbunge wa ccm atapataje funzo hapa ukizingatia hata hayo makosa yaliyofanyika awali yote yalifanywa na wana ccm?
 
Mkuu mleta UZI hayo yote unayo yasema yametokea KIPINDI CHA ZAMA za yule MZEE WA WATU mliyekuwa mna muita DHAIFU ambaye leo hii mna MUONA ni HERO wetu na HAKUNA kesi ambayo ipo MAHAKAMANI juu ya HAO ULIOWATAJA mpaka sasa...na kama zingekuwepo ungeona ambacho KINGEWATOKEA kama wangekutwa na HATIA katika AWAMU hii.....KUKUSAIDIA tu AWAMU hii atuangalii mtu usoni...Mfano mdogo WE MSIKILIZE MKUU WA NCHI ASIVYO NA SONI juu ya watu wanaotenda UPUUZI....sasa msitake kuhararisha UPUUZI wa huyo MBUNGE kuwa alichofanya si KOSA.....SOMENI ALAMA ZA NYAKATI........kibaya zaidi WATANZANIA hatujui ni nini TUNACHOTAKA...tuna UNAFIKI...UVIVU...WA MBEA NA KUPENDA SANA VYA BURE.......ndio maana unakuta TOTO ZIMA LA KIUME NA NGUVU ZAKE LINA LIA LIA ETI MAISHA MAGUMU na hapo unamkuta amekaaa tu.....Mwisho wa siku wananunuliwa VIROBA na kuja KUANDIKA PUMBA HUMU
Huo uandishi gani?Jirekebishe maana unatia kinyaa kusoma!
Tatizo hapa lipo kwa wenye mamlaka ya kukamata na kushtaki mahakamani!Hilo liko wazi kuwa DPP na jeshi la polisi wanafanya kazi kwa maslahi ya ccm!
 
Mkuu Barafu......

Huyu kuwekwa tu ni Fulani kushikilia hiyo Uda.........

Wenye uda wanajulikana mkuu acha kujitoa ufahamu.........

Ni sawa sawa na zile sheli zilizojengwa nchi nzima na kupewa majina ya watu daaah ufisadi uliofanyika nchini kipindi hiki ni hatari sana ........

Swala la kiombewa ni mpumbavu pekee tu ndiye anaweza kumuombea mtu Mwenye visasi wivu wa maendeleo kwa wasio ccm na roho mbaya ........

Tupo wote tu hapa tuendelee kuwepo malipo ni hapa hapa duniani......
 
Hivi huyu wa Kilombero mlalamikaji alikuwa ni nani ? Labda wa Simiyu hakukuwa na Mlalamikaji
 
Mkuu mleta UZI hayo yote unayo yasema yametokea KIPINDI CHA ZAMA za yule MZEE WA WATU mliyekuwa mna muita DHAIFU ambaye leo hii mna MUONA ni HERO wetu na HAKUNA kesi ambayo ipo MAHAKAMANI juu ya HAO ULIOWATAJA mpaka sasa...na kama zingekuwepo ungeona ambacho KINGEWATOKEA kama wangekutwa na HATIA katika AWAMU hii.....KUKUSAIDIA tu AWAMU hii atuangalii mtu usoni...Mfano mdogo WE MSIKILIZE MKUU WA NCHI ASIVYO NA SONI juu ya watu wanaotenda UPUUZI....sasa msitake kuhararisha UPUUZI wa huyo MBUNGE kuwa alichofanya si KOSA.....SOMENI ALAMA ZA NYAKATI........kibaya zaidi WATANZANIA hatujui ni nini TUNACHOTAKA...tuna UNAFIKI...UVIVU...WA MBEA NA KUPENDA SANA VYA BURE.......ndio maana unakuta TOTO ZIMA LA KIUME NA NGUVU ZAKE LINA LIA LIA ETI MAISHA MAGUMU na hapo unamkuta amekaaa tu.....Mwisho wa siku wananunuliwa VIROBA na kuja KUANDIKA PUMBA HUMU
Mkuu ukitaka kutuaminisha hili ulisemalo unahalalisha uwepo wa Mkono wa mkulu ktk kufanikisha hii aibu ya awamu yake maana navyoelewa mahakama ni mamlaka inayojitegemea na haiko chini ya mamlaka nyingine. Kwanini hukumu kama hizi zisiwepo enzi hizo wakati mahakama ni hizi hizi tulizonazo.

Ama kweli namba zinasomwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom